Jamani hizi supplementary kwa finalists UDSM zinatutesa

Nilipokuwa hapo UDSM miaka ya themanini, tulikuwa tunatumia term system badala ya semester. Kati ya mambo ambayo sikupendelea wakati ule ni kwamba University Exam ilikuwa inafanyika mwisho wa mwaka baada ya term tatu na ilikuwa inahusisha mambo yaliyofundishwa mwaka mzima! Kule Engineering kulikuwa na masomo ambayo yalikuwa yanafundishwa mwaka wa pili na wa tatu kabla ya kupata University Exam, kwa hiyo mwanafunzi anakumbana na mambo aliyofundishwa miaka miwili iliyopita. Supplementary Exam ilikuwa ni kama lifeline pekee kwa mwanafunzi aliyefeli somo ambapo alikuwa anapewa miezi mitatu kujiandaa tena na kurudia mtihani aliofeli kabla hajalazimika kurudia mwaka wote ikiwa ni pamoja na yale aliyopasi. Tuliupigia kelele mfumo ule na leo nasikia kuwa higher education system yote Tanzania wanatumia mfumo wa semester.

Chini ye semester system, nina imani kuwa mwanafunzi akifeli somo anatakiwa arudie tena kusoma somo hilo alilofeli kwa semester nzima, siyo kupewa supplementary exam. Kama bado UDSM inatoa supplementary exam chini ya mfumo wa semester, basi wanawasaidia wanafunzi wao sana. Kwa vyuo vingi vya marekani hasa nilikosoma na nilikowahi kufanyia kazi, huwa hakuna kabisa kitu kinaitwa supplementary exam. Unafeli somo, basi inabidi ulichukue tena semester ijayo hadi utakapopasi. Kuna chuo kimoja kilikuwa na utaratibu wa kuonyesha lwenye transcript kuwa ulirudia somo mara ngapi.

Ni muhimu sana wanafunzi mnapokuwa mashuleni mzingatia masomo yenu na kupasi masomo yote bila kuchagua. As long as somo liko kwenye list yako, ni lazima ulichukulia kwa maanani sana somo lile na uhakikishea unalipasi bila kujali unalipenda au la. Kumbukeni kwa waalimu wote hupenda wanafunzi wao wapasi kusudi wafanikiwe maishani mwao, hasa kwa kutumia mambo waliyowafundisha. Binasi, niliwahi kukutana na mwalimu wangu aliyenifundisha hesabu form 2, na aliposikia kuwa wakati huo nilikuwa mwalimu wa engineering, aliita waalimu wenzake wote pale shuleni kuwatambia kuwa hesabu alizonifundihsa ndizo zimenifanye nami niwe mwalimu wa engineering. Kila mwalimu huona ufahari sana anapokutana na mwanafunzi wake wa zamani aambaye amefanikiwa maishani, na vile vile huona aibu sana kukutana na mwanafunzi wake aliyeshindwa mwaisha. Unapoona mwalimu anakukazania usome na kutaka upasi mtihani aliokupa kwa kiwango fulani, ni kwa sababu anajua kuwa hutakuwa mjuzi wa mambo aliyokufundisha bila kufikia kiwango hicho. Unapokuwa shuleni, zingatia sana shule yakeo. muda wako shuleni ni mfupi sana, miaka mitatu au minne tu; baada ya hapo utakuwa na muda wote kiuutumia upendavyo, kama utakuwa na bahati hiyo.

Kumbukeni tena, chuo kikuu siyo kama chooni ambako kila mtu anaweza lkwenda.
 
WanaJF tatizo la SUP UDSM ni kubwa sana zaidi ya tunavyolijadili!

nimependa ushauri uliotolewa wa kuwafatilia na kuwaripoti kwa daruso ili wafuatiliwe.....pia wajaribu kuripoti kwa seneti!

Nakumbuka kijana mmoja aliwahi kuja yupo full kachiz analalamika full sup....huko huko kwa sociology!ati wanasema wnainua kiwango cha elimu mmh kwa mwendo wa kushindana sup?!!

hata hao maticha wenyewe wengine wanashutuma kuwa waliingia katika nyadhifa hizo kwa kugawa na kutoa hongo afu wao wanajidahi wajuaji wa kutoa sup!

kisaikolojia ni mawili....mtu huyo anaweza kuwa madhubuti na kutojali na kuendelea na maisha yake angalau huyo sasa hatari ni pale atakapo kuwa na msongo ambapo wapo wengi yaani full frustrations kwani vitisho na ubabe wa kitaaluma hasa kutishia kugawa sup!

Ni hayo tu kwa leo nitarejea tena
 
naomba nitoe dukuduku langu kuhusdu hawa wasomi wa enzi hizi, ninaona hoja yako haina msingi ila inawezekana ina maana kwako ila it doesnt make sense wewe ulikua na coursework ngapi ya 40 maana hiyo pia ni indiketa kua kama utafaulu mtihani wa mwisho au la,

cku hizi wanafunzi wapenda kuzima moto yaani kusoma kwa kukremu tena karibu na mitihani kabla ya hapo wanazunguka tu mlimani city, steers mabibo na mjini kwa ujumla hawazingatii coursework ( assignments and homeworks seminar na quizes etc,
kumbe hawajui kua asilimia 80% ya mambo unayojibu ktk ue ni yale ambayo uliyasoma muda mrefu na yapo stored permenantly ktk medula yale ya kudonoa cku moja au 2 kabla ya pepa hayakai kichwani haya. mjifunze kusoma kwa techniques sio kupita kudonoa kama kuku.

halafu unadai mmekamatwa wengi 88 hata ingekua mimi ni huyo lecturer kama wajinga ni 3000 nakamata wote nifanyeje?
tafakari haya ujione ww ulikua kundi gani?
 
Mimi hapo naona ni mawasiliano dhaifu baina ya mwalimu na wanafunzi. Yes ni kweli wapo wahadhiri pale mlimani wana hako katabia, sina hakika na sasa ila ule wakati wetu walikuwepo. Kuna mdau mmoja alipigwa ndevu chini eti kisa tu mwalimu na mwanafunzi wail beam same focal point.
Lakini ndio hivyo kunakuwa hakuna oversight ya kueleweka kwa wakufunzi wetu kwani wanajiona kama miungu mtu. Mbali na wanafunzi kuwa na uzembe wao, kila muda fulani ingekuwa bora kama walimu wangekuwa wanafanyiwa evaluation then walipwe kutokana na performance. Lakini nalo litakuja kuwa shida ya kuwa na wahandisi wa magorofa yanayoanguka ovyo nchini.
All in all, ningeshauri kuwe na kaoversight fulani ili mwalimu naye ajione anatakiwa kuwajibika katika performance ya darasa.
 
Jamani tusipnde kulaumu bure please inawezekana ni kweli tatizo liko kw awalimu but hata wanafunzi wa siku hizi ni kuwalaumu.. jamani SIKU HIZI WATOTO HAMSOMI kwa wasichana wamekalia urembo tu na kushindana leo nitavaa pedo gani.

Ni kweli hamsomi tena hasa wanaosoma Sociology huko aliko Mwami mnaemlalamikia hamsomi kwa kuwa mnadai kuwa sociology ni saluni course eti unaweza kusoma huku unapaka rangi ya kucha au unaroll nywele na ukafaulu!!

Lugha mbovu mtu anajibu swali hata hajui anajibu kitu gani
Mtu swali la essay type anaaandika one or two paragraphs??
Take home assignment mnadeseana one assignment inakuwa submitted na watu wa4 au hata wa 5 wanabadilisha ile page ya juu tu jina na registration number- Hata ningekuwa mimi ningekamata tu.

Tatizo ni kuwa waalimu wa department ile sasa wameamua kuinua sifa ya idara yao kwa kuwa strict na ndio maana mnaona madesa hayafanyi kazi tena so kwa wale wanaotegemea madesa chaliii


Tutizame pande zote
 
miwaya hata wlio nje wanapata ila swala la msingi ni elimu inaelekea wapi tutakapokuwa na walimu wa kufelisha..je tutafikia malengo kwa kufelisha..isitoshe kama hao madr ni wazuri wamefanya nini cha ziada tokea uhuru...au wanajifariji kwa kukamata.
 
Jamani tusipnde kulaumu bure please inawezekana ni kweli tatizo liko kw awalimu but hata wanafunzi wa siku hizi ni kuwalaumu.. jamani SIKU HIZI WATOTO HAMSOMI kwa wasichana wamekalia urembo tu na kushindana leo nitavaa pedo gani.

Ni kweli hamsomi tena hasa wanaosoma Sociology huko aliko Mwami mnaemlalamikia hamsomi kwa kuwa mnadai kuwa sociology ni saluni course eti unaweza kusoma huku unapaka rangi ya kucha au unaroll nywele na ukafaulu!!

Lugha mbovu mtu anajibu swali hata hajui anajibu kitu gani
Mtu swali la essay type anaaandika one or two paragraphs??
Take home assignment mnadeseana one assignment inakuwa submitted na watu wa4 au hata wa 5 wanabadilisha ile page ya juu tu jina na registration number- Hata ningekuwa mimi ningekamata tu.

Tatizo ni kuwa waalimu wa department ile sasa wameamua kuinua sifa ya idara yao kwa kuwa strict na ndio maana mnaona madesa hayafanyi kazi tena so kwa wale wanaotegemea madesa chaliii


Tutizame pande zote
tukubali yafuatayo;

1. kama vijana hawasomi, basi na walimu hawako serious, maana inawezekana je mamia ya walimu wakawapa alama nzuri isipokuwa Mwami na Karamagi? na kama ndio hivyo, basi chuo katika department ya sociology, baada ya hayati Chachage kututoka, amebaki Mwami tu, anayekamata wanafunzi waliowengi na walimu wengine hawako serious.


2. kama vijana hao wanasoma, basi nadhani hao walimu waliowakamata ndio wenye matatizo, kati ya walimu wote waliochuoni hapo kwa sociology.


ZAMANI ILIKUWA SHERIA IKIONGOZA KWA KUKAMATA SASA HIVI WAMEJIRUDI?
 
tukubali yafuatayo;

1. kama vijana hawasomi, basi na walimu hawako serious, maana inawezekana je mamia ya walimu wakawapa alama nzuri isipokuwa Mwami na Karamagi? na kama ndio hivyo, basi chuo katika department ya sociology, baada ya hayati Chachage kututoka, amebaki Mwami tu, anayekamata wanafunzi waliowengi na walimu wengine hawako serious.


2. kama vijana hao wanasoma, basi nadhani hao walimu waliowakamata ndio wenye matatizo, kati ya walimu wote waliochuoni hapo kwa sociology.


ZAMANI ILIKUWA SHERIA IKIONGOZA KWA KUKAMATA SASA HIVI WAMEJIRUDI?

Sheria ilikuwa kwa "MANGWINI" ndio inaongoza ili kwa chuo kizima ENGINEERING ilikuwa ni mauaji. maana jamaa walikuwa wanapukutishwa kinoma, Ila nasikia sikuhizi wamelegeza maana mpaka na wanawake wapo wengi tu. zamani wanaume 80 wanawake 3 darasa moja.
 
ndugu yangu nimekusikia ila kwa wakati huu pakuanzia ni kwenda kufanya hiyo supplementary then ukaonane na ma DR pale UDASA uwaeleze kwa kina yanayowasibu wakati mwiingine malalamiko huwa hayawafikii wanaoweza kusaidia kwa heshima na taadhima pale kuna watu wanaofikiri na kaumini panapo haki watumie hao
pia washauri wadogo zako kuwa wawe wanaomba kuwa na Faculty Baraza kama nilivyosikia wanafunzi wa Bcom walivyofanya kwa kuwaeleza dean na associate dean yanayowasibu kwenye mitihani huenda ikasaidia
 
