Jairo asimamishwa kazi

Status
Not open for further replies.
KATIBU Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo anadaiwa kuwakashfu wabunge kwa kuwafananisha na wasanii wa maigizo wa kikundi cha The Original Comedy. Jairo anadaiwa kutoa maneno hayo juzi nje ya ukumbi wa Bunge muda mfupi baada ya Bunge kuahirishwa na wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenda katika kikao chao kabla ya mjadala wa bajeti kuahirishwa juzi jioni.

Chanzo chetu cha habari kilichokuwa ndani ya kikao hicho cha wabunge wa CCM kiliiambia MTANZANIA juzi kuwa madai ya kashfa hiyo yaliwekwa wazi na Mbunge wa Mafia, Abdulkarim Shaha alipokuwa akichangia mada katika kikao hicho. Kwa mujibu wa chanzo hicho, Jairo alitoa lugha hiyo iliyoonekana kuwaudhi wabunge wa CCM baada ya kukutana na Shaha nje ya ukumbi wa Bunge.

"Tulipokuwa katika kikao chetu hali ilikuwa mbaya kwa sababu wabunge walikuwa wakitoa madukuduku yao kuhusu hali ilivyokuwa juu ya hiyo bajeti iliyokwamishwa. Wakati tunajadili, Shaha alisimama na kueleza jinsi Serikali inavyotakiwa kufanya kukabiliana na huu mgawo wa umeme ambako alipendekeza inunuliwe mitambo haraka iwezekanavyo na Jairo achukuliwe hatua za haraka kwa kuondolewa katika nafasi yake. Pamoja na maelezo mengi aliyosema, alituambia kuwa wakati wabunge tumetoka nje ya ukumbi wa Bunge baada ya Bunge kuahirishwa, alikutana na Jairo, wakazungumza kisha akamwambia sisi wabunge ni kama ‘comedy' hatumfanyi kitu hata tukifanyaje.

Aliposema hivyo, wabunge wakalipuka kwa hasira wakasema lazima huyu ang'oke kwa sababu anaonekana kuwa na kiburi kwa kuwa anateuliwa na Rais. Kauli hiyo ya Shaha ikaungwa mkono na Mbunge wa Shinyanya Mjini, Stephen Masele ambaye alipigilia msumari na kusema alichosema Shaha ni kweli kwa kuwa hata yeye alimsikia. Inaonekana kauli hiyo ya Shaha ilimshangaza Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ndiye alikuwa Mwenyekiti wa kikao kwani aliuliza, ni kweli amesema hivyo?, ‘Shaha akasema ni kweli, ‘I swear' (naapa) aliniambia," kilisema chanzo chetu.

http://www.newhabari.com/2011/07/20/jairo-kashfa-nyingine/
 
He is a scapegoat and he has to bear the consequences, furthermore his decision to circulate a letter asking for lobbying money was entirely puerile and perhaps he has now learned a lesson. However, as it is always been the case, he will soon be appointed to a new post.
 
huku nikopoteza mda na rasilimali za nchi uchunguzi gani wakati barua inajitosheleza??? au wanataka kusema ile hela ilikuwa for stationaries..!!!
 
amesema nini kuhusu ngeleja na watu wake, hiyo cabinet itafanya vipi kazi chini ya ngeleka kama mkuu wa wizara.!? Hili ni changa la macho wangestep down wote afu ndo uchunguzi ufanywe..
sasa Luhanjo na Ngeleja wapi na wapi? Huelewi tu kuwa Ngeleja sio saizi ya Luhanjo wala Pinda wala Ustaadh Bilal? Msubirini Mkwer.e arudi tu
 
Breaking news,hivi punde Katibu wa wizara ya nishati na madini Bwana,David Jairo amesimamishwa kazi,taarifa hiyo imetolewa na katibu mkuu kiongozi philemon Luhanjo ,amesimamishwa ili kupisha uchunguzi wa tuhuma anazokabiriwa nazo.source ITV breaking news.


