JAJI MKUU atua Arusha kwa Lema

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kumekucha watanzania na wapenda haki.Jaji Mkuu wa Tanzania,Mheshimiwa Mohamed Chande Othman tayari amewasili jijini Arusha kwa ajili ya kusikiliza rufaa ya Mh.Godbless Lema. Jaji Mkuu,katika jopo la Rufaa,atakuwa na Majaji Massati(wa Zombe) na Kimario. Rufaa ya Mh.Lema imepangwa kuanza kusikilizwa kuanzia tarehe 20/9/2012 katika Mahakama ya Rufaa kituo cha Arusha.

Hii inafuatia kuwasilishwa kwa hoja za rufaa na pande za kesi husika kimaandishi(written submissions) kama inavyotakiwa na Kanuni za Mahakama ya Rufaa,2009(kanuni ya 106). Arusha wanahitaji Mbunge.Walimchagua Lema na bado wanamhitaji.Wanaisubiri Mahakama ya Rufaa kuamua.
 
Jaji kachaguliwa na Rais na huyo Rais katokea Chama Cha Majangiri a.k.a CCM, na huyo aliekata rufaa ni mpinzani...Je! haki itapatikanwa hapo?......mna Bosi wa jaji ni Kikwete sasa atatetea Chama Cha Majangiri au atafanya vile haki inavyotakiwa??? ukweli hapa Tanzania hakuna haki kwa mpinzani wala masikini.....CCM OYeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Ipo wazi rufaa ya Mh. Lema hata hakimu aliyetoka shule anaamua na kutoa haki, wakipindisha uma utawahukumu.
 
Kumekucha watanzania na wapenda haki.Jaji Mkuu wa Tanzania,Mheshimiwa Mohamed Chande Othman tayari amewasili jijini Arusha kwa ajili ya kusikiliza rufaa ya Mh.Godbless Lema. Jaji Mkuu,katika jopo la Rufaa,atakuwa na Majaji Massati(wa Zombe) na Kimario. Rufaa ya Mh.Lema imepangwa kuanza kusikilizwa kuanzia tarehe 20/9/2012 katika Mahakama ya Rufaa kituo cha Arusha.

Hii inafuatia kuwasilishwa kwa hoja za rufaa na pande za kesi husika kimaandishi(written submissions) kama inavyotakiwa na Kanuni za Mahakama ya Rufaa,2009(kanuni ya 106). Arusha wanahitaji Mbunge.Walimchagua Lema na bado wanamhitaji.Wanaisubiri Mahakama ya Rufaa kuamua.

nimepatwa na wasi wasi.........
 
Nina imani sana na Jaji Massati ni jaji asiyeyumbishwa ( mgombea binafsi) pia Chande, hawa ni majembe 90%, wana wa Arusha anzeni kushangilia ushindi, ila M4C itayumba...dah!
 
Massati ni jaji makini vibaya sana...we subiri utasikia nini kitaamuliwa ....i have a lot of trust on massati kuliko Chande.
 
nimepatwa na wasi wasi.........
Zombe hakuuwa Fact, pelekeni aliyeuwa amuhukumu.

Lema hajatukana mtu fact ndio maana Batilda Burhan hakushtaki wala hakutowa ushahidi.

Lema anarudishiwa Ubunge wake hili halina mjadala, na chombezo la Tundu Lisu kuhusu Majaji fake litachangia zaidi kutenda haki. hawa ni Learned Brothers, huwa hawapendi wastaafu huku wakiwa hawana credibility yoyote.
 
Chande bado anatafuta kazi UN. Hawezi kuchezea kitumbua chooni. Majembe TL yanamngojea acheze vibaya kijiji kinachoitwa Dunia kijue kila kitu.

Jembe Masati hawezi kukubali. Ni mwana mawazo huru!!
 
Arusha ilikuwa shwari baada ya huyu mwehu kupigwa chini,sala zetu zote ni kuhakikisha hoja zake zote zinatupiliwa mbali ili amani ya bwana iendelee kudumu.. Ameeeeeeeeen!!!
 
Kama kweli ccm na serikali yake wanataka utulivu ndani ya chama chao, basi watumia akili waliyoitumia kumvua Lema ubunge kumrudishia ubunge wake! Kitendo cha kumvua ubunge kimemwongeze umaarufu na kumpa nafasi ya kuwamaliza kupitia m4c!
 
Vipi kuhusu Tundu Lisu kufiwa na baba yake? Ataweza kweli kuwepo kwenye shauri hiyo siku?
 
Nathalia Kimaro alikuwa na Massati kwenye mgombea binafsi, Chande ndiye aliyemuachia Justin Nyari akiwa jaji wa mahakama kuu akitokea mahakama kuu kanda ya mbeya. Jaji mkuu Chande ni mmoja kati ya waliolalamikiwa na Lissu kuwa hakufikisha miaka 9 kama jaji wa mahakama ya rufaa ili awe na sifa ya kuiwa jaj mkuu
 
Tunamuombea kwa mola arudishiwe ubunge wake. Mh lema kaa tayari mambo yanaweza kuwa ya ukweli maana hawa waheshimiwa majaji ni watu makini sana.
 
Vipi kuhusu Tundu Lisu kufiwa na baba yake?? Ataweza kweli kuwepo kwenye shauri hiyo siku??

Next to Impossible, tarehe 20 mwili wa baba yake ndio unaagwa Tegeta Dar kuelekea Singida na kuzika ni Jumamosi, kama Rufaa itasikilizwa mfulululizo Lisu ni wa kumtegemea kuanzia Jumatatu. ila Wanasheria wenyewe wanajuwa namna ya kuendesha mambo yao. Lisu he know how to handle those matters.
 
Arusha ilikuwa shwari baada ya huyu mwehu kupigwa chini,sala zetu zote ni kuhakikisha hoja zake zote zinatupiliwa mbali ili amani ya bwana iendelee kudumu.. Ameeeeeeeeen!!!

sasa we na yeye nani mwehu?
Amani ya Arusha itarudi Jembe letu litakaporejeshwa bungeni!
 
Arusha ilikuwa shwari baada ya huyu mwehu kupigwa chini,sala zetu zote ni kuhakikisha hoja zake zote zinatupiliwa mbali ili amani ya bwana iendelee kudumu.. Ameeeeeeeeen!!!

Ni Arusha ipi hiyo mkuu. Mbona sisi tuliopo huku tunajawahi kusali kuomba hayo unayosema!
 
Arusha ilikuwa shwari baada ya huyu mwehu kupigwa chini,sala zetu zote ni kuhakikisha hoja zake zote zinatupiliwa mbali ili amani ya bwana iendelee kudumu.. Ameeeeeeeeen!!!

Akili kama ni za kitwana sana, yaani unashindwa kufikiri kitu kidogo kama hicho!!!!!
 
Nina imani sana na Jaji Massati ni jaji asiyeyumbishwa ( mgombea binafsi) pia Chande, hawa ni majembe 90%, wana wa Arusha anzeni kushangilia ushindi, ila M4C itayumba...dah!

Mhe.Jaji Kimario alikuwa mmoja wa majaji watatu walioamua rufaa yangu pia. Hili ni jopo lisiloyumbishwa. Huwa linapenda kufanya kazi kwa standard ya kuweka Case study nzuri kwa ajili ya mifano siku zijazo.. Nawaamini.
 
Back
Top Bottom