Jakaya Mrisho Kikwete, Mungu atakulipa!

Jakaya Mrisho Kikwete, Mungu atakulipa!

Ndugu zangu watanzania wenzangu, kupitia jamvi hili, kwa heshima na taadhima nichukue fursa hii kumwandikia Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, kwanza kumpa pole kwa majukumu mazito aliyonayo katika kulitumikia taifa lake. Ninampa pole kutokana na kutambua ugumu wa majukumu aliyonayo.

Kwa nafasi yake, yeye ndiye wa kutupiwa lawama zote pale mambo yanapokwenda si sawa. Pia ni mtu wa kupongezwa pale mambo yanaponyooka. Hii ni kawaida kwani wahenga walikwushasema kuwa mkubwa ni jalala.

Ndugu zangu watanzania wenzangu, mimi leo ningependa kuzungumzia kazi nzuri ambayo Rais Kukwete ameifanya ambapo hata kama baadhi yetu tutaibeza, ukweli utajidhihirisha.

Kikwete, katika kipindi cha miaka 9 amefanya yafuatayo mazuri;
1. Uchumi; amefanya mabadiliko kwenye kilimo ambapo wakulima wengi kwasasa wanalima kisasa na kwa msaada wa pembejeo za ruzuku.

Walau imesaidia taifa kuwa na akiba ya chakula cha kutosha hivyo kutokuwa na hofu ya wananchi kufa njaa. Kilimo cha umwagiliaji kimeongezeka, kilimo cha biashara kimekua. Mabadiliko ya sheria ya uwekezaji angalau yamewezesha nchi kuanza kunufaika na kodi ya uzalishaji ingawa bado si kwa kiasi kikubwa. Uboreshaji wa huduma za kibenki, mikopo ya saccos, uboreshaji wa njia za uchukuzi kama barabara, vivuko, reli kwa kununua vichwa na mabehewa, ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege e.g. Rungwe, Katavi, Gombe, DSM. n.k.

2. Kisiasa; Ni katika kipindi cha Kikwete ambapo uhuru wa shughuli za kisiasa umetolewa. Watanzania sote ni mashahidi kwamba vyama vya siasa vimekuwa huru kiasi kwamba baadhi vimeshindwa kuutumia uhuru huo ambapo baadhi vimeishia kuitisha maandamano, kukitisha chama cha mapinduzi na kutishia uvunjifu wa amani kama mbinu ya kutaka kutimiza adhma zao za kisiasa.

Ni wakati huu ambapo majukwaa ya siasa yametumika kuvitukana na kuvidhalilisha vyombo vya dola kwamba havina lolote. Ni wakati huu ambapo wanasiasa wa vyama pinzani wameachwa kuichambua serikali kwa kadiri ya hazina ya maneno iliyoko vinywani mwao.

Ni wakati huu ambao hakuna mwanasiasa aliwekwa kizuizini kwa kutoa kauli zenye kuhatarisha usalama wa nchi. Wanasiasa baadhi yao walifikia hatua ya kutisha kuwa wanao uwezo wa kuifanya nchi isitaealike, hakuna aliyeshughulika nao.

Aidha ni wakati huu ambao siku moja watu walikuwa wakishuhudia chama fulani kimeitisha maandamano nchi nzima kisha muitisha maandamano akakimbilia South Africa! Kiukweli ni wakati unaelekea mwishonu lkn kwa wanasiasa hasa wa upinzani mtaukumbuka!!!

3. Kijamii; Rais Kikwete amejitahidu kuimarisha huduma za kijamii kama usambazaji wa umeme vijijini kupitia REA, Ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme wa gesi asilia huko Mtwara ambapo sote tunajua jinsi wanasiasa walivyoupinga na kufanya kila aina ya uchochezi ili usifanikiwe, leo tunashuhudia mradi unelekea kujamilika.