Ni masihara mazima tu mkuu. Haiingii akilini ati walikuwa wanamsubiri rais afanye maamuzi na hivyo ndivyo alivyoamua. What a joke!!!
 
Breaking news,hivi punde Katibu wa wizara ya nishati na madini Bwana,David Jairo amesimamishwa kazi,taarifa hiyo imetolewa na katibu mkuu kiongozi philemon Luhanjo ,amesimamishwa ili kupisha uchunguzi wa tuhuma anazokabiriwa nazo.source ITV breaking news.
Nilisha comment kwenye ukurasa huu toka jana kuwa Kuwajibika pekee kwa serikali juu ya hili ni kumshtatim Jairo na Ngeleja na si kuwasimamisha kazi. Washitakiwe na haki dhidi ya watanzania walipakodi ionekane ikitendeka Karamagi Mabaha na Lowasa walijiuzulu hawajashtrakiwa adi leo. Chenge amefanya madudu yupo anapeta na serikali ilithubutu kumsafisha hajashtakiwa hadi leo. Jamani tuamke huu ni mchezo sasa.Walioiba kuku wanahukumiwa mara moja ila hawa wezi na wahujumu uchumi tunawaacha watanzania tusikubali.
 
Mimi nasema sio uonezi, kwa sababu mara zote anashikwa mmoja huyo atawataja wenzake kisha wote wataswekwa mahakamani. Ngeleja hatapua.
 
Pamoja na makosa mengine; hili la kula bila kunawa ndio litamfunga; tukumbuke mtoa rushwa na mpokea rushwa wote ni wahalifu; sijui wabunge waliopokea huo mshiko nao waunganishwe ndio tutakomesha huu ubazazi!
 
Breaking news,hivi punde Katibu wa wizara ya nishati na madini Bwana,David Jairo amesimamishwa kazi,taarifa hiyo imetolewa na katibu mkuu kiongozi philemon Luhanjo ,amesimamishwa ili kupisha uchunguzi wa tuhuma anazokabiriwa nazo.source ITV breaking news.

Kasimamishwa kazi kwa sababu zipi, serikali mbona inataka kutuingiza katika hasara ya waziwazi, huyu jamaa hana kosa wala hatia, akiingia mahakamani kudai fidia ni hela zetu ndiyo atakazolipwa.
 
Hawajasema lolote,eti amepisha uchunguzi jukumu alilokabidhiwa CAG,kwanini hajafukuzwa kazi kabisa?
Kwa nini TAKUKURU wasichunguze na kupeleka kesi mahakamani, kwa nini CAG ili kulefusha mambo, uozo mtupu!!!!!!! Magambazi in action!!!!!!!!! HATUDANGANYIKI!!!!!!!!!
 
huku nikopoteza mda na rasilimali za nchi uchunguzi gani wakati barua inajitosheleza??? au wanataka kusema ile hela ilikuwa for stationaries..!!!

Lazima mabilioni mengi yatafunwe ili "kufanya uchunguzi" kama ile barua kweli iliandikiwa na fisadi Jairo!!!!
 
Breaking news,hivi punde Katibu wa wizara ya nishati na madini Bwana,David Jairo amesimamishwa kazi,taarifa hiyo imetolewa na katibu mkuu kiongozi philemon Luhanjo ,amesimamishwa ili kupisha uchunguzi wa tuhuma anazokabiriwa nazo.source ITV breaking news.

Same old shyt kwa hizo chunguzi!..chunguzi ngapi zimefanyika hamna lolote!!Nchi hii basi tu ila tupo tupo na hii serikali ya ajabu!!
 
huku nikopoteza mda na rasilimali za nchi uchunguzi gani wakati barua inajitosheleza??? au wanataka kusema ile hela ilikuwa for stationaries..!!!
hapana mkuu ni ya kuwapatia chai na gahawa wahishimwa saaana!!
hahahahaaa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom