Jamani hizi supplementary kwa finalists UDSM zinatutesa

Jamani hizi supplementary kwa finalists UDSM zinatutesa

Suala la walimu kuwachoa vyupi madenti ili wawafaulishe halina ubishi udsm......suala la wanafunzi wa udsm kuwa wavivu wa kutafiti,kujisomea halina ubishi.....suala la utawala wa kimla udsm halina ubishi.....suala la kutoa vihiyo udsm halina ubishi.......SOLUTION?
 
Ni kweli kuna tatizo kubwa sana na nadhani hatuwezi kulifafanua kwa kuangalia idara husika peke yake.
1. Utaratibu wa ku-appeal kama kweli umeonewa upo- tena siku hizi unapoappeal mnaitwa na mwalimu husika thenm unakuwana uwezo wa kumuumbua kama amekufelisha kwa kunyimwa chupi. Taratibu ni kuwa unaandika barua ya kuappeal ukiombwa mtihani wako usahihishwe upya na mara nyingi huwa anayerudia kusahihisha si mwalimu yule bali ni mwingine.
2. Kabla matokeo hayajatoka kwa wanafunzi kuna utaratibu wa ma-external exerminers kupitia mitihani yote ya wanafunzi. Zamani ilikuwa hivyo bali kutokana na wanafunzi kuwa wengi esp Sociology na ukweli wa muda wanaokaa hawa ma-external kuwa mfupi basi huchukuliwa zile paper zote zilizopata As na zile zilizofanya vibaya na baadhi (sample) ya zile za kati ndio ambazo External anazipitia. Akiona ambayo imesahihishwa kimakosa anairemark then anaweka Grade yake pale na usually kazi ya walimu idarani ni kuaccept comments za External ikiwa ni pamoja na kubadili grade zilizobadilishwa na External.
3. Ni makosa kwa chou na level ya Masters kutungiwa fill in the blanks mtihani. Hii ni kwa sababu Master wanafunzi si wengi so hoja yao eti wanatunga hiyo ni kwa sababu ya wingi wa wanafunzi haihold water- Hivi kuna darasa la masters lenye wanafunzi 100 kweli? Maana hiyo ndio idadi ambayo ninawezakufikiria mtu unaweza kuanza kulalamikia ukubwa wa darasa na si pungufu ya hapo! Fill in the Blank kwa Matsers ni kuua kiwango cha Elimu ya juu.
b) Kwa undergrads- si sawa but kwa mwalimu ambaye darasa lake lina wanafunzi zaidi ya 1200 ( am talking about ile kozi ya wote ya research Methodology) au kwa sociology sijui (introduction of Sociology) au kozi yoyote ambayo wanafunzi wake wanazidi 1000 na mwalimu anayefundisha ni mmoja. Na mbaya zaidi mwalimu huyo anapewa ONLY TWO WEEKS awe amekwishasahihisha scripts zote na kurecorde grades! What do you expect? Atawezakweli kutunga essay types and awaruhusu wanafunzi wajaze scripts? Ataweza kweli kuzisahihisha within the GIVEN time na kuwa makini? Kama si kuanza kumtaka abuni marks kutokana na mwandiko wako?
c. Mwalinu huyo huyo atajilinganisha na mwalimu ambaye ana darasa lenye wanafunzi 30 tu. Mshahara wanalipwa sawa kama wako rank moja na hakuna incentive yoyote (Kama Mzumbe au SUA- ya kulipwa kwa idadi ya extra scripts). Morale wa kujitesa atapata wapi wakati mwenzake (mwenye 30) akimaliza kumark anaruhusiwa kwenda kusaka pesa kwenmye tafiti............. Obvious na yeye atatafuta njia ya kumharakishia aende akatafute tafiti so atatunga fill in the blanks!!

4. Nafikiri ni jukumu la UONGOZI wa MKANDALA kuangalia tatizo hili na kutafuta suluhisho na si kukazana kuongoza idadi ya wanafunzi bila kuangalia waalimu kama wanatosha au la.

N.B:
Tusiangalie upande mmoja wa shilingi eti mwanafunzi huyo huyo aliyefeliutakuta ana A kwenye somo la mwingine- Huwezi jua inawezekana huyo aliyempa A ameamua kugawa tu kwa kuwa alitaka amalize upesi na hakusahihisha kwa umakini au ana kaupendeleo fulani kwa huyo mwanafunzi ( huwenda pia kwa vile ni Professor mwanafunzi alimkubalia matakwa yake!! You never know

But inapotokea the same mwanafunzi amefaulu katika masomo karibia yote na only moja ndio kafeli na anahisi kuwa kafelishwa then uwezekano wa kuwa kafelishwa huwa ni mkubwa

Aksanteni
 
Jamani huku mlimani kuna DR mmoja wa Sociology (jina lipo) amekuwa na tabia ya kukamata wanafunzi wengi sana hasa finalists. haina maana hawasomi ila ni kama kuwakomoa tu. mfano mzuri ni mwaka huu kakamata wanafunzi 88 kati ya wanafunzi 190. mimi pia ni mwathirika na nilikuwa nasoma sana kwa kadri ya uwezo wangu. masomo yote nimefaulu vizuri ila yeye tu ndo kanikamata. naombeni tushauriane kwa hili kwani sasa niko mkoani sins kazi, je hiyo naulu ya kuja kufanya supplementary nitapata wapi? maisha yamshakuwa magumu ndugu zangu. aksanteni

Pole sana Sipo, kwa mambo anayofanya huyo Dr was Sociology. Ni kweli baadhi ya lecturers wana majivuno na wanafikiri kum'felisha' mwanafunzi ndiyo kutukuka kwao. Ni ujinga tu!

Rafiki yangu mmoja ni lecturer hapo UDSM. Naye ni Dr lakini ni 'fair'. Huwa ananiambia lecturers wenzake wanamlaumu kwa vile wanaona kwenye masomo yake wanafunzi wanapata maksi nzuri. Walikuwa wanamshinikiza naye aanze kuwapa maksi ndogo ili aonyeshe 'solidarity'. Ila aliniambia, yeye hawezi kufanya upuuzi huo kwani anatoa maksi kulingana na jinsi mwanafunzi anavyojibu au kufaulu kuliko wenzake wanavyotaka afanye. Nami nilimsihi asilegeze msimamo.

Huyu Dr (rafiki yangu) tulisoma kwenye mazingira yanayofanana. Masomo yalikuwa magumu sana na mengi, ila yanayojenga uwezo wa kufikiri na kufanya uamuzi sahihi.

Kwa upande mwingine, wanafunzi wengi wanataka kusoma bila kuhangaika. Wanataka ikiwezekana wafundishwe majibu ili wapate maksi za juu. Walau mimi sikusoma katika mazingira hayo. Mfano, walimu wetu walikuwa wanakazia zaidi uelewa wa mtu kuliko maksi. Mfano, mwalimu anaweza kutoa swali ambalo halina jibu moja na anataka maelezo yako ndiyo yafanye akupe maksi nzuri kuliko kujua, mfano, maji yanachemka katika nyuzi ngapi usawa wa bahari.

Kusoma kwa kukariri majibu ndiko kunakoleteleza wanafunzi wengi washindwe kufanya vizuri kwenye masomo yao. Ningekuwa mwalimu wa chuo kikuu, hakika wanafunzi wangu wasingeshindwa. Chuo nilichosoma mimi (siyo hapa Tz, of course) katika mwaka wetu lowest ilikuwa BA (Honours) ya 2.2. Hakuna aliyepata chini ya hapo. Ila wa first class - haikutegemea tu maksi za darasani lakini pia jopo la walimu ambao licha ya maksi waliweza kujadili kama kweli mwanafunzi fulani anastahili first class.

Cha kufanya katika nchi yetu, hasa katika vyuo vyetu ni kubadilika wote - wanafunzi na walimu. Yaani, namna yao ya kufundisha ibadilike kabisa na vilevile wanafunzi wabadilike katika kujifunza. Sisi mwaka wetu wa 1 tulifanya 'memory test' ili kujua mwanafunzi ana uwezo kiasi gani wa kukumbuka katika masomo magumu na pia rahisi. Baadaye tulipata ushauri kulingana na 'performance' ya kila mmoja wetu - kujua strong na weak points za mwanafunzi.

Kwa bahati mbaya sana, katika vyuo vyetu hakuna huo mpango na pia wanafunzi hawajifunzi 'study methodology'. Mimi nilipoanza mwaka wa kwanza, tulifanya 'induction week'. Yaani, unapata 'introduction' ya kila facility chuoni kabla ya kuanza rasmi masomo.

Muda huo ilikuwa inaruhusiwa pia kubadilisha masomo, hasa baada ya kupata 'introduction' ya kutosa kuhusu 'programmes' zinazotolewa chuoni. Pia, pamoja na masomo tuliyokuwa tunafundishwa, ilibidi tuendelee kujifunza lugha - Kiswahili (kwa wale wasio kifahamu vizuri), Kifaransa na Kiingereza na pia lugha ya watu waliotuzunguka.

Hali hii ilinipa mwanzo mzuri katika elimu na hadi sasa bado najiendeleza kwa kununua vitabu na kusoma mwenyewe. Sasa hivi nachukua masomo ya sheria, lakini hata kama nashindwa kuhudhuria tuition, najisomea nyumbani na napata maksi nzuri zaidi hata kushinda wale wanaohudhuria tuition.

Kwangu kuibiwa mtihani ni kufanya 'intellectual masturbation'. Kwa kifupi, kuanzia elimu ya sekondari nilijitahidi kujifunza peke yangu bila kumtegemea mwalimu. Siyo kwamba nawadharau walimu ila nasema kwamba hata kama mwalimu hafiki darasani bado nasoma mwenyewe na kuelewa.

Nilikuwa najitahidi kusoma chapter moja zaidi ya wenzangu katika kila somo na hii iliniwezesha kufanya kama marudio wakati mwalimu alipokuwa anafundisha.

Mtu mwingine anaweza kufkiri mimi ni genious, la sivyo. Mimi ni mtu wa kawaida tu ila nimejiendeleza sana katika kutafuta njia mbalimbali za kujifunza karibu katika kila mazingira (including concentration skills).

Nilijizoeza, mfano, wakati nafanya kazi library kuazimisha wanafunzi wenzangu vitabu bila kuandika majina yao na nilijua nani kaazima nini, tarehe gani na anatakiwa kurudisha nini. Inanisaidia pia mtu akikopa hela kwangu siandiki kwenye daftari ila nitaweka kichwani tu na kujua ni kiasi gani na tumekubaliana arudishe lini.

Kwa kifupi, Mungu ametujalia vipaji vingi sana na inabidi tu'explore' talents zetu na kuzitumia. Mara nyingi tunakata tamaa tukiona mambo yanakuwa magumu. Anza leo kujitahidi na utaona utakuwa na mabadiliko mengi tu katika masomo yako na katika maisha yako pia.

Jitahidi kujifunza mambo mengi kwa muda mfupi na utaona unafanikiwa! 'Programme your brain and you'll see wonders' na hata utaweza kuwaelimisha watu kama hao akina Dr wa Sociology. Sisi bwana tulikuwa tunasoma na hata kukosowa walimu katika uelewa. Yaani, mtu aki'argue' hata mwalimu haoni ndani.
 
Tatizo bongo..ticha akikupa mtihani ukifeli anafurahi..anasema hamumuwezi yeye ni hodari kutunga mitihani.......sidhani kama hali hii utaweza kuipata katika univesity yeyote duniani..ni Bongo tu....
 
Hivi KARAMAGI bado yupo???? maana ni mpuuzi kuliko walim wote waliopata kunifundisha,,,,akiingia tu siku ya kwanza anawatajia idadi ya watu atakaokamata mwisho wa mwaka..

(i)Karamagi
(ii) Prof Osoro
(iii) Ndoroi

Hao juu wanamakusudi nina mashaka na taalluma yao
 
kawaida mwadhiri chuo kikuu, msaada wake kwa mwanafunzi ni 15% na zinazosalia unajitafutia, JE, huko inakuwaje?

uku ni spoon feeding at 25/75.......................+++hata ukilala unatafuta elimu huku labda tujaribu mwakani====uko mnapotafutaiwa 15 lazima litukule.
 
Supplimentary ni mitihani ya kawaida tu! kaka anahaha kwa sababu amezoea kufaulu tangu aanze shule. Halafu anazungumzia sup. mia moja na ushee wakati EC 216 (Intemidiate microeconomics I)na EC 226 Intermidiate microeconomics II) unazungunzia sup 290 na 400's respectively (Dr. Karamagi na Prof. Osoro)!
Hayo ndo maisha, but i know the grounds for your complains!

usimusingizie prof.osoro bwana yeye afadhari, sasa la kushangaza akina karamagi mlimani hawataisha kuna kijana mmoja anaitwa joel office moja na karamagi si kawaida.
 
Watoto someni acheni kulalama ama.............
"Mtu akishaonja kitu ndo ujua utamu" watoto wanasoma mpaka kuche lakini hola we kama sio sisiemu basi tuitorial assistant(TA),,na kama wewe uko hivyo basi unaidanganya nafsi yako...mana mi nirishuudia prof akipishana na TA kuwa ametoa A's nying hivyo apunguze hizo A's ila MWENYE MACHO AAMBIWI TAZAMA
 
Pole sana Ila kusoma sana sio sababu ya kufaulu, unaweza kuwa ulikuwa unasoma sana magazeti ya udaku badala ya relevant material. Pia hutakiwi kuwa na haraka na kukariri, fikiria mitihani ipo ili kupima uwezo wa kufikiri na si ku memorise, Pia fanya proof lead ukimaliza kuandika mtihani sio unakimbilia kutoka nje na kusheherekea umemaliza shule, usifanye makosa kama uliyofanya hapa kwenye kuandika thread, fanya kazi. Kusoma ni kazi sio kuendekeza kusuka nywele/ au kufukuzia freshers kwa ticket wewe ni finalist.
fact
 
Mmh aisee huu uzi ni wa enzi aiseeee
 
Back
Top Bottom