ndugu yangu nimekusikia ila kwa wakati huu pakuanzia ni kwenda kufanya hiyo supplementary then ukaonane na ma DR pale UDASA uwaeleze kwa kina yanayowasibu wakati mwiingine malalamiko huwa hayawafikii wanaoweza kusaidia kwa heshima na taadhima pale kuna watu wanaofikiri na kaumini panapo haki watumie hao
pia washauri wadogo zako kuwa wawe wanaomba kuwa na Faculty Baraza kama nilivyosikia wanafunzi wa Bcom walivyofanya kwa kuwaeleza dean na associate dean yanayowasibu kwenye mitihani huenda ikasaidia

Karibu jamvini Masoud,

Ila kumwambia aende UDASA ni kumwambia akawanunulie Dons pombe ili apate ubwete, au kama ni "KE" ajaribu kale kamchezo ka kwenda ofisini na kimini, huku kajilemba na kubana sehemu za kifua huku kidogo zikichungulia na kulembualembua na kumbeleza lecturer kwa sauti ya kuchombeza, ila afanye hivyo wakati Lecturer yupo peke yake ofisini ajipulizie na ile perfume ya kuamsha hisia fulani, huenda anaweza pass Supp hata kabla ya kuifanya, kanalipa sana kamchezo haka na wengi wamekatumia we uliza tu
 
Kweli wanafunzi wanaweza wakawa na matatizo lakini amini usiamini si wote bwana....pia jiulize ni kwanini mwanafunzi huyo huyo ukiangalia matokeo yake masomo mengine nje ya idara vimeo amefanya vyema?

Inshu ya kuwa na coursework nzuri hasa katika idara jadiliwa ni soo hapa huwezi kuepuka coursework uchwara wakati mwingine endapo mwalimu anaonyesha nia fulani ya kurudi na watu...mtu kama mose hadi anafikia hatua ya kukopesha ili watu waingie kufanya pepa!!!na si vijana hawasomi ingawa vilaza wapo wachache lakini!

Idara hii ukitaka kujua inawalakini we ilinganishe hii na hata angalau ile ya Political Science "PSPA" kwa walimu hawa jamaa wana ma Prof wa kutosha...madaktari...hawa ma MA holders wengi tu kama ma assistance lakini ingia sociology hata hao ma Prof unahesabu yaani kubaniana hadi huku juu ya wana masters na PHD!

Jus imagine mtu unafanya masters wanakupa mtihani wa fill in the blanks ambao sasa umeingia sana pale idara ya sociology yaani pepa zinakuwa za kujaza sehemu iliyoachwa wazi staili ya shule za msingi kwa essay ni wachache sana ati sababu oohh..wanafunzi wengi wanashindwa kusahihisha so fill in blanks inakuwa suluhisho kwao walipue fasta watimue zao kwenye tafiti!

Nature hata ya mfumo wa mitihani inakuwa balaa....pia kuna walimu wameshazeeka sana hadi duuuhh..mtu kama Dk.Masanja yaani anaboa mpaka basi watu wanavumilia tu lakini kipindi kizima ticha haeleweki ukija full makarai ama kukamata madogo!

am sure baada ya muda vyuo kama Dodoma ambavyo wamekubali kuwahukua madogo wapya katika fani ya ualimu vinaweza kuwa bora sana kwa uzalishaji wa wanafunzi wazuri na UD itaendelea kubakia title tu!

Nakumbuka kijana Bashiru aliwahi kusema mwalimu anayejuvunia amekamata vichwa vingi huyo hajue ethics za ualimu kwani hapo yeye ndiye mjinga kwani hiyo ni indicator ya yeye kutoeleweka sawia kwa wanafunzi wake!!
 
Kwa nini usiombe ukawa mshauri wa wanafunzi. Nimependa mawazo yako sana. vijana wetu ebu someni huu ushauri wa bure, Utawasaidia.