Miradi ya maji vijijini imetekelezwa kwa kasi awamu hii. Upande wa elimu mafanikio yako wazi ambapo ongezeko la ajira za walimu, ongezeko la shule za msingi na sekondari na pia ujenzi wa vyuo vikuu kwa ujumla vimetokea wakati wako.

Maboresho ya mishahara kwa wafanyakazi yamefanyika wakati wako. Kwa upande wa afya, siyo siri ununuzi wa vifaa vya kisasa mahospitalini walau umefanyika wakati huu kwa kiwango cha kuridhisha, ujenzi wa zahanati na vituo vya afya kupitia TASSAF, hospitali za mikoa kuwa za rufaa, mapambano dhidi ya malaria na UKIMWI, uzuiaji wa vifo vya mama wajawazito, juduma bure za matibabu kwa wazee (bado changomoto katika utekelezaji), maboresho ya Hospitali ya taifa ya Muhimbili ambapo sasa ina uwezo wa kutibu magonjwa ambayo awali matibabu yake yalipatikana nje yanchi n.k.

4. Kimataifa; Kwanza amejitahidi kukwepa mitego ya maadui zetu waliotaka kuliingiza taifa vitani kwasababu za chuki binafsi na wivu kutokana na nchi yetu kuanza kukua kiuchumi kwa kasi. Mfano wa nchi hizo sote tunao. Kikwete alijua kwamba vita kwasasa siyo kipaumbele cha nchi ingawa uwezo wa kuwachapa hao maadui zetu tunao.

Alifanya uamuzi mzuri na wa kizalendo. Isingekuwa rahisi kwa Rais asiye busara kuacha kuiingiza nchi vitani dhidi ya Rwanda, Malawi na Kenya wakati ambao nchi hizo zilionesha wazi kuichokoza Tanzania. Ni busara ya kiwango cha juu aliyonayo Kikwete hata kufanikiwa kuukwepa mtego huo.

Pia amejitahidi kusuluhisha migogoro katika nchi mbalimbali kama vile ule wa Kenya mwaka 2008, wa Sudan ya Kusini, Congo DR, Comoro, Afrika ya kusini (wa ndani ya ANC). Amekuwa na ushawishi mkubwa kwa mataifa makubwa kwa kuifuata sawasawa sera mama ya taifa ya kutofungamana na upande wowote kwa lengo la kuiepusha nchi kuwa na uadui unaotokana na mivutano baina ya mataifa makubwa.

Katiba mpya; Jambo hili halijaisha, tumwombe Mungu liishe salama!. Sote ni mashahidi juu ya umahiri alionao Kikwete katika namna anavyolihandle swala hili muhomu kwa mstakabali mwema wa taifa letu. Siyo siri swala hili limegubikwa na mambo mengi lkn mbaya na hatari inayoonekana ni kuibuka kwa kundi la watu linaloipinga katiba iliyopendekezwa.

Sina tatizo na kupingwa huko ola nina tatizo na sababu za kuipinga. Mfano wengi wanadai kuwa katiba pendekezwa imekiondoa kipengele cha uadilifu, si kweli kwani kipengele hicho kipo isipokuwa kiliondolewa kwenye Ibara inayohusu tunu za taifa na kuwekwa kwenye ibara ya maadili ya mtumishi wa umma. Kiukweli uadilifu siyo tunu kwa tafsiri yake bali ni swala la uadilifu.

Tunu ni kama vile Lugha ya kiswahili,amani, muungano n.k. Swala la katiba limeingiliwa na siasa kiasi kwamba watu hawajadili tena kwa uchungu wa kulinda misingi ya utaifa wetu bali kwa maslahi na kupata upenyo wa kisiasa.

Ninaamini kwa umakini wa Rais wetu atasimamia na hatimaye tutapata katiba yenye maslahi mapana ya historia ya taifa letu hasa Muungano, udugu na amani.

My take; Pamoja na mafanikio hayo wapo baadhi ya watanzania ambao wameendelea kubeza kwa namna yoyote ile. Baadhi yao wamediriki kukashifu kwa matusi na kumdhihaki Kikwete kwa lugha mbaya kabisa. Ni kweli hakuna binadamu aliyetimilika kwa kufanya bila kukosea.

Inawezekana katika utendaji wake kuna mahali amekosea hata hivyo sidhani kama anastahili kulaumiwa kiasi hicho. Ninawaambia ndugu zangu watanzania wenzangu, tutamkumbuka Kikwete siku moja!. Wanasiasa hasa wa vyama pinzani iko siku mtamkumbuka Kikwete!.

Waropokaji msio na staha katika kauli zenu mtamkumbuka Kikwete!. Na kwako Mheshimiwa Rais, nikusihi usokate tamaa, endelea kuchapa kazi kwani kama ni ng'ombe umebakiza kipande cha mkia tu!. Ulishawashinda tayari mbona!. Up to this moment, you are the winner Sir!.

Cha muhimu malizia kazi zako na Mungu Baba Mwenyezi atakulipa kwa kazi nzuri uliyowafanyia watanzania. Jifunze kwa Prof. Muhongo, aliyekuwa waziri wako ambaye pamoja na mazuri yote aliyoyafanya mwisho wa siku watanzania wasio shukurani walimwandalia manila na kumnyonga kisiasa hadharani!.

As you signing off Sir keepon praying for your nation ili kikombe cha siasa chafu ya wasaka madaraka hali mikono yao ikinuka rushwa, kiliepushe taifa kuingia kwenye machafuko.

Usifanye mchezo na hiyo malaria!! Itakuua muda si mrefu! Sifa zote za nini? Kwa akili yako unawezalinganisha alofanya Mkapa na Kikwete?!

Usiwe mpuuzi kisa upo karibu na raisi, mengine mweleze mkeo/mumeo, sio sisi watanzania wa leo!!
 
-ni kipindi cha kikwete ambapo ajira imekuwa ngumu kuliko awamu zote
-Ufisadi umekuwa up to the maximum kuliko kuwahi kutokea
-ni kipindi chake JK AMBACHO FISADI NA WEZI wanatambaa mtaani na wanasema hawawezi kufungwa
-Ni kipindi cha Jk Ambacho inflation rate iko juu sana kuwahi tokea na mwenye jukumu la kuhakikisha anasema hela zenu za madafu,
-ni kipindi cha JK ambacho wanaharakati wanatekwa hadharani,wauwaji wanapandishwa vyeo
-Ni kipind hiki cha JK ambacho ikulu inaendeshwa toka makongo juu,yaani fisadi anamuandikia barua rais ikulu kuwa usiwasikilize Watanzania
-Ni kipindi hiki cha JK ambacho kila rafiki wa mwana mfalme ni mkuu wa WILAYA
-Ni kipindi hiki ambacho baba,mama na mtoto wote viongozi wa chama
TUSIPENDE KUSIFIA UJINGA,KUMLINGANISHA BEN NA HUYU NI KUTOITENDEA HAKI TANZANIA

Mleta mada ni mpuuzi sana na hata hajielewi kabisa!
 
"Mzawa JF"huwezi kuwa mzalendo wewe!. Uzalendo tuachie sisi "wazawa wa Tanzania". Wewe baki na kazi yako ya kuitumikia JF!

MJENGA# jibu maswali ya watu waliouliza ! acha ujinga" ww ndio mzalendo ktk nchi gani?
 
Ndugu zangu watanzania wenzangu, kupitia jamvi hili, kwa heshima na taadhima nichukue fursa hii kumwandikia Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, kwanza kumpa pole kwa majukumu mazito aliyonayo katika kulitumikia taifa lake. Ninampa pole kutokana na kutambua ugumu wa majukumu aliyonayo.

Kwa nafasi yake, yeye ndiye wa kutupiwa lawama zote pale mambo yanapokwenda si sawa. Pia ni mtu wa kupongezwa pale mambo yanaponyooka. Hii ni kawaida kwani wahenga walikwushasema kuwa mkubwa ni jalala.

Ndugu zangu watanzania wenzangu, mimi leo ningependa kuzungumzia kazi nzuri ambayo Rais Kukwete ameifanya ambapo hata kama baadhi yetu tutaibeza, ukweli utajidhihirisha.

Kikwete, katika kipindi cha miaka 9 amefanya yafuatayo mazuri;
1. Uchumi; amefanya mabadiliko kwenye kilimo ambapo wakulima wengi kwasasa wanalima kisasa na kwa msaada wa pembejeo za ruzuku.

Walau imesaidia taifa kuwa na akiba ya chakula cha kutosha hivyo kutokuwa na hofu ya wananchi kufa njaa. Kilimo cha umwagiliaji kimeongezeka, kilimo cha biashara kimekua. Mabadiliko ya sheria ya uwekezaji angalau yamewezesha nchi kuanza kunufaika na kodi ya uzalishaji ingawa bado si kwa kiasi kikubwa. Uboreshaji wa huduma za kibenki, mikopo ya saccos, uboreshaji wa njia za uchukuzi kama barabara, vivuko, reli kwa kununua vichwa na mabehewa, ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege e.g. Rungwe, Katavi, Gombe, DSM. n.k.

2. Kisiasa; Ni katika kipindi cha Kikwete ambapo uhuru wa shughuli za kisiasa umetolewa. Watanzania sote ni mashahidi kwamba vyama vya siasa vimekuwa huru kiasi kwamba baadhi vimeshindwa kuutumia uhuru huo ambapo baadhi vimeishia kuitisha maandamano, kukitisha chama cha mapinduzi na kutishia uvunjifu wa amani kama mbinu ya kutaka kutimiza adhma zao za kisiasa.

Ni wakati huu ambapo majukwaa ya siasa yametumika kuvitukana na kuvidhalilisha vyombo vya dola kwamba havina lolote. Ni wakati huu ambapo wanasiasa wa vyama pinzani wameachwa kuichambua serikali kwa kadiri ya hazina ya maneno iliyoko vinywani mwao.

Ni wakati huu ambao hakuna mwanasiasa aliwekwa kizuizini kwa kutoa kauli zenye kuhatarisha usalama wa nchi. Wanasiasa baadhi yao walifikia hatua ya kutisha kuwa wanao uwezo wa kuifanya nchi isitaealike, hakuna aliyeshughulika nao.

Aidha ni wakati huu ambao siku moja watu walikuwa wakishuhudia chama fulani kimeitisha maandamano nchi nzima kisha muitisha maandamano akakimbilia South Africa! Kiukweli ni wakati unaelekea mwishonu lkn kwa wanasiasa hasa wa upinzani mtaukumbuka!!!

3. Kijamii; Rais Kikwete amejitahidu kuimarisha huduma za kijamii kama usambazaji wa umeme vijijini kupitia REA, Ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme wa gesi asilia huko Mtwara ambapo sote tunajua jinsi wanasiasa walivyoupinga na kufanya kila aina ya uchochezi ili usifanikiwe, leo tunashuhudia mradi unelekea kujamilika.

Miradi ya maji vijijini imetekelezwa kwa kasi awamu hii. Upande wa elimu mafanikio yako wazi ambapo ongezeko la ajira za walimu, ongezeko la shule za msingi na sekondari na pia ujenzi wa vyuo vikuu kwa ujumla vimetokea wakati wako.

Maboresho ya mishahara kwa wafanyakazi yamefanyika wakati wako. Kwa upande wa afya, siyo siri ununuzi wa vifaa vya kisasa mahospitalini walau umefanyika wakati huu kwa kiwango cha kuridhisha, ujenzi wa zahanati na vituo vya afya kupitia TASSAF, hospitali za mikoa kuwa za rufaa, mapambano dhidi ya malaria na UKIMWI, uzuiaji wa vifo vya mama wajawazito, juduma bure za matibabu kwa wazee (bado changomoto katika utekelezaji), maboresho ya Hospitali ya taifa ya Muhimbili ambapo sasa ina uwezo wa kutibu magonjwa ambayo awali matibabu yake yalipatikana nje yanchi n.k.

4. Kimataifa; Kwanza amejitahidi kukwepa mitego ya maadui zetu waliotaka kuliingiza taifa vitani kwasababu za chuki binafsi na wivu kutokana na nchi yetu kuanza kukua kiuchumi kwa kasi. Mfano wa nchi hizo sote tunao. Kikwete alijua kwamba vita kwasasa siyo kipaumbele cha nchi ingawa uwezo wa kuwachapa hao maadui zetu tunao.

Alifanya uamuzi mzuri na wa kizalendo. Isingekuwa rahisi kwa Rais asiye busara kuacha kuiingiza nchi vitani dhidi ya Rwanda, Malawi na Kenya wakati ambao nchi hizo zilionesha wazi kuichokoza Tanzania. Ni busara ya kiwango cha juu aliyonayo Kikwete hata kufanikiwa kuukwepa mtego huo.

Pia amejitahidi kusuluhisha migogoro katika nchi mbalimbali kama vile ule wa Kenya mwaka 2008, wa Sudan ya Kusini, Congo DR, Comoro, Afrika ya kusini (wa ndani ya ANC). Amekuwa na ushawishi mkubwa kwa mataifa makubwa kwa kuifuata sawasawa sera mama ya taifa ya kutofungamana na upande wowote kwa lengo la kuiepusha nchi kuwa na uadui unaotokana na mivutano baina ya mataifa makubwa.

Katiba mpya; Jambo hili halijaisha, tumwombe Mungu liishe salama!. Sote ni mashahidi juu ya umahiri alionao Kikwete katika namna anavyolihandle swala hili muhomu kwa mstakabali mwema wa taifa letu. Siyo siri swala hili limegubikwa na mambo mengi lkn mbaya na hatari inayoonekana ni kuibuka kwa kundi la watu linaloipinga katiba iliyopendekezwa.

Sina tatizo na kupingwa huko ola nina tatizo na sababu za kuipinga. Mfano wengi wanadai kuwa katiba pendekezwa imekiondoa kipengele cha uadilifu, si kweli kwani kipengele hicho kipo isipokuwa kiliondolewa kwenye Ibara inayohusu tunu za taifa na kuwekwa kwenye ibara ya maadili ya mtumishi wa umma. Kiukweli uadilifu siyo tunu kwa tafsiri yake bali ni swala la uadilifu.

Tunu ni kama vile Lugha ya kiswahili,amani, muungano n.k. Swala la katiba limeingiliwa na siasa kiasi kwamba watu hawajadili tena kwa uchungu wa kulinda misingi ya utaifa wetu bali kwa maslahi na kupata upenyo wa kisiasa.

Ninaamini kwa umakini wa Rais wetu atasimamia na hatimaye tutapata katiba yenye maslahi mapana ya historia ya taifa letu hasa Muungano, udugu na amani.

My take; Pamoja na mafanikio hayo wapo baadhi ya watanzania ambao wameendelea kubeza kwa namna yoyote ile. Baadhi yao wamediriki kukashifu kwa matusi na kumdhihaki Kikwete kwa lugha mbaya kabisa. Ni kweli hakuna binadamu aliyetimilika kwa kufanya bila kukosea.

Inawezekana katika utendaji wake kuna mahali amekosea hata hivyo sidhani kama anastahili kulaumiwa kiasi hicho. Ninawaambia ndugu zangu watanzania wenzangu, tutamkumbuka Kikwete siku moja!. Wanasiasa hasa wa vyama pinzani iko siku mtamkumbuka Kikwete!.

Waropokaji msio na staha katika kauli zenu mtamkumbuka Kikwete!. Na kwako Mheshimiwa Rais, nikusihi usokate tamaa, endelea kuchapa kazi kwani kama ni ng'ombe umebakiza kipande cha mkia tu!. Ulishawashinda tayari mbona!. Up to this moment, you are the winner Sir!.

Cha muhimu malizia kazi zako na Mungu Baba Mwenyezi atakulipa kwa kazi nzuri uliyowafanyia watanzania. Jifunze kwa Prof. Muhongo, aliyekuwa waziri wako ambaye pamoja na mazuri yote aliyoyafanya mwisho wa siku watanzania wasio shukurani walimwandalia manila na kumnyonga kisiasa hadharani!.

As you signing off Sir keepon praying for your nation ili kikombe cha siasa chafu ya wasaka madaraka hali mikono yao ikinuka rushwa, kiliepushe taifa kuingia kwenye machafuko.

Asante sana mkuu, kuna watanzania hawajaona haya yote!! Kikwete atabarikiwa sana, ila Shetan ndo atakaembariki sio Mungu!

Swala la madawa ya kulevya kalisimamia barabara na amehakikisha majina ya wauza madawa anayalinda. Hili nalo anastahili pongezi. Vijana wanavoteketea kwa kutumia madawa na wengine wapo jela kwa kusafirisha.

JK ashukuriwe kwa hili, ni nani raisi pekee alieweza kuwalinda Tembo wetu na twiga wetu. Sote tumeshuhudia hili!

Maalbino wanateketea kwa uzembe wa serikali, JK apewe sifa kwa hili. Maana albino sio watu na ameweza kuwafanya kafara. Jumuia za kuimataifa zinalaani hiki kitendo, yeye ameweka pamba masikion, apewe sifa JK kwa hili!!

Mkuu umejitahidi, hayo ni baadhi ya mambo ambayo watanzania hawatokaa wamsahau JK kwa kutufanyia! Usisahau babu Seya yupo gerezani kwa amri ya JK!
 
Hizo zoooote porojo.

Ukweli ni kwamba walikuwepo wote wanne kwa wakati mmoja Tanzania hii, mwenyeji wao akiwa Kikwete. Obama, Bush, Clinton na Jimmy Carter. Hata kwenye maziko ya Mandela haijatokea hiyo Huyo ndiyo Kikwete. Kumbuka hilo.

Record.
. Faiza hao wote mbona ni makafiri?
 
Watakuja watu kubeza hayo mafanikio. Mimi huwa nnawaambia wachanganye awamu zote waone kama Kikwete hajafanya zaidi ya wote.

Ni kweli kabisa; awamu ya nne chini ya uongozi wa Prof. Dr. Kikwete tumeshuhudia mengi ikiwamo;
; Kushamiri kwa biashara ya madawa ya kulevya, mauaji ya tembo na kuendelea kuangamizwa kwa kizazi cha albino
; Chini ya uongozi wa Kikwete tumeshuhudia Serikali ikikiri wazi kushindwa kuwakamata wahalifu na mafisadi kwa kigezo kuwa kwa kufanya hivyo nchi itatikisika
; Kikwete kama rais wa nchi alikiri wazi kuwa hajui sababu ya umaskini wa Watanzania
; Chini ya utawala wa Kikwete tumeshuhudia familia za watawala zikipora kwa kasi ya ajabu rasilimali za taifa na mashirika ya umma kama vile UDA, eneo la iliyokuwa TANGANYIKA PACKERS, kushamiri kwa migogoro ya ardhi na kuendelea kushuka kwa huduma muhimu kama vile maji, afya na elimu.

KWA UJUMLA KAMA NI BARAKA ATAZIPATA KUTOKA KWA SHETANI NA SIO MUNGU TUNAYEMUOMBA KILA UCHAO.
 
Sasa ulitaka mimi nifanye nini ikiwa wewe ndiye unasema hao ni makafiri?

Vipi wewe? si kafiri?

FaizaFoxy naona unatoa majibu mepesi kwa maswali nondo.....siamini kama umeishiwa namna hiyo
 
Ni kweli kabisa; awamu ya nne chini ya uongozi wa Prof. Dr. Kikwete tumeshuhudia mengi ikiwamo;
; Kushamiri kwa biashara ya madawa ya kulevya, mauaji ya tembo na kuendelea kuangamizwa kwa kizazi cha albino
; Chini ya uongozi wa Kikwete tumeshuhudia Serikali ikikiri wazi kushindwa kuwakamata wahalifu na mafisadi kwa kigezo kuwa kwa kufanya hivyo nchi itatikisika
; Kikwete kama rais wa nchi alikiri wazi kuwa hajui sababu ya umaskini wa Watanzania
; Chini ya utawala wa Kikwete tumeshuhudia familia za watawala zikipora kwa kasi ya ajabu rasilimali za taifa na mashirika ya umma kama vile UDA, eneo la iliyokuwa TANGANYIKA PACKERS, kushamiri kwa migogoro ya ardhi na kuendelea kushuka kwa huduma muhimu kama vile maji, afya na elimu.

KWA UJUMLA KAMA NI BARAKA ATAZIPATA KUTOKA KWA SHETANI NA SIO MUNGU TUNAYEMUOMBA KILA UCHAO.

- Nioneshe wakai adawa ya kulevya yameshikwa kwa wingi na wauza madawa kushikwa kwa wingi kabla ya awamu ya Kikwete.

- Nioneshe awamu ambayo hata mawaziriwameionja keko kwa ufisadi ka si hii ya Kikwete.

- Naam, alisema hilo, ulitaka aseme kuwa Watanzania umasikini wao ni ujinga walio nao? ungemuelewa? amekuwa diplomat sana kujibu hilo. Mimi nakuuliza wewe, kwani wewe ni masikini?

- UDA limekufa zamani sana na limewekwa katika kumilikishwa kwa watuu binafsi, hebu nioneshe wamiliki wa UDA niwajuwe ni akina nani, mimi siwajui. usije na porojo, njoo na ushahidi. Maana ulimi hauna mfupa.

-Tanganyika Packers ni lini ilikuwa ya Serikali na sasa ni ya nani?

- Maji, afya na elimu, hakuna wakati wowote viko juu zaidi ya huu wa Kikwete.

Juu huko nimeshaweka kwa uchache kuhusu Afya, ngoja nirudie darsa tena labda lilikupita; Kabla ya Kikwete uwiano wa matarajio ya Mtanzzania kuishi ulikuwa chini ya miaka 50, Nyerere miaka 43, Mwinyi 45, Mkapa 48, wakati wa Kiwete ni miaka isiyopinguwa 62 (2012). Jee ni nani kawapa Watanzania Afya bora?

Jibu hilo kwanza kabla sijaja na a maji na elimu. Usikimbie tafadhali.
 
FaizaFoxy naona unatoa majibu mepesi kwa maswali nondo.....siamini kama umeishiwa namna hiyo

Swali "nondo" liko wapi?

Mtu kishasema yeye kuwa wale ni makafiri, unataka nimbishie? Unanchekesha!
 
Hizo zoooote porojo.

Ukweli ni kwamba walikuwepo wote wanne kwa wakati mmoja Tanzania hii, mwenyeji wao akiwa Kikwete. Obama, Bush, Clinton na Jimmy Carter. Hata kwenye maziko ya Mandela haijatokea hiyo Huyo ndiyo Kikwete. Kumbuka hilo.

Record.

Hili nalo ni lakujivunia jamani!? Unajivunia nini hapo sasa? Walipokuja mimi kama mtanzania wa kawaida nimefaidika nini!? Hivi FF, ni akili yako au umelewa madaraka?
 
Swali "nondo" liko wapi?

