Kenya 2022 Jaji Othman Chande kuongoza Majaji waangalizi wa Pingamizi la Urais

Kenya 2022 General Election

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Kundi la Majaji na Wanasheria mashuhuri ambao ni wanachama wa Jukwaa la Majaji na Wanasheria wa Afrika limewasili nchini Kenya kwa ajili ya kuangalia na kisha kutoa taarifa ya mchakato wa kesi ya Pingamizi la Urais katika Mahakama Kuu.

Ujumbe huo unaongozwa na Mohammed Chande Othman, Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, wengine ni Jaji Lilian Tibatemwa-Ekirikubinza wa Mahakama Kuu ya Uganda, Jaji Ivy Kamanga kutoka Mahakama ya Rufaa ya Malawi, Jaji Moses Chinhengo wa Mahakama Kuu ya Rufaa ya Lesotho na Jaji Henry Mbha, Rais wa Mahakama ya Uchaguzi ya Afrika Kusini.

Majaji hao watahudhuria vikao vyote vya Mahakama Kuu na kuandika mashauri kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa vya Haki za Binadamu, pia watachanganua jukumu na uhuru wa Idara ya Mahakama katika kuchunguza mizozo ya uchaguzi pamoja na kupitia hali ya kijamii na kisiasa katika maandalizi ya maombi hayo.
 
Tujutane kuanzia tarege 31
20220829_104308.jpg
 
hii Tanzania ambayo Manyang'au wana ibeza kumbe ndio wanayo ililia kwa ajili ya mustakhabari wao...

Kiongozi wa waangalizi JK
Kiongozi wa Waanglizi Chande

Afrika mashariki yote hii mmeshindwa tafuta hata kutoka Somalia, Sudan, Burundi na Kongo?

Mkija hapa kelele kibao...
 
Duh....Tanzania tumekuwa tu 'waangalizi' wa wenzetu wakitekeleza demokrasia ya kweli. Toka marais wastaafu hadi majaji...waangalizi!
 
Tanzania haiwasikilizi wazee hawa, sasa jumuiya za kimataifa zinawatumia.

TOKA MAKTABA:
On 18-19 October 2016, the Africa Group for Justice and Accountability and the Wayamo Foundation hosted International Symposium on the theme, “Towards a System of International Justice” in Arusha, Tanzania. Mohamed Chande Othman, the Chief Justice of Tanzania, and member of the Africa Group for Justice Accountability, reflects on the symposium and on justice systems in Africa
 
Chande enzi za mwendazake alikaa kimyaaaaa mpk jiwe siku 1 akamsifia akasema 'angalia wazee wetu Kama wakina jaji Chande wamestaafu zao wametulia kimyaaaaaa'.


Jiwe aliwaweza wastaafu,hakuna Cha kulalamika mambo ya haki za binadamu Wala Nini hahahah.
 
Chande enzi za mwendazake alikaa kimyaaaaa mpk jiwe siku 1 akamsifia akasema 'angalia wazee wetu Kama wakina jaji Chande wamestaafu zao wametulia kimyaaaaaa'.


Jiwe aliwaweza wastaafu,hakuna Cha kulalamika mambo ya haki za binadamu Wala Nini hahahah.


kitabu cha Supremacy of Law
Kitabu cha Jaji mstaafu B. Samata kimeelezea mapungufu mengi ya law reports and reporting


15 Apr 2021

kitabu cha Supremacy of Law

Prof. Chris Maina Peter, Mhariri wa kitabu cha Supremacy of Law akikichambua kitabu cha Supremacy of Law, cha Judge Mkuu Mstaafu, Barnabas Samatta, akikielezea nini kilichopo ndani ya kitabu hicho

  • Kesi ya rais awajibike kwa matendo yake
  • Lumumba to Mlimani journey
  • Army mutiny
  • Kesi ambazo Judge Samatta aliziamua toka akiwa acting judge mpaka jaji kamili
  • Vitu anavyokumbuka jaji Samatta
  • "A judge who is not independent, he or she is not a judge"
  • Mapungufu makubwa katika Law Reporting nchini Tanzania, Tanzania inaweza kuchukua miaka 16 kabla ya kutiwa ktk Law Report wakati nchi zingine wanachapisha chapuchapu
  • Advocates maarufu Eric Ng'maryo na Jenerali Ulimwengu hawakubali Jaji Samatta astaafu na kupotea, waapa watamfuatilia ili aendelea kuelimisha umma
  • Kwa kirefu kuna sehemu kubwa 8 ndani ya buku hili kubwa muhimu kusomwa
Source : Ngowi TV


Rejea zaidi za mhimili wa mahakama :

 
kitabu cha Supremacy of Law
Kitabu cha Jaji mstaafu B. Samata kimeelezea mapungufu mengi ya law reports and reporting


15 Apr 2021

kitabu cha Supremacy of Law

Prof. Chris Maina Peter, Mhariri wa kitabu cha Supremacy of Law akikichambua kitabu cha Supremacy of Law, cha Judge Mkuu Mstaafu, Barnabas Samatta, akikielezea nini kilichopo ndani ya kitabu hicho

  • Kesi ya rais awajibike kwa matendo yake
  • Lumumba to Mlimani journey
  • Army mutiny
  • Kesi ambazo Judge Samatta aliziamua toka akiwa acting judge mpaka jaji kamili
  • Vitu anavyokumbuka jaji Samatta
  • "A judge who is not independent, he or she is not a judge"
  • Mapungufu makubwa katika Law Reporting nchini Tanzania, Tanzania inaweza kuchukua miaka 16 kabla ya kutiwa ktk Law Report wakati nchi zingine wanachapisha chapuchapu
  • Advocates maarufu Eric Ng'maryo na Jenerali Ulimwengu hawakubali Jaji Samatta astaafu na kupotea, waapa watamfuatilia ili aendelea kuelimisha umma
  • Kwa kirefu kuna sehemu kubwa 8 ndani ya buku hili kubwa muhimu kusomwa
Source : Ngowi TV


Rejea zaidi za mhimili wa mahakama :


Thnxs mkuu.
 
Back
Top Bottom