JAJI MKUU atua Arusha kwa Lema


Mkuu wangu Ritz nadhani utakubalina na mimi kwamba wanaoshinda kesi yoyote iwe ya jinai au civil case mara nyingine utakuta wanashinda kwasababu ya uhodari wa mawakili wanaowawakilisha na si kwamba wana haki sana.

Katika kesi ya Bwana Lema na wanachama wa CCM yapo mambo kadhaa ambayo kama yangezingatiwa Lema asingechomoka hata kidogo lakini kwa mshangao wa wengi wanaCCM walimfungulia kesi either walishindwa kujipanga au hawakupewa ushirikiano wa kutosha na muathirika mkuu Dr Batilda na uongozi wa CCM mkoa wa Arusha.

Kwa maoni yangu Dr Batilda angetakiwa binafsi amshitaki Lema.Hilo halikufanyika badala yake wakajitokeza wanachama wa CCM ambao walidai matusi ya Bwana Lema yaliwaathiri na kupelekea mgombea wao Dr Batilda kushindwa.Mengine tuwaachie majaji wenyewe wana akili na ujuzi wa kupembua chuya na mchele.

Kwakuwa Dr Batilda hakumshitaki Bwana Lema ilitarajiwa na wengi angekuwa shahidi muhimu hasa ikizingatiwa aliyedhalilisha ni yeye na si wanachama wa CCM au chama cha mapinduzi.Kwa mshangao wa wengi Dr Batilda hakujitokeza mahakamani.

Ilitarajiwa wakili wa wanachama wa CCM wangewasilisha ushahidi wa video kwakuwa ulikuwepo lakini nao pia hakutumika mahakamani !.

Hukumu haikuwa na case law pia jaji alikosea kumkataza Bwana Lema asigombee kwasababu hapakuwa na mashitaka ya rushwa ambayo yanakipengele cha kumzuia anayepatikana na hatia kutogombea.Niko tayari kusahihishwa Mheshimiwa Steven Wasira aliwahi kuzuiliwa kugombea katika kesi aliyofunguliwa na Mhe Jaji Warioba.

Ninaamini Bwana Lema atashinda si kwasababu hakumkashifu Dr Batilda bali ni ubovu wa mawakili wa wanachama wa CCM kwa kutoiandaa kesi vyema na ubovu wa jaji aliyewapa ushindi.Ifahamike wazi ni kweli yapo baadhi ya maneno yaliyotamkwa na Bwana Lema hasa sakata la Redio Safina kama yangewasilishwa vizuri mahakamani Lema asingekuwa na jeuri ya kukata rufaa.
Nyongeza, na kwa wale ambao ni wageni hapa JF au ambao hawamfahamu huyu Member mwenzetu Ngongo huyu jamaa hampendi hata chembe Lema na haitokaa aje kumpenda. mwenye akili zake timamu anajuwa ni nini nimeongea na Ngongo ni mkweli kiasi gani kutoka moyoni mwake licha ya kwamba hampendi hata chembe Lema.
Ngongo hongera sana kwa hili kwamba nimepata kitu kutoka kwako na nitakutumia pm ni kwa nini unamchukia Lema huenda una sababu za msingi sana. viwavi wadandia hoja hawawezi kukuelewa ila naelekea kukuelewa.
 
Last edited by a moderator:
kumbe Lema ni Mbunge wa Mkoa, kwa vigezo vyako basi wabunge wa CCM hawahitajiki kabisa.
 
Lema sasa hivi anaogopa hata mgambo wa manispaa kumbe ubunge ndio ulikuwa unampa kiburi na majigambo.
 
Kuna harakati zinaendelea pale Arusha mjini natapa wasiwasi lakini tunaambiwa tusiupe nafasi uoga na bahati zuri kwetu chadema uchaguzi hata ukirudiwa upepo kwetu siyo mubaya...
nimepatwa na wasi wasi.........
 
Next to Impossible, tarehe 20 mwili wa baba yake ndio unaagwa Tegeta Dar kuelekea Singida na kuzika ni Jumamosi, kama Rufaa itasikilizwa mfulululizo Lisu ni wa kumtegemea kuanzia Jumatatu. ila Wanasheria wenyewe wanajuwa namna ya kuendesha mambo yao. Lisu he know how to handle those matters.

kaka huku kwetu majita ni shida kweli kweli hapo pekundu.
 
Mwaka mmoja bila Madiwani! Miezi sita bila Mbunge! hata kama Lema atapigwa chini lakini jimbo la Arusha mjini ni la wapinzani na CCM wanalijua hilo!
 
