Jakaya Mrisho Kikwete ni nani?

Jakaya Mrisho Kikwete ni nani?

Paul Alex

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2012
Posts
4,346
Reaction score
9,846
Rais wetu aliwahi kutoa onyo kuwa watu wasidanganyike na sura yake, wasidanganyike na tabasamu lake.

Nimekuwa nikimfuatilia kwa karibu sana toka alipotoa maneno hayo ili nifahamu sura yake kamili na maana ya tabasamu lake ila nimefeli, sijaambulia kitu.

Ndio maana leo naomba msaada kwa waliomfahamu vizuri, wapendwa; Jakaya Mrisho Kikwete ni nani?

1. Je, ni mwanamapinduzi au labda ni mwanamageuzi?

2. Je,ni mtu asieogopa kujaribu au ni mtu asiyejua anachojaribu?

3. Je,ni dicteta aliyejificha kwenye ngozi ya democrasia au ni mtu mwenye misimamo isioyumba?

4. Je, ni mtu msafi aliyezungukwa na wezi au ni mafia anayetumia mkono wa giza kufanya mambo yake?

5. Je, Magufuli ni zawadi ya Kikwete kwa Tanzania au ni toleo la pili la Kikwete?

Au ni mchawi anayetaka kuizamisha Tanzania?

6.Uzuri wake mkubwa ni nini na kosa lake kubwa ni nini?

7.Je, ni rais aliyehujumiwa na watendaji wake au anatumia kisingizio cha kuhujumiwa kuficha udhaifu wake?

8.Je, anajua alipo Mwamunyange? na kama anajua mbona hatuambii?

9.Je, CCM ikishindwa uchaguzi atarudi Msoga kulima kweli?

Wadau nisaidieni kujua, Jakaya Mrisho Kikwete ni nani?
 
Ni tolea la pili, Kwan Kwa hali iliyopo ni vigumu ccm kutuletea maendeleo tunayoyahitaji. Ikiwa pindi ipo madarakani ilikuwa hawez kufanya maamuz magumu zidi ya miss use of public funds
 
Ni m-badhilifu wa mali za umma, anaogopa kuamua jambo wakati yeye ndiye mwenye mamlaka. Ni mtu muoga sana, alianza vizuri anamaliza vibaya
 
Ni tolea la pili, Kwan Kwa hali iliyopo ni vigumu ccm kutuletea maendeleo tunayoyahitaji. Ikiwa pindi ipo madarakani ilikuwa hawez kufanya maamuz magumu zidi ya miss use of public funds

Kingunge anasema wameishiwa pumzi!
 
ni muhusika mkuu wa richmond-Lissu
 
Maamuzi yake yananifanyaga niote vipele vya baridi. Mfano: unapobadilisha wakuu wa wilaya na kuweka wapya mwezi mmoja kabla ya kuachia madaraka ni kama unatuma ujumbe gani.Maana kwa miaka kumi sasa uongozi wote ni sura na mfano wake, kuna nini labda alisahau anataka kifanyike sasa.
Watu wanabadilishwa kwenye tume ya uchaguzi na maelezo ni kuwa ni utaratibu tu wa serekali.

Hivi haya ni mambo ya kawaida duniani?
Nisaidieni jamani maana nahisi uongozi wa CCM unatudhalilisha watanzania.
 
anajifanya aogopi lakn ni mtu mwoga sana aliyepata kutokea anajua kitu hataji anawaambia wengine wataje
 
Ni RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awali ya Nne anayetarajiwa kumaliza muda wake mwanzo wa November 2015 Mara baada ya Magufuli kuapishwa Kuchukua nafasi yake
 
Ni Mume wa Salma
Ni baba yake Ridhiwani
NI mkazi wa Bagamoyo mkoani Pwani
Ni Mtanzania
Ni mwanamume
 
Ndio maana leo naomba msaada kwa waliomfahamu vizuri, wapendwa; Jakaya Mrisho Kikwete ni nani?

1. Je, ni mwanamapinduzi au labda ni mwanamageuzi?

2. Je,ni mtu asieogopa kujaribu au ni mtu asiyejua anachojaribu?

3. Je,ni dicteta aliyejificha kwenye ngozi ya democrasia au ni mtu mwenye misimamo isioyumba?

4. Je, ni mtu msafi aliyezungukwa na waizi au ni mafia anayetumia mkono wa giza kufanya mambo yake?

5. Je, Magufuli ni zawadi ya Kikwete kwa Tanzania au ni toleo la pili la Kikwete?

Wadau nisaidieni kujua, Jakaya Mrisho Kikwete ni nani?
mkuu Paul Alex, hoja yako imesimama vizuri. Nakushauri hizo contents zako uziwekee namba kama hivi ili kurahisisha watoa mawazo.

Hiyo namba nne naiona kama imesimama.
 
Back
Top Bottom