Niseme kidogo tu, Kwa sasa vyuo vyetu tusifichane wanafunzi wamepageuza vijiwe vya umalaya, kuvuta unga na uhuni mwingi sana. Ukiacha kusoma then ukakamatwa kwenye somo fulani huoni kama ni halali yako? tusikimbilie kulaumu waalimu. Pia waalimu wenye chuki binafsi punguzeni lakini hasa ziacheni chuki hizo tunahitaji watalaam. Pole kama umeonewa lakini itakuwa bora kama umefail kwa uzembe wako
 
we kweli unaweza kuwa umesema kitu lakini shida unatoka kwenye idara hiyohiyo lakini hiyo si tatizo ila kama wewe ud product umekubali kuwa vyuo vingine vitafanya vizuri kuliko ud basi unauwezo wa kufikiria kidogo;ANGALIA VYUO KAMA DIT WANAFANYA MAMBO YANAONEKANA SIO KAMA WENZETU WA MLIMANI WANABAKI KUSEMA STATE UNIVERSITY kumbe ndo wanakufa taratibu angalia pia SUA wanafanya mambo angalau lakini MLIMANI unasikia eti tuna mtaalamu wa nyuklia na je huyu amefanya nini?eti tuna wachumi kama KARAMAGI furaha yake kukamata...Eti tunawanasheria akina KABUDI furaha yake kudhalau vitivo vingine kama anajua sheria za mazingira mbona majangwa yanaongezeka na wengine kama MAJAMBA........
 
Au mwandiko? make hawa watu siku hizi walishachoka na kazi. mwingine anaona nilazima abalance kwani asipokamata watamuona hana sifa za kupata PhD kama ndo bado anaitafuta.
nyie wenyewe jiulizeni kwa nini maprofessor huwa hawana matatizo mengi na mitihani yao.tena unaweza kupata A mtihani wa professor na kajamaa kenye master kwenye course hiyohiyo kakakung'ang'ania.
wengine ni kasumba kama yule jamaa wa uchumi hapo mlimani nisha msahau jina. Kenya waliomba mwalimu wa uchumi hapo UD Akaenda jamaa walimkataa sisi tulipona kuangukia mikononi mwake.
kuna mwingine anaitwa Mbamba wa FCM yule jamaa anasaisha kwa kubuni na pengine miandiko.
we jipe moyo supp ni kama ajari
 
Kweli wanafunzi wanaweza wakawa na matatizo lakini amini usiamini si wote bwana....pia jiulize ni kwanini mwanafunzi huyo huyo ukiangalia matokeo yake masomo mengine nje ya idara vimeo amefanya vyema?]
Kama mtu ana uhakika na alichokifanya kwani chuo hakina utaratibu wa ku-appeal? Nasikia gharama yake ni kidogo tu kuliko kukaa na kulia lia pembeni. Otherwise soma ufanye hiyo supp ufunike ile mbaya mpaka mwalimu aone kuwa kulikuwa na tatizo. Kingine ni kuwa mitihani inapitiwa na watu wengine wa nje au utaratibu umefutwa siku hizi?
 
sijui kuna walakini gani katika michango yangu maana kila nikichangia mjadala huu thread yangu inatolewa .....vp JF lakini?!

Okay itanibidi niweke tena baadhi ya maoni;
1.mwalimu anayejisifia kufelisha si mwalimu bora kwani hajafikia objective ya kuelimisha watu wake!lengo la kufundisha ni ueleweke na si vinginevyo!

UDSM kweli kuna tatizo hilo na wakati mwingine si wanafunzi sana wa kulaumiwa kwani waalimu ndiyo wamuzi wa mwisho wa namna ya kuielekeza elimu.

Nilitazama gazeti wiki iliyopita na kwenda moja kwa moja katika idara hiyo mmh nikaona ni mwendo wa SUP tu duuhh..yaani kuna jambo hapa maana si kawaida.....!! ni tofauti sana na hata idara nyingine kama ya PSPA ambayo ayo ilikuwa tishio kipindi flani.

Sociology wanatatizo la msingi;
1. Nature ya mitihani wanayotoa si standard ya kichuo kikuu yaani kutoa mitihani ya fill in the blank katika level ile ni aibu tupu!!hilo ni tatizo yaani kisa wingi ndo kusababisha kutoa mitihani ya standard ya darasa la kwanza?eti wawahi kwenda kufanya research na kuacha taaluma!?

haki anani wasipo kuwa makini in no time vyuo kama Dodoma nk vitawapita wabakie na jina tu!
 
Tazama safu ya walimu ndani ya socioligy....mungu wangu yaani ni tofauti sana na idara nyingine....kuna uhaba wa walimu sana mfano Maprof hawazidi watatu na madaktari wachache sana sasa nenda idara kama PSPA, geography utashangaa kwani kuna idadi ya maProf ya kutosha mpaka kusaza, madaktari ndo usiseme!

si wote wanaotaka kusoma pale wanatarget kuwa malecturers so nini kubania watu coz ndo inshu wao wanadhani wanakuja kuporwa nafasi zao....!

we angalia hata first year hadi final ukiangalia kwenye gazeti utaona full SUP hapo kuna tatizo!
 
Pole kwa yaliyokusibu. Kama una uhakika ulifanya mtihani huo uliokamatwa kwa umakini na ukawa na uhakika wa uliyoyaandika, ninakushauri upeleke/mpeleke malalamiko yenu kwa chuo UDSM kupitia chama cha wanafunzi DARUSO ili answer sheets za wote waliokamatwa zisahihishwe upya na mshauri hiyo kazi ya kusahihisha upya apewe mwalimu mwingine na si huyo aliyewakamata


MHACHE WAZO ZURI ILA UKIMWAMBIA MWALIMU IFANYIKE HIVYO HATOFUNDISHA TENA NA NDUGU YETU VC ANAVYOWAOGOPA HAKUNA KAMA HICHO
 
Nakumbuka kijana Bashiru aliwahi kusema mwalimu anayejuvunia amekamata vichwa vingi huyo hajue ethics za ualimu kwani hapo yeye ndiye mjinga kwani hiyo ni indicator ya yeye kutoeleweka sawia kwa wanafunzi wake!!


OOOOOOOOHHHHHHHHHHHH UR RIGHT

ULIKUWA WAPI ????????????????????????????????????
 
Pale Chuoni Kuna Mambo Mengi Sana Ya Kufanyia Kazi Kama Huyu Vc Anapenda Kile Chuo

1))))ake Na Maprofesa Wake Na Kuwahakikishia Paper Si Njia Ya Kuwapata Wanake Pale Chuoni

2))akae Na Wanafunzi Wote Awahakikishie Kufaulu Si Lazima Utembee Na Profesa Au Dk Yoyote Na Sasa Hivi Mpaka Tutor Nasikia Unamvulia Chupi

3)))awahakikishie Profesa Mitihani Si Sehemu Ya Kuwaongezea Mapato Yao
Ya Kila Siku Kama Walichelewa Muda Wote Hivi Sasa Wafunge Mkanda

4)))awahakikishie Wanafunzi Kwamba Atakuwa Wazi Kuonyesha Mitihani Iliyosahahihishwa Kama Kutatokea Malalamiko Kwa Profesa Na Mwalimu Na Kukubali Kutoa Nafasi Kwa Mwalimu Mwingine Asahishe Bila Mhusika (mwl Kujua Nani Anahusika

5))awatanagzie Walimu Wake Kufaulisha Wanafunzi Si Njia Ya Kujulikana Kwa Watu Nafikiri Hiyo Itawakomesha Kabisa

6))ndugu Zanguni Hakuna Malalamiko Yatakayotokea!!!labda Nije Kwenye Mada Kikamilifu Niliona Hyo Mada Nkafwatilia Sana Na Mwisho Nikaenda Kwa Mguu Pale Udsm...kama Nilivyonukuu

Kipengele ....1

Hilo Ndilo Tatizo La Huyo Mkuu!!!!!ila Kuna Mengi Tu Ya Kuongelea
Kwa Leo Ni Hayo Tu
 
Back
Top Bottom