Na pia isitoshe ni kua kwa habari nilizozipata kutoka chumba cha habari ndani ya chama cha CCM nikua pamoja na ujasiri wa wao kua wanaweza kushinda hii kesi kwaupande mwingine pia wanaogopa mno kurudia uchaguzi huu kwakua kwanza hawana uhakika wa kushinda na isitoshe pia wanaogopa kupoteza hela na la mwisho pia chama chao kinaukata! TIME WILL TELL!
 
Jurisdiction ipi? Ni suala la jurisdiction kivipi? Hebu itaje hiyo jurisdiction halafu useme mahakama yake iko wapi.

Hivi Arusha kuna Mahakama ya Rufaa? Manake kama ipo inabidi kuwe na jaji wake huko huko! Na kama hakuna sasa huyu Jaji Mkuu anaenda kusikiliza kesi kwenye mahakama gani, ya kata au chini ya mwembe? This is a mindless arrangement! What do you mean ni suala la jurisdiction, jurisdiction ipi?

Mfumo unaomsafirisha jaji kuifata kesi kwa gharama na hasara kwa walipa kodi ni mbovu, usinipe sheria, huo mfumo mzima wa sheria hizo ndio nasema mbovu! Halafu wanasheria wa kibongo ni wepesi mno, ungekuwa makini ungesema hiyo sheria in a nutshel inasemaje kuhusu hoja yako, sio kunambia kasome chapter 84 to 85! Inasemaje?

hii inaonyesha ni jinsi .gani shule za kata .zitahadhiri umoja wa taifa letu .kwani kwa hoja yako ina maana umesoma msingi ,secondary ,high ,na labda chuo .kwenye hiyo hiyo kata yako ya shimo la udongo ..kiasi sasa ujui kama Arusha kuna mahakama na mahakama kuu ya kanda ya kasikazini ? Hapana shaka wewe ni huzuni kwa baba yako .na uchungu kwa mama yako kwakukuzaa ,na hasara kwa maendeleo ya nchi .
 
Jaji kachaguliwa na Rais na huyo Rais katokea Chama Cha Majangiri a.k.a CCM, na huyo aliekata rufaa ni mpinzani...Je! haki itapatikanwa hapo?......mna Bosi wa jaji ni Kikwete sasa atatetea Chama Cha Majangiri au atafanya vile haki inavyotakiwa??? ukweli hapa Tanzania hakuna haki kwa mpinzani wala masikini.....CCM OYeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
Acha kulilia kwani hao wapinzani na wa vyama tawala walioshindwa na kushinda majaji wameteuliwa na nani?Tu
 
Haki lazima itendeke,wananchi wanayo haki ya kumpata mbunge wao kwa wakati muafaka.Siasa zisizo na tija zinaendelea kupoteza mashiko


Kumekucha watanzania na wapenda haki.Jaji Mkuu wa Tanzania,Mheshimiwa Mohamed Chande Othman tayari amewasili jijini Arusha kwa ajili ya kusikiliza rufaa ya Mh.Godbless Lema. Jaji Mkuu,katika jopo la Rufaa,atakuwa na Majaji Massati(wa Zombe) na Kimario. Rufaa ya Mh.Lema imepangwa kuanza kusikilizwa kuanzia tarehe 20/9/2012 katika Mahakama ya Rufaa kituo cha Arusha.

Hii inafuatia kuwasilishwa kwa hoja za rufaa na pande za kesi husika kimaandishi(written submissions) kama inavyotakiwa na Kanuni za Mahakama ya Rufaa,2009(kanuni ya 106). Arusha wanahitaji Mbunge.Walimchagua Lema na bado wanamhitaji.Wanaisubiri Mahakama ya Rufaa kuamua.
 
Kuna harakati zinaendelea pale Arusha mjini natapa wasiwasi lakini tunaambiwa tusiupe nafasi uoga na bahati zuri kwetu chadema uchaguzi hata ukirudiwa upepo kwetu siyo mubaya...
Tunafuatilia kwa makini, maana mambo yako wazi mno, hata kwa sisi tusiojua sheria.
 
Kuna harakati zinaendelea pale Arusha mjini natapa wasiwasi lakini tunaambiwa tusiupe nafasi uoga na bahati zuri kwetu chadema uchaguzi hata ukirudiwa upepo kwetu siyo mubaya...

sijapenda ulivyotumia hiyo sentensi ati upepo kwetu sio mmbaya" hiyo kauli mbiu ya sisiem ya kikwete
 
hivi maana ya haki kutendeka in this case ni lema kushinda only?haaa haaa haaa daaa kweli kuna wapuuzi wengi humu ndani
 
Arusha ilikuwa shwari baada ya huyu mwehu kupigwa chini,sala zetu zote ni kuhakikisha hoja zake zote zinatupiliwa mbali ili amani ya bwana iendelee kudumu.. Ameeeeeeeeen!!!

Wewe ndio mwehu kabisa......wala hujui ukisemacho!
 
Back
Top Bottom