Msongoru
JF-Expert Member
- Apr 16, 2008
- 306
- 24
Na Samson Mwigamba
NAAM! Nimetaja Spika Sitta Group kwa kuwa si peke yake. Kuna kundi la wanachama wa CCM wanaoishi ndani ya CCM lakini kwa mtazamo wa juu juu wakionekana kana kwamba hawatendi matendo ya CCM. Ni kama vile wanatimiza ile kauli ya Yesu, aliyowaasa wafuasi wake kwamba waishi ndani ya ulimwengu lakini wasitende ya walimwengu.
Ama wachangamane na watu wa mataifa lakini wasitende matendo ya mataifa. Ndivyo mtazamo wa juu juu unavyoweza kuwaonyesha hawa wana mtandao mpya ambao nimeupachika jina la Spika Sitta Group (SSG). Ndani wamo akina Harrison Mwakyembe, Anne Kilango Malecela, Lucas Selelii, Christopher Ole Sendeka, William Shelukindo, Said Nkumba, Lazaro Nyarandu, n.k, hawa ni wachache kwa idadi.
Mapema mwaka jana, Richmond ilitegeka. Ikaanzia kwenye Kamati ya Biashara iliyokuwa ikiongozwa na William Shelukindo na baadhi ya wajumbe wake akiwemo Dk. Mwakyembe, ikadaiwa baada ya miaka mingi kwamba ni muhimu sasa kuundwa kwa kamati teule ya bunge ya kuchunguza mkataba wa Richmond. Bunge lote likaridhia na hatimaye kamati ikateuliwa. Majina yakawa ni yale yale yaliyotarajiwa Kazi ikawa ni moja, kumtafuta mchawi wa Richmond.
Napenda nieleweke wazi mapema kabisa kwamba, katu katika makala hii silengi kuwatetea mafisadi wa aina yoyote ile. Wasomaji wanaonifuatilia sana ni mashahidi. Nimetumia nguvu nyingi mno kupiga vita ufisadi wa aina yoyote.
Kupitia kalamu hii nimetamka maneno mengi yenye kuhatarisha maisha yangu kiasi cha wasomaji wengi kunitumia ujumbe wa kuniuliza Hivi Mwigamba huogopi?. Na kwa kupigana vita dhidi ya mafisadi, mara kadhaa nimetishiwa kushtakiwa mahakamani, achilia mbali vitisho kutoka kule kwenye jumba jeupe. Nawakumbusha pia wasomaji kwamba nilishaapa kwamba hata kama kwa sababu yoyote ile nitaacha kuandika leo, bado nitaendelea kupigania haki ya mnyonge wa nchi hii.
Lakini wakati nikiwa na msimamo mkali kiasi hicho dhidi ya mafisadi, nawatangazia pia vita watu wa aina yoyote ambao hujifanya kupigana vita dhidi ya ufisadi wakati wakiwa na ajenda yao ya siri ya maslahi binafsi.
Hawa nao dhamiri ya moyo wangu inanituma kuwatangaza kwamba nao ni mafisadi. Yaani wanazo sababu binafsi za kuchukiana na fulani na kwa kweli wakipata fursa ya kum-fix wanamfix kweli kweli lakini huku wakitangaza kwamba ni kwa maslahi ya taifa.
Huu pia ni ufisadi na ni ufisadi mbaya kuliko. Bora ule ufisadi wa moja kwa moja maana ni rahisi kuugundua na kuushughulikia kuliko huu wa kuvaa ngozi ya kondoo kumbe ndani mbwa mwitu.
Baada ya dokezo hilo, naomba turejee kwenye mada yenyewe hasa. Kama wewe ni mtunza kumbukumbu mzuri, utakumbuka kwamba bunge jipya lilipoapishwa tu, Spika Sitta aliongoza jopo la wabunge wenzake kadhaa kudai nyongeza ya kile ambacho wao hukiita posho za wabunge na kuziepusha na kodi ya serikali wakati kimsingi ni kubwa mara elfu ya mishahara ya watumishi wengi wa serikali na sekta binafsi ambao hulipia kodi mishahara yao.
Hatimaye sakata hilo likaisha kwa Sitta kukosana na baadhi ya wanahabari kwa kurusha hewani pilikapilika zao za kudai nyongeza ya mafao hata kabla hawajaanza kazi. Hii ni sehemu ya sura halisi ya Sitta anayedai kupigana vita dhidi ya ufisadi.
Lakini pia wenye kumbukumbu watakumbua kwamba Richmond (ile kampuni feki ya kufua umeme wa dharura), iliingia mkataba na serikali mapema mwaka 2006. Na baadaye ikaonekana dhahiri kwamba ile kampuni ilikuwa imetuliza Watanzania kwa ajili ya ufisadi wa baadhi ya watendaji wa serikali.
Kulikuwa na maneno ya chini chini ya kuihusisha kampuni hiyo na aliyekuwa Waziri Mkuu wa wakati huo. Na maneno hayo yakapata nguvu mara tu baada ya mvua kunyesha na mabwawa yakajaa, akakimbilia kuwatangazia wananchi kwamba achaneni na Richmond maana hatuna shida tena na umeme wake huku akijua kabisa kwamba Richmond ilikuwa inakula pesa ya wavuja jasho wa nchi hii ipatayo milioni 152 kwa siku tena bila kuzalisha umeme.
Kukapigwa kelele kila kona ya nchi Watanzania tukidai mkataba wa kampuni hiyo ujadiliwe bungeni au sivyo, iundwe kamati teule ya bunge kuchunguza mkataba huo. Kila mkutano wa bunge ukifika ripoti ya Richmond ikawa hailetwi na badala yake Spika Sitta akawa wa kupiga tarehe ya kujadili Richmond bungeni kila kukicha na hatimaye ikatulia na ikawa imetoka!.
Ajabu kubwa ikaja kutokea mara baada ya sakata la Reginald Mengi na Malima ambalo baadaye liligeuka sura na kuwa la Sitta na Malima. Yakawepo maneno kwamba Malima hayuko peke yake katika kumvaa Sitta. Kukawa na maneno mengi tu kwamba nyuma ya Malima kuna mtu mkubwa anayetaka kumtumia Malima na mbunge fulani wa CCM aliyezoea kulipua mabomu ili kumngoa Sitta kwenye uspika.
Wenye akili kulingana na mazingira yaliyokuwepo, tayari waliweza kugundua kwamba mkubwa huyo ni nani. Ni baada tu ya Sitta kulimaliza sakata lake na Malima kwa staili ambayo haijawahi kutokea katika bunge la Tanzania, ndipo kwa mshangao kamati ya Shelukindo ikaibuka na taarifa kwamba Richmond imeliibia taifa na kudai bunge liunde kamati teule (miaka zaidi ya miwili baada ya Watanzania kuidai hiyo kamati teule).
Na kwa sababu spika anapewa mamlaka na kanuni za bunge akawateua wale wale (tunaweza kuwaita watu wake) kuunda kamati hiyo. Kwa baadhi yetu tulishajua matokeo ya kamati teule hata kabla ya ripoti yake kwamba itakwenda na kigogo. Na hata gazeti moja la kila wiki likaandika mapema kile kitakachotokea. Na ndicho kilichotokea.
Ni gazeti hilo hilo ambalo liliwahi kuandika makala ndefu iliyotokana na mahojiano yake na Zitto Kabwe, mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) ambapo ilielezwa kwamba kulikuwa na ugomvi wa chinichini lakini mkubwa kati ya Spika Sitta na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.
Na kikubwa ilikuwa ni kugombea kumrithi Kikwete mwaka 2015. Ni gazeti hilo hilo pia lililowahi kuandika makala nyingine ambayo haikuwahi kukanushwa na Sitta mwenyewe wala mtu mwingine (nakala zote hizo ninazo) ikidaiwa kwamba Sitta alikuwa ameahidiwa nafasi ya waziri mkuu wakati wa kampeni lakini baada tu ya ushindi wa mtandao wa kimbunga kama walivyopenda kuuita, Sitta aliitwa na kigogo mmoja na kutakiwa ajaze fomu ya kuomba uspika.
Ingawa walibishana kidogo na kigogo huyo, hatimaye alisalimu amri na kuchukua fomu ambapo alishinda. Ikiwa yote haya tuliyoelezwa ni ya kweli, basi tunaweza kufanya muhtasari wa ugomvi kati ya Sitta na Lowassa kama ifuatavyo:
Kwanza kugombea uwaziri mkuu wa awamu ya nne chini ya Kikwete, pili kitendo cha Sitta kuunda kamati ya kubadilisha kanuni za bunge ambazo zilikuwa zinambana zaidi waziri mkuu kwa kuwekewa kipindi cha kuhojiwa live na wabunge bila kujiandaa kwanza. Tatu, kitendo cha Malima kudaiwa kutaka kutumiwa kumngoa Sitta (nasisitiza kama ni kweli maana haikuwahi kuthibitishwa), Nne kitendo cha Sitta kuunda kamati teule ya wafuasi wake kummaliza Lowassa kupitia Richmond.
Ni baada ya ugomvi huu wa mwisho unaohusu Richmond ndipo sasa akina Sitta wakatangaza rasmi kuwa wapigana vita dhidi ya ufisadi na wakaamua kwa makusudi kuwanyanganya vita hiyo waanzilishi wake akina Dk. Slaa na kujifanya wao ndio wapiganaji dhidi ya ufisadi. Ni hicho ninachokipinga kwa nguvu zote.
Kwa kuainisha hivyo historia ya Spika wetu, napenda kusema kwa dhati kabisa ndani ya moyo wangu na nitakuwa tayari kabisa spika na watu wake wanipeleke mahakamani lakini kwa dhati nasema Sitta, Mwakyembe, Shelukindo, Kilango, Selelii, Sendeka, na wenzao wote, si wapiganaji wa vita dhidi ya ufisadi bali ni wapiganaji vita dhidi ya Lowassa na wenzake.
Hakuna vita dhidi ya ufisadi huku akiongoza wabunge kumzomea na kumbeza Dk. Slaa bungeni eti kwa sababu tu kasema ni vema posho zao za siku zipunguzwe ili wafanyakazi wanyonge kama polisi, waalimu, madaktari na waaguzi, na watumishi wengineo wa umma waongezewe mishahara. Haiwezekani akawa mpiganaji wa vita dhidi ya ufisadi huyo.
Na napenda niseme wazi kwamba, naamini kwa dhati wote tukiwachambua mmoja baada ya mwingine kuanzia kwa Mwakyembe, Kilango, Selelii, Sendeka, na wenzao wote wanaojidai kupigana vita dhidi ya mafisadi kila mmoja wao atakutwa tu na sababu binafsi ya kulichukia kundi la akina Lowassa.
Hakuna hata mmoja anayeweza kunidanganya eti kweli anaumwa na hali duni za wananchi. Walikuwa wapi siku zote. Na ukweli wa maneno yangu unaweza kuthibitishwa kama leo watu hawa hawa watapewa vyeo serikalini. Sitta awe waziri mkuu, Mwakyembe awe waziri wa Nishati na Madini, na wenzao wote hao wapewe uwaziri. Mtawasikia kama kweli watakumbuka vita dhidi ya ufisadi.
Nasema, ni vema Watanzania tukatambua ukweli. Ukweli kwamba hakuna hata mmoja anayewapigania wananchi ndani ya CCM. Nimemnukuu mbunge wa CCM katika makala yangu ya juma lililopita aliyesema kwamba ndani ya serikali ya CCM ni Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein peke yake ndiye mwadilifu. Wengine wote wameshaathiriwa na ufisadi.
Wanaojifanya kupiga vita ufisadi, wanasukumwa na sababu binafsi tena mara nyingi za ugomvi na wenzao. Sikutarajia Lazaro Nyarandu aliyekuwa akifoka bungeni juu ya ufisadi unaomaliza raslimali za taifa kwa sauti hiyo hiyo anamfokea Dk. Slaa kwenye kipindi cha moja ya kituo kimoja cha televisheni hapa nchini kisa kuomba mafao ya wakubwa yaangaliwe upya ili watu wa chini nao wafaidi.
Nasema sura halisi ya group hili la Sitta linalojifanya kupigana na ufisadi ndiyo hii. Hawana lolote isipokuwa maslahi binafsi. Suluhisho ni kuwangoa wote, mafisadi wa hadharani (wale tuliowabamba katika kashfa za EPA, Richmond, n.k) na hata wale mafisadi waliojificha (wanaojidai kupigana vita dhidi ya ufisadi kumbe wana ajenda yao binafsi).
Naamini mmenielewa!
NAAM! Nimetaja Spika Sitta Group kwa kuwa si peke yake. Kuna kundi la wanachama wa CCM wanaoishi ndani ya CCM lakini kwa mtazamo wa juu juu wakionekana kana kwamba hawatendi matendo ya CCM. Ni kama vile wanatimiza ile kauli ya Yesu, aliyowaasa wafuasi wake kwamba waishi ndani ya ulimwengu lakini wasitende ya walimwengu.
Ama wachangamane na watu wa mataifa lakini wasitende matendo ya mataifa. Ndivyo mtazamo wa juu juu unavyoweza kuwaonyesha hawa wana mtandao mpya ambao nimeupachika jina la Spika Sitta Group (SSG). Ndani wamo akina Harrison Mwakyembe, Anne Kilango Malecela, Lucas Selelii, Christopher Ole Sendeka, William Shelukindo, Said Nkumba, Lazaro Nyarandu, n.k, hawa ni wachache kwa idadi.
Mapema mwaka jana, Richmond ilitegeka. Ikaanzia kwenye Kamati ya Biashara iliyokuwa ikiongozwa na William Shelukindo na baadhi ya wajumbe wake akiwemo Dk. Mwakyembe, ikadaiwa baada ya miaka mingi kwamba ni muhimu sasa kuundwa kwa kamati teule ya bunge ya kuchunguza mkataba wa Richmond. Bunge lote likaridhia na hatimaye kamati ikateuliwa. Majina yakawa ni yale yale yaliyotarajiwa Kazi ikawa ni moja, kumtafuta mchawi wa Richmond.
Napenda nieleweke wazi mapema kabisa kwamba, katu katika makala hii silengi kuwatetea mafisadi wa aina yoyote ile. Wasomaji wanaonifuatilia sana ni mashahidi. Nimetumia nguvu nyingi mno kupiga vita ufisadi wa aina yoyote.
Kupitia kalamu hii nimetamka maneno mengi yenye kuhatarisha maisha yangu kiasi cha wasomaji wengi kunitumia ujumbe wa kuniuliza Hivi Mwigamba huogopi?. Na kwa kupigana vita dhidi ya mafisadi, mara kadhaa nimetishiwa kushtakiwa mahakamani, achilia mbali vitisho kutoka kule kwenye jumba jeupe. Nawakumbusha pia wasomaji kwamba nilishaapa kwamba hata kama kwa sababu yoyote ile nitaacha kuandika leo, bado nitaendelea kupigania haki ya mnyonge wa nchi hii.
Lakini wakati nikiwa na msimamo mkali kiasi hicho dhidi ya mafisadi, nawatangazia pia vita watu wa aina yoyote ambao hujifanya kupigana vita dhidi ya ufisadi wakati wakiwa na ajenda yao ya siri ya maslahi binafsi.
Hawa nao dhamiri ya moyo wangu inanituma kuwatangaza kwamba nao ni mafisadi. Yaani wanazo sababu binafsi za kuchukiana na fulani na kwa kweli wakipata fursa ya kum-fix wanamfix kweli kweli lakini huku wakitangaza kwamba ni kwa maslahi ya taifa.
Huu pia ni ufisadi na ni ufisadi mbaya kuliko. Bora ule ufisadi wa moja kwa moja maana ni rahisi kuugundua na kuushughulikia kuliko huu wa kuvaa ngozi ya kondoo kumbe ndani mbwa mwitu.
Baada ya dokezo hilo, naomba turejee kwenye mada yenyewe hasa. Kama wewe ni mtunza kumbukumbu mzuri, utakumbuka kwamba bunge jipya lilipoapishwa tu, Spika Sitta aliongoza jopo la wabunge wenzake kadhaa kudai nyongeza ya kile ambacho wao hukiita posho za wabunge na kuziepusha na kodi ya serikali wakati kimsingi ni kubwa mara elfu ya mishahara ya watumishi wengi wa serikali na sekta binafsi ambao hulipia kodi mishahara yao.
Hatimaye sakata hilo likaisha kwa Sitta kukosana na baadhi ya wanahabari kwa kurusha hewani pilikapilika zao za kudai nyongeza ya mafao hata kabla hawajaanza kazi. Hii ni sehemu ya sura halisi ya Sitta anayedai kupigana vita dhidi ya ufisadi.
Lakini pia wenye kumbukumbu watakumbua kwamba Richmond (ile kampuni feki ya kufua umeme wa dharura), iliingia mkataba na serikali mapema mwaka 2006. Na baadaye ikaonekana dhahiri kwamba ile kampuni ilikuwa imetuliza Watanzania kwa ajili ya ufisadi wa baadhi ya watendaji wa serikali.
Kulikuwa na maneno ya chini chini ya kuihusisha kampuni hiyo na aliyekuwa Waziri Mkuu wa wakati huo. Na maneno hayo yakapata nguvu mara tu baada ya mvua kunyesha na mabwawa yakajaa, akakimbilia kuwatangazia wananchi kwamba achaneni na Richmond maana hatuna shida tena na umeme wake huku akijua kabisa kwamba Richmond ilikuwa inakula pesa ya wavuja jasho wa nchi hii ipatayo milioni 152 kwa siku tena bila kuzalisha umeme.
Kukapigwa kelele kila kona ya nchi Watanzania tukidai mkataba wa kampuni hiyo ujadiliwe bungeni au sivyo, iundwe kamati teule ya bunge kuchunguza mkataba huo. Kila mkutano wa bunge ukifika ripoti ya Richmond ikawa hailetwi na badala yake Spika Sitta akawa wa kupiga tarehe ya kujadili Richmond bungeni kila kukicha na hatimaye ikatulia na ikawa imetoka!.
Ajabu kubwa ikaja kutokea mara baada ya sakata la Reginald Mengi na Malima ambalo baadaye liligeuka sura na kuwa la Sitta na Malima. Yakawepo maneno kwamba Malima hayuko peke yake katika kumvaa Sitta. Kukawa na maneno mengi tu kwamba nyuma ya Malima kuna mtu mkubwa anayetaka kumtumia Malima na mbunge fulani wa CCM aliyezoea kulipua mabomu ili kumngoa Sitta kwenye uspika.
Wenye akili kulingana na mazingira yaliyokuwepo, tayari waliweza kugundua kwamba mkubwa huyo ni nani. Ni baada tu ya Sitta kulimaliza sakata lake na Malima kwa staili ambayo haijawahi kutokea katika bunge la Tanzania, ndipo kwa mshangao kamati ya Shelukindo ikaibuka na taarifa kwamba Richmond imeliibia taifa na kudai bunge liunde kamati teule (miaka zaidi ya miwili baada ya Watanzania kuidai hiyo kamati teule).
Na kwa sababu spika anapewa mamlaka na kanuni za bunge akawateua wale wale (tunaweza kuwaita watu wake) kuunda kamati hiyo. Kwa baadhi yetu tulishajua matokeo ya kamati teule hata kabla ya ripoti yake kwamba itakwenda na kigogo. Na hata gazeti moja la kila wiki likaandika mapema kile kitakachotokea. Na ndicho kilichotokea.
Ni gazeti hilo hilo ambalo liliwahi kuandika makala ndefu iliyotokana na mahojiano yake na Zitto Kabwe, mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA) ambapo ilielezwa kwamba kulikuwa na ugomvi wa chinichini lakini mkubwa kati ya Spika Sitta na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.
Na kikubwa ilikuwa ni kugombea kumrithi Kikwete mwaka 2015. Ni gazeti hilo hilo pia lililowahi kuandika makala nyingine ambayo haikuwahi kukanushwa na Sitta mwenyewe wala mtu mwingine (nakala zote hizo ninazo) ikidaiwa kwamba Sitta alikuwa ameahidiwa nafasi ya waziri mkuu wakati wa kampeni lakini baada tu ya ushindi wa mtandao wa kimbunga kama walivyopenda kuuita, Sitta aliitwa na kigogo mmoja na kutakiwa ajaze fomu ya kuomba uspika.
Ingawa walibishana kidogo na kigogo huyo, hatimaye alisalimu amri na kuchukua fomu ambapo alishinda. Ikiwa yote haya tuliyoelezwa ni ya kweli, basi tunaweza kufanya muhtasari wa ugomvi kati ya Sitta na Lowassa kama ifuatavyo:
Kwanza kugombea uwaziri mkuu wa awamu ya nne chini ya Kikwete, pili kitendo cha Sitta kuunda kamati ya kubadilisha kanuni za bunge ambazo zilikuwa zinambana zaidi waziri mkuu kwa kuwekewa kipindi cha kuhojiwa live na wabunge bila kujiandaa kwanza. Tatu, kitendo cha Malima kudaiwa kutaka kutumiwa kumngoa Sitta (nasisitiza kama ni kweli maana haikuwahi kuthibitishwa), Nne kitendo cha Sitta kuunda kamati teule ya wafuasi wake kummaliza Lowassa kupitia Richmond.
Ni baada ya ugomvi huu wa mwisho unaohusu Richmond ndipo sasa akina Sitta wakatangaza rasmi kuwa wapigana vita dhidi ya ufisadi na wakaamua kwa makusudi kuwanyanganya vita hiyo waanzilishi wake akina Dk. Slaa na kujifanya wao ndio wapiganaji dhidi ya ufisadi. Ni hicho ninachokipinga kwa nguvu zote.
Kwa kuainisha hivyo historia ya Spika wetu, napenda kusema kwa dhati kabisa ndani ya moyo wangu na nitakuwa tayari kabisa spika na watu wake wanipeleke mahakamani lakini kwa dhati nasema Sitta, Mwakyembe, Shelukindo, Kilango, Selelii, Sendeka, na wenzao wote, si wapiganaji wa vita dhidi ya ufisadi bali ni wapiganaji vita dhidi ya Lowassa na wenzake.
Hakuna vita dhidi ya ufisadi huku akiongoza wabunge kumzomea na kumbeza Dk. Slaa bungeni eti kwa sababu tu kasema ni vema posho zao za siku zipunguzwe ili wafanyakazi wanyonge kama polisi, waalimu, madaktari na waaguzi, na watumishi wengineo wa umma waongezewe mishahara. Haiwezekani akawa mpiganaji wa vita dhidi ya ufisadi huyo.
Na napenda niseme wazi kwamba, naamini kwa dhati wote tukiwachambua mmoja baada ya mwingine kuanzia kwa Mwakyembe, Kilango, Selelii, Sendeka, na wenzao wote wanaojidai kupigana vita dhidi ya mafisadi kila mmoja wao atakutwa tu na sababu binafsi ya kulichukia kundi la akina Lowassa.
Hakuna hata mmoja anayeweza kunidanganya eti kweli anaumwa na hali duni za wananchi. Walikuwa wapi siku zote. Na ukweli wa maneno yangu unaweza kuthibitishwa kama leo watu hawa hawa watapewa vyeo serikalini. Sitta awe waziri mkuu, Mwakyembe awe waziri wa Nishati na Madini, na wenzao wote hao wapewe uwaziri. Mtawasikia kama kweli watakumbuka vita dhidi ya ufisadi.
Nasema, ni vema Watanzania tukatambua ukweli. Ukweli kwamba hakuna hata mmoja anayewapigania wananchi ndani ya CCM. Nimemnukuu mbunge wa CCM katika makala yangu ya juma lililopita aliyesema kwamba ndani ya serikali ya CCM ni Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein peke yake ndiye mwadilifu. Wengine wote wameshaathiriwa na ufisadi.
Wanaojifanya kupiga vita ufisadi, wanasukumwa na sababu binafsi tena mara nyingi za ugomvi na wenzao. Sikutarajia Lazaro Nyarandu aliyekuwa akifoka bungeni juu ya ufisadi unaomaliza raslimali za taifa kwa sauti hiyo hiyo anamfokea Dk. Slaa kwenye kipindi cha moja ya kituo kimoja cha televisheni hapa nchini kisa kuomba mafao ya wakubwa yaangaliwe upya ili watu wa chini nao wafaidi.
Nasema sura halisi ya group hili la Sitta linalojifanya kupigana na ufisadi ndiyo hii. Hawana lolote isipokuwa maslahi binafsi. Suluhisho ni kuwangoa wote, mafisadi wa hadharani (wale tuliowabamba katika kashfa za EPA, Richmond, n.k) na hata wale mafisadi waliojificha (wanaojidai kupigana vita dhidi ya ufisadi kumbe wana ajenda yao binafsi).
Naamini mmenielewa!