Mtu kishasema yeye kuwa wale ni makafiri, unataka nimbishie? Unanchekesha!

Apo niliku quote tuu ila nazungumzia comments zako zilizopita yani nimekudharau kweli.
 
Hili nalo ni lakujivunia jamani!? Unajivunia nini hapo sasa? Walipokuja mimi kama mtanzania wa kawaida nimefaidika nini!? Hivi FF, ni akili yako au umelewa madaraka?

Dah! ikiwa hujuwi ulichofaidika, ni vigumu sana kukuelewesha, lakini ntakupa darsa dogo la halafu wewe fatilia zaidi kama kweli unataka kuelewa:

Ubungo Plaza, Symbion Power Plant
Dar es Salaam, Tanzania
10:58 A.M. EAT

PRESIDENT OBAMA: Good morning, everybody. Please have a seat. It is wonderful to be here with President Kikwete. I want to thank everybody from Ubungo Power Plant for this visit. We are here today to focus on one of the biggest hurdles to Africa's economic development -- the fact that nearly 70 percent of Africans lack access to electricity.
And that's why in my speech in Cape Town I announced a major new initiative -- Power Africa -- to double access to electricity here in Africa. Now, the first step that we're going to take is to try to bring electricity to 20 million homes and businesses.

And this plant represents the kind of public-private partnership that we want to replicate all across the continent. This facility was idle. But the Tanzanian government, under President Kikwete's leadership, committed to making reforms in the energy sector. With support from the Millennium Challenge grant, General Electric, and Symbion, they got it up and running again. More Tanzanians got electricity.

So Power Africa embraces this model. Public and private resources will be matched with projects led by African countries that are taking the lead on reform. In this case, African governments commit to energy reforms. And the U.S. is committing some $7 billion in support, and private sector companies have already committed more than $9 billion. And this is just the beginning -- because we look forward to even more companies joining this effort.

Soma zaidi: http://www.whitehouse.gov/the-press...ks-president-obama-ubungo-symbion-power-plant

Hivi hizo shule huwa mnaenda kusomea ujinga?
 
Dah! ikiwa hujuwi ulichofaidika, ni vigumu sana kukuelewesha, lakini ntakupa darsa dogo la halafu wewe fatilia zaidi kama kweli unataka kuelewa:

Ubungo Plaza, Symbion Power Plant
Dar es Salaam, Tanzania
10:58 A.M. EAT

PRESIDENT OBAMA: Good morning, everybody. Please have a seat. It is wonderful to be here with President Kikwete. I want to thank everybody from Ubungo Power Plant for this visit. We are here today to focus on one of the biggest hurdles to Africa’s economic development -- the fact that nearly 70 percent of Africans lack access to electricity.
And that’s why in my speech in Cape Town I announced a major new initiative -- Power Africa -- to double access to electricity here in Africa. Now, the first step that we’re going to take is to try to bring electricity to 20 million homes and businesses.

And this plant represents the kind of public-private partnership that we want to replicate all across the continent. This facility was idle. But the Tanzanian government, under President Kikwete’s leadership, committed to making reforms in the energy sector. With support from the Millennium Challenge grant, General Electric, and Symbion, they got it up and running again. More Tanzanians got electricity.

So Power Africa embraces this model. Public and private resources will be matched with projects led by African countries that are taking the lead on reform. In this case, African governments commit to energy reforms. And the U.S. is committing some $7 billion in support, and private sector companies have already committed more than $9 billion. And this is just the beginning -- because we look forward to even more companies joining this effort.

Soma zaidi: http://www.whitehouse.gov/the-press...ks-president-obama-ubungo-symbion-power-plant

Hivi hizo shule huwa mnaenda kusomea ujinga?

Hakuna kitu umeandika apo marais wanne unajibu kingine
 
Malipo ya Mungu ni so complex hata kwenda jehanam ni sehemu moja ya malipo.
 
Back
Top Bottom