Magulumangu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 3,047
- 452
Uzuri wa mtandao wa JF bwana ni ushauri mtu unaoweza kuupata.
Ushauri tu unaweza okoa maisha ya mtu.
Mimi ni mgeni sana JF lakini si mgeni wa maisha.
Nimepitia ukurasa huu ma mimi ninatizo linalo nisibu, tena tatizo linalonipa presha.
Mimi ni mjasiriamali mzuri tu kanda hii ya pwani.
Kuna dada ambaye kumbe ananifuatilia kwa karibu sana na kwa muda mrefu.Mwishowe akabisha hodi ofisini kwangu kama dada wa kutoka sehemu zetu huko milimani na akasema anasalimia tu.
Muda si mrefu simu zikaanza kuwa nyingi na hatimaye akaomba out.
Nisionekane mshamba masikini miye nikamtoa out. Kweli pombe mjumbe wa Ibilisi, muda si muda tukawa tunavunja amri ya sita na huyu dada akwa antaka sana kunimiliki.
Mimi nimeoa na yeye hajaolewa.
Mambo yakaendelea kwa muda kuidogo lakini nikakataa kabisa kujicommit na mabo yote ikawa kwa soksi ili isijetokea ajali ya mimba.
Nafikiri malengo ya dada yakawa hayajakamilika, na akazidi kuwa mkali kwangu kadri siku zilivyoendelea, ikiwa ni pamoja na vitisho kuwa ataniexpose kwa jamii kama nitamwacha.
Nikanwekea mtego siku moja , alipiga simu sikuipokea , lakini nikajidai mimi mke wa jamaa unyempigia.Nikamuuliza unashida gani na mume wangu maana nimesikia sauti ya kike.
Hapo yalianza matusi ya kuua mtu, matusi balaa-ati wewe ulicho nacho ndo mumeo anachofuata kwangu!
Hakika nilipigwa butwaa!
Siku ya pili nikamuuliza mbona ulibishana na mke wangu? naye akajibu, ati anajidai mjanja atanikoma mie!
Hapo ndo nikajua hapa kuna walakin na nika mwacha kwa muda mrefu.
Wanaume tuna matatizo sana, baada ya muda akanibembeleza na kulia sana, baadaye nikampeleka kinywaji tukanywa.
Punde si pundeikawa mechi tena isiyo na soksi safari hii.Bibie alifurahi sana siku hiyo, na akapotea zaidi ya mwezi.
Aliporudi akaja na stori kuwa yeye tayari.Nikamuuliz tayari nini, akaniambia mimba.
Nikachanganyikiwa kabisa lakini baada ya muda mrefu wa kufikiri nikamwambia nitamtafutia kiwanja ajenge ili mtoto asije pata taabu.
Lakini Mungu si Asumani, baada ya miezi minne kumbe mimba haikukaa na nikamuuliza vipi akaanza ukali tena ili mimba ikuzwe.Hapo nikakataa kabisa maana nikaona nimeponea tundu la sindano.
Kuona hivyo huyu bibi akawa kichaa na akaja ofsini nakutukana matusi ya mguoni , na nikaaibika sana.
Bibie akaahidi kunishitaki kanisani na kweli akaenda kumwona Mchungaji ,hata hivyo akapuuzwa kwa vile walimwona punguani.
Mambo yalipozidi kuwa mabaya akaanza kunisimamisha barabarani kwa nguvu, watu wantazama sinema na kushangaa!
Hapo ndo nikaenda fungua RB na kuwajulisha ndugu zake juu ya huyo mtoto wao.
Nilivyokuwa serious , aliwekwa ndani siku moja kwa kunibugidhi lakini ndugu zake wengine wakamwokoa na janga zaidi.
Wana JF hadithi ni ndefu lakini mwisho ndugu zake wakamkana kwa tabia yake na kusihi kutonisumbua na hii ni baada ya kuwalipa wazazi wake kifuta aibu cha kulala na binti wao(ana miaka 32).
Sijawasiliana naye(kwa maana ya kumpigia au kuongea naye) kwa zaidi ya mwaka sasa.
Lakini ka muda huo woote hadi leo ananipigia simu karibu mara kumi wiki na meseji kama kumi hadi ishirini kwa wiki ambazo sizijibu kamwe.
Kwenye simu yangu kama ushahidi nina meseji zilizofikia 831
Meseji ya mwisho imeingia kwangu kama nusu saa iliyopita.
Kwa hakika zinanichefua rohoni kupita kiasi.
Nsaidieni ndugu zangu huyu bibie anamapepo? na mnaweza nishauri nini?
lamba halafu kula kona njoo uombe ushauri tena...