Jaji Ihema, Kumbe Tundu Lissu alikuwa sahihi...

Chezea Tundu Lissu wewe, huyu jamaa kila anacho kisena huwa ameisha kifanyia research ya kutosha, alitoa kama tahadhari na sasa leo tumeona!
 
Ripoti ya kamati haikuwekwa wazi kama wananchi walivyotaka na imefichwa fichwa eti kwa kuogopa kuingilia uhuru wa mahakama,hivi hii tabia itaisha lini ya kuwahadaa watu wasizungumze mambo ambayo yapo mahakamani?Kwani mahakimu wetu utashi wao kimaamuzi una mashaka kiasi kwamba tunaogopa kuongelea mambo ambayo yapo wazi?
Siku za ukombozi zinakaribia na usanii huu wanaotupa utaisha.
 
...jamani huyu IHEMA mkumbeni kuwa ndo huyu alotajwa na Tundu Lisu kuwa hakuwa na hata tu uwezo wa kuandika hukumu alipokuwa Mahakama Kuu. Je vp angekuwa na uwezo wa kuandika ripoti nzuri leo? Wenye akili ndo mtaanza sasa kumkubali Tundu-Lisu. Mind you: dhaifu ni dhaifu tu!!

Kweli kaka, ktk prison break kuna msemo unasema "Once a looser always a looser.."
 
Jaji Ihema ni moja wapo wa wale majaji vihiyo aliosema Tundu Lissu, gazeti la Mwananchi ni ant Chadema, kwa hiyo hakuna cha kushangaza hapo, sana sana tu uhuru wa Mahakama umeingiliwa kwa kumuona yule askari aliyerusha lile bomu hana hatia bali wenye hatia ni Chadema.Tuna subiri tamko la mahakama kwa kuingilwa majukumum yake na gazeti la Mwananchi
 
huyu jaji mstaafu amejivunjia heshima bila sababu, hii kamati yake itaibua mengi kuelekea katiba mpya hata hukumu zake sasa zitapitiwa, kama aliwahi kualamlungula sasa amejianika, kisutu inamsubiri kwa hamu
 
wana macho lakini hawaoni, wana masikio na hawasikii! ...huyu jaji naye sina uhakika kama alikuwa kwenye list ya Mh. Lissu

na hapa tanzania hakuna sheria wala utawala, huwezi ukafanyia uchunguzi jambo ambalo lipo mahakamani... maana kwa kutoa hiyo report maana yake tayari wamesha judge..kwa hiyo hakimu akihukumu kua polisi ndio wenye hatia tumsikilize nani..mahakama au tume ya uchunguzi? bongo bana...sijui hata nani ndio anaongoza hii nchi.
 
Gazeti la mwananchi limeanza kupoteza dira! Watanzania tunaujua ukweli! Kuanzia leo sitanunua gazeti la mwananchi.hawa wahariri waganga njaa wanatumika kama toilet paper.

usiwahukumu gazeti la Mwanachi wao wamechukua jukumu la kukusaidia kujua yaliyosemwa na tume ya waziri.
 
Kusema chochote si tatizo,bali kushindwa kueleza ukweli ni ubovu wa akili. Chanzo cha mauaji kitabaki kile kile cha dola kutaka kunyamazisha harakati za mabadiliko ya kweli Tanzania
 
Tusilaumu gazeti la mwananchi kama kweli walichokiandika ndicho kilichopo kwenye Ripoti ya Ihema badala yake tuwapongeze kwa kuandika ukweli kama ulivyo kwenye ripoti. Ukweli kuhusu kifo cha Mwangosi hakuna asiyejua, tunachokifanya hapa ni kuangalia je ukweli tunaoujua sisi uko reflected kwenye hiyo ripoti? Kama hauko reflected then we conclude kwamba Iheme na waliomtuma wote ni wahuni na na hukumu ya mwenye haki juu yao hawawezi kuiepuka.

Mwananchi iko sahii kuandika kilichoko kwenye ripoti kwa kuwa hata kabla ya ripoti na tume kuundwa tayari tunajua ukweli, na ripoti ilichokiandika ndicho hicho watu walikipinga kwa kuonyesha picha za mauaji kwa wale ambao walikuwa hawajui na kila mmoja alikiri kuhusika kwa polisi na si CDM!
 
tatizo lake huyu muda wote yupo kwenye MMU atayaonea wapi haya matukio? mzee wa malavidavi huyo
 
Hujui kuwa Jaji Ihema ndiye alieongoza tume ya Nchimbi kuhusu mauaji ya Mwangosi?
Hujui kuwa amesoma ripoti yake leo, pamoja na mambo mengne akidai
"NGUVU YA POLISI ILIYOTUMIKA KUTAWANYA WATU, HAIKUHUSIKA KUMUUA Mwangosi!"
Na kwamba hawawezi kutaja chanzo cha kifo, wataingilia mahakama!
Sasa ambacho hukuelewa ni nini ewe kichwa ngumu?
hahhaha,,,,,sasa mdau unadhan watu wanaelewa dots zote za events,,,,,???wengine hawajui,mueleweshe tu taratibu
binadam wote vichwa vyao vigume,chako laini????
 
