tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,835
- 18,248
Kada maarufu wa CCM na aliyewahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema, anatazamiwa kuchukua fomu za kuwania kuteuliwa na chama chake kugombea nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mapema wiki hii. "Haiko wazi ni tarehe gani rasmi atafanya hivyo lakini, kwa vyovyote vile, itakuwa ndani ya wiki hii". "Alisema mpambe wake mmoja".
Kuchukua fomu kwa kada huyo nguli wa CCM kutafanya jumla ya watia nia kutoka mkoani Mara kufikia 5. Mpaka sasa makada 4 kutoka Mara wameishachukua fomu za kuwania uteuzi.
Jaji Werema alijiudhuru wadhifa wake wa AG kufuatia kashfa ya ESCROW ambayo bado inaendelea kuitikisa nchi. Pia Werema aliwahi kumuita Mbunge Kigoma kusini, Dr David Kafulila, jina la TUMBILI baada ya mbunge huyo kumuandama sana na tuhuma za Escrow bungeni.
MAONI YANGU
Naona ndoto za urais wa nchi hii kurejea mkoa wa Mara zinakaribia kutimia. Mpigania uhuru na Rais wa kwanza wa Tanzania, Mtakatifu Julius Kambarage Nyerere, ni mwenyeji wa mkoa wa Mara.
:israel:
Kuchukua fomu kwa kada huyo nguli wa CCM kutafanya jumla ya watia nia kutoka mkoani Mara kufikia 5. Mpaka sasa makada 4 kutoka Mara wameishachukua fomu za kuwania uteuzi.
Jaji Werema alijiudhuru wadhifa wake wa AG kufuatia kashfa ya ESCROW ambayo bado inaendelea kuitikisa nchi. Pia Werema aliwahi kumuita Mbunge Kigoma kusini, Dr David Kafulila, jina la TUMBILI baada ya mbunge huyo kumuandama sana na tuhuma za Escrow bungeni.
MAONI YANGU
Naona ndoto za urais wa nchi hii kurejea mkoa wa Mara zinakaribia kutimia. Mpigania uhuru na Rais wa kwanza wa Tanzania, Mtakatifu Julius Kambarage Nyerere, ni mwenyeji wa mkoa wa Mara.
:israel: