BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,118
Kundi la Majaji na Wanasheria mashuhuri ambao ni wanachama wa Jukwaa la Majaji na Wanasheria wa Afrika limewasili nchini Kenya kwa ajili ya kuangalia na kisha kutoa taarifa ya mchakato wa kesi ya Pingamizi la Urais katika Mahakama Kuu.
Ujumbe huo unaongozwa na Mohammed Chande Othman, Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, wengine ni Jaji Lilian Tibatemwa-Ekirikubinza wa Mahakama Kuu ya Uganda, Jaji Ivy Kamanga kutoka Mahakama ya Rufaa ya Malawi, Jaji Moses Chinhengo wa Mahakama Kuu ya Rufaa ya Lesotho na Jaji Henry Mbha, Rais wa Mahakama ya Uchaguzi ya Afrika Kusini.
Majaji hao watahudhuria vikao vyote vya Mahakama Kuu na kuandika mashauri kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Haki za Binadamu, pia watachanganua jukumu na uhuru wa Idara ya Mahakama katika kuchunguza mizozo ya uchaguzi pamoja na kupitia hali ya kijamii na kisiasa katika maandalizi ya maombi hayo.
Ujumbe huo unaongozwa na Mohammed Chande Othman, Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, wengine ni Jaji Lilian Tibatemwa-Ekirikubinza wa Mahakama Kuu ya Uganda, Jaji Ivy Kamanga kutoka Mahakama ya Rufaa ya Malawi, Jaji Moses Chinhengo wa Mahakama Kuu ya Rufaa ya Lesotho na Jaji Henry Mbha, Rais wa Mahakama ya Uchaguzi ya Afrika Kusini.
Majaji hao watahudhuria vikao vyote vya Mahakama Kuu na kuandika mashauri kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Haki za Binadamu, pia watachanganua jukumu na uhuru wa Idara ya Mahakama katika kuchunguza mizozo ya uchaguzi pamoja na kupitia hali ya kijamii na kisiasa katika maandalizi ya maombi hayo.