Hakuna Jaji pale wakati akisoma roho ilikuwa inamsuta hadi anatetemeka........hakika huu ni ujinga

Asipofanya hivo watoto wake watakula wapi? TAFAKARI ndo TZ ya sasa maadili yamepotea. HIVI huyu IHEMA Alisoma Chuo kipi?
 
Bora hata umenisaidia, nilikuwa najiuliza nimuelezeeje bwana Kichwa ngumu, maana mambo haya yako wazi leo nzima, halafu eti yeye hajasikia na wala haelewi!

taab kwei kweli, huyu jamaa anaishi dunia gani?? Tatizo lake anatumia muda wote kule MMU atayajulia wapi matukio?? Mzee wa malavidavi huyu msameheni bure
 
Uchunguzi wa tukio la uhalifu daima hufanywa na polisi na baadaye kupelekwa mahakamani kama ushahidi.

Mkuu huyu jaji kasema jana hawawezi kwenda further kwa sababu wataingilia kesi ilio mahakamani,swali linakuja wakati anapewa kaz ya kuchunguza hakujua kama kesi ipo mahakamani? mkuu huyu jaji ni hopeless ndio naungana na maandishi ya mchambuzi

Kwa nyakati fofauti, wengi wetu tumejifunza katika historia ya nchi yetu kwamba moja ya sababu za msingi ambazo Mwalimu Nyerere alizitaja miaka 50 iliyopita kwamba ni kikwazo kwa Maendeleo ya taifa letu ni uhaba wa wataalam wa kusaidia kujenga taifa. Hivyo, katika miaka ya mwanzo ya uhuru, ilimlazimu Mwalimu na serikali yake kuagiza wataalam kutoka nje na hawa walikuwa wanalipwa na fedha za walipa kodi wa nchi yetu. Miaka 50 baadae, hali sio tofauti sana kwa maana ya kwamba bado kama taifa, hatuoni bado mchango wa kutosha kutoka kwa wataalam wetu katika kuendeleza nchi yetu. Tunabaki kujiuliza, tatizo ni nini hasa:
JokaKuu,
Ukitazama siasa za CCM, hiki sio chama kinacho appreciate wasomi tena tofauti na miaka ya mwalimu. Nimetolea mfano jinsi gani wasomi wa chuo kikuu walivyokuwa wanashirikishwa katika mijadala inayohusu hali ya nchi kisiasa, kiuchumi na kijamii. Nina kitabu kimoja kinachoelezea pia ni jinsi gani Mwalimu Nyerere alipata ujasiri wa kuingiza nchi yetu kwenye ujamaa kutokana na wasomi wengi wa Mlimani kukubaliana na mtazamo wake, tatizo likaja tu baadae kwenye utekelezaji. Miaka ya sasa, tuna wasomi wengi sana na wenye hekima sana kutokana na elimu yao na uzoefu wao lakini hawatumiki ipasavyo na wakitumika ni kwa malengo ya kisiasa peke yake na wakishatumika na kufanikishia watawala malengo yao, shughuli yao imekwisha. Pia Tazama tume ya katiba, wengi ya walioteuliwa mle ni kwa malengo ya kisiasa tu; inastaajabisha kuona mawakili wa katiba (constitution lawyers) kama Professor Shivji wanaachwa katika tume hii; hakuna msomi anayejulikana ndani na nje ya nchi kuhusu utafiti wake katika masuala ya katiba kama Issa Shivji; Wasomi wengi walioteuliwa mle ni wale wenye political orientation ya CCM - hili halina mjadala, kama wapo wenye mtazamo ambao ni no-partisan basi ni wachache sana. Na wanasiasa wengi walioteuliwa mle ni kwa ajili ya to heal political wounds, na sio vinginevyo.
The bottom line ni kwamba wasomi wanapotumika kama unavyosema, basi mara nyingi huwa on a partisan way (kwa malengo ya kisiasa - CCM), na sio non-partisan (kwa maslahi ya taifa over and above party politics).
 
mimi nakushangaa wewe uliyekuwa unategemea haki itendwe na serikali hii, wewe unafikiria kwanini serikali ilikataa kuunda Tume huru yenye nguvu ya kisheria kwa sababu wana nia ya kuwalinda watu wao conclusion yako uliyofikia leo wenzako akiwemo Tundu Lissu walishafikia mwezi uliopita. siku nyingine uwe unasikiliza ushauri wa bure wa chadema hautoumia kichwa tena mkuu.

Nilimwelewa Lissu siku nyingi mkuu, ila sikutarajia Ihema mwenyewe angejitokeza hadharani na kuuthibitishia umma kwamba yeye ni dhaifu na feki mapema namna hii, na ndio msingi wa uzi huu.
Pia nimeshangazwa na usaliti wa Makunga, mhariri wa gazeti nililokuwa naliamini, nilitarajia atoe ripoti mbadala!
 
I salute You Hon. Tundu Lissu, wengine huwa hatuamini hadi tushike kovu la mkuki, nimelishika jana wakati mh jaji wakuchonga akisoma ripoti ya kifo cha Mwangosi, huu ni utumiaji mbaya wa mali za walipa kodi. Waziri Nchimbi anatakiwa aachie ngazi na alipe pesa zilizotumiwa na hao watu wake.
 
Back
Top Bottom