Jack Zoka astaafu

Jack Zoka astaafu

Status
Not open for further replies.
ngoja nitume maombi kujaza hilo pengo faster,nirudishe imani ya watanzania kwa serekali yao..
kesi ya kwanza ntakayoanza nayo ni kuhakikisha wezi wa kuku wote wanarudi uraiani,ili nipate vyumba vya kutosha magerezani kwa ajili ya mipapa ya madawa ya kulevya,majangiri,wachumia tumbo wote wenye utajiri ulopindukia usio na detail za kujitosheleza
Kwani Jack Zoka alikuwa ni Jaji au Hakimu?
 
twamtakia mapumziko mema ya kustaafu,karibu sana mtaani ambako hakuna kusaini posho za vikao,ni full mishemishe ndo mkono uende kinywani

Mzee atakuwa amejiandaa na maisha ya uswazi, siyo kama wabunge wetu wanaolilia posho wakafanye anasa na muda wao ukiisha wanaanza kurudia kazi zao za ujambazi.
 
Nasikia alikuwa mkuu wa kitengo cha siasa. Kazi yake ni nzuri sana na kila mtu atamkumbuka kwa yote aliyowafanyia Watanzania....lol!!

Pia wahanga wa jitihada zek hawatakaa wamsahau!
Kweli mkuu na kazi yake aliifanya barabara hadi kitengo kikajeuka cha siasa kabisa!!! Kuhakikisha mambo mengi yanafanyika kukiwezesha kilicho madarakani kuendelea kushika hatamu hata kama likishindwa 2010.
 
Sidhani kama ni kipimo tosha kuwa Usalama wa Taifa hawafanyi kazi. Ninachojua mimi ni kwamba kazi yao ni kuishauri serikali na siyo kuchukua hatua. Vile vile siamini kama kuwakamata wauza madawa ya kulevya, kukamata najangili ndiyo majukumu pekee ya Idara ya Usalama wa taifa.

Mkuu thatha, kwa kipindi hadi kufikia 2010 mpaka sasa kitengo hiki kinafanya siasa!!! Kumbe na member ametusaidia hapo juu kuwa kumbe alikuwa idara ya siasa!!! Kama matendo ya kihalifu yanatokea hasa ya mabomu na watu kutekwa kweli usalama uko wapi??? Wale mashushushu wa zamani wako wapi? Tunawataka hao!!! Jambo likipangwa tu baya walikuwa wanapangua!!! Sasa imekuwaje?? Wameua mapadre na kuwamwagia tindikali na mashehe pia!!! Kweli imeshindikana kufanya ushushushu!!! Sitaki kuamini sana unachosema hapa!!! Idara hii imeshindwa majukumu yake!!! Na polisi wanachukulia udhaifu wa usalama na hawatekelezi majukumu yao!!
 
Kama amavyo jina lako lilivyo, wewe ni BUNDI kati kati ya ndege mchana kweupeee, ndege watakuwa TISS wenzako sema siku wakikugundua utakoma, yaani unajua mpaka kipindi ambacho hamkufanya kazi eti ni kufikia 2010? TISS kazi kwenu, mna bundi kati yenu.

Mkuu thatha nimecheka sana, sena mimi nina upeo wa kuangalia mambo tu. Hao ndege bundi si ndugu yao, mimi ni Bundimkubwa wao ni bundi!!! Anyway, sasa hali si shwari na inabidi kufanyike mabadiiko ya kizalendo!!
 
Nasikia huko kwao wanamasifu sana kwan ameboresha masirahi ya wafanyakazi wengi wao wanatembelea magari

Kwao wapi mkuu? Kwao ni Bunda hakuna lolote kwa yeyeyote anaye kujua musoma ataelewa halisi ya maisha ya kule.Aje ashiriki nasi ulinzi wa sungusungu kando ya ziwa victoria.
 
Taarifa ni za kweli na sasa anajiandaa huenda akapata promosheni ya ubalozi nchini Venezuela namkumbuka zoka tangu yuko ubalozini ubelgiji aliporejea alikuwa chini ya mzee Magere. baadae ndio akapa hiyo nafasi.
Unathibitisha umbea?
 
Kama amelinda vizuri viongozi wa ccm ambacho ndo chama tawala, well done. Hilo lilikuwa ni jukumu lake na anastahili kupongezwa kwa hilo. CHADEMA subirini muda wenu ukifika nanyi mtalindwa vizuri na idara yetu mahiri


Mshangao wangu kama kastaafu ni jinsi ambavyo roho yake imekuwa mbaya hata katika uzee wake. Nilifikiriaga kuwa ni kijana tu anayesumbuliwa na nguvu za ujana, kumbe kabali hata wazee wanaziweza loh! Atapewa cheo kingine lakini soon, ubalozi..... mwenyekiti au mjumbe wa bodi flani, mkuu hawezi muacha achakalie nyumbani
 
Kazi zifanywazo na usalama wa taifa zinajumuisha mambo mengi ukisema madawa ya kulevya na ujangili haitoshelezi kusema ndio kazi pekee zifanywazo ndani ya idara hiyo nyeti kwa gorvenment, kuna masuala mengi sana ambayo yapo chini ya TISS ambayo huwezi kuyaorodhesha yote hapa
 
Kwao wapi mkuu? Kwao ni Bunda hakuna lolote kwa yeyeyote anaye kujua musoma ataelewa halisi ya maisha ya kule.Aje ashiriki nasi ulinzi wa sungusungu kando ya ziwa victoria.

wewe kama ni mtumishi wa Umma, jukumu la kustawisha maisha ya wananchi wa kijijini kwenu ni lako? aisee mbona CHADEMA viroba vinawapelekesha sana?
 
Kama source yako ni ya kweli, basi tumtakie kila la heri katika maisha yake nje ya system. Kuna mengi amefanya mazuri japo hayatasemwa au hayataonekana machoni kwa wengi tulioko uraiani na baadhi ya wana JF, basi yaigwe na vijana alowaacha nikiamini bado tuna vijana waadilifu wengi tu ndani ya system, pale ambapo hakufanya vizuri basi parekebishwe tukitegemea ufanisi katika kipindi hiki chenye changamoto nyingi kisiasa hasa kwa nchi zinazotuzunguka.
 
Kazi zifanywazo na usalama wa taifa zinajumuisha mambo mengi ukisema madawa ya kulevya na ujangili haitoshelezi kusema ndio kazi pekee zifanywazo ndani ya idara hiyo nyeti kwa gorvenment, kuna masuala mengi sana ambayo yapo chini ya TISS ambayo huwezi kuyaorodhesha yote hapa

Mleta mada atakuwa REDBRIGADE, anajua kazi yao ni moja tu, kumwagia watu TINDIKALI basi.
 
Kazi zifanywazo na usalama wa taifa zinajumuisha mambo mengi ukisema madawa ya kulevya na ujangili haitoshelezi kusema ndio kazi pekee zifanywazo ndani ya idara hiyo nyeti kwa gorvenment, kuna masuala mengi sana ambayo yapo chini ya TISS ambayo huwezi kuyaorodhesha yote hapa
 
Kama source yako ni ya kweli, basi tumtakie kila la heri katika maisha yake nje ya system. Kuna mengi amefanya mazuri japo hayatasemwa au hayataonekana machoni kwa wengi tulioko uraiani na baadhi ya wana JF, basi yaigwe na vijana alowaacha nikiamini bado tuna vijana waadilifu wengi tu ndani ya system, pale ambapo hakufanya vizuri basi parekebishwe tukitegemea ufanisi katika kipindi hiki chenye changamoto nyingi kisiasa hasa kwa nchi zinazotuzunguka.

hilo ndilo la msingi. Binadamu akifa, PADRE au SHEIKH anapowausia waliokusanika Makaburini huwa hamshutumu Marehemu bali anawaaza waliobaki kuishi katika matendo yampendezayo Mungu.
 
POLISI wanachukulia udhaifu wa usalama na hawatekelezi majukumu yao? ina maana POLISI wao wanategemea hiyo TISS ili kutekeleza majukumu yao? mkuu mimi siamini kama ni kazi ya TISS kwenda kwenye mikutano ya vyama vya siasa, ili kufanya nini?

Kule hawafanyi kazi waziwazi kama polisi!! wanakuwa kama askari kanzu tu!! Katika mkusanyiko wowote official ni lazima wanakuwepo!!!! How about informers!!!!! Kila mahali mwanausalama yupo!!!! Hata wauza mchicha na matenga yao!!!! Ha ha ha!!! Utasomaje kila category kama hawapo!!! Wewe!!!!!! Hata bar wapo, wanatuhudumia!!!! Jioni mkiondoka naye anakufyonza!!!! Sitaki kusema mengi, ila angalao ninapenda kujua mambo mengi na kuangalia movies imenisaidia sana kufahamu ufanyakazi wa idara za usalama duniani kote!!
 
Kweli mkuu na kazi yake aliifanya barabara hadi kitengo kikajeuka cha siasa kabisa!!! Kuhakikisha mambo mengi yanafanyika kukiwezesha kilicho madarakani kuendelea kushika hatamu hata kama likishindwa 2010.

Ndiyo hivyo mkuu....

Ila basi hawa jamaa wangekuwa na huruma kwa watanzania wenzio. Na labda wangetakia kukumbuka kuwa kuna siku nchi inatachukuliwa na watu wengine kutoka kwenye timu ya sasa!
 
duh yaani nchi yetu ipo uchi kiasi hiki hadi mtu akawa na access ya kujua viongozi waandamizi wa idara nyeti kama hii tena na mrithi wake? nadhani mtoa mada atakuwa ni mTISS aliyekiuka maadili ya kazi yake
sana tu mkuu. Hata mie nimeliona hilo. Hawa ndo wale wanaoropoti kwa watu na si kwa manufaa ya nchi
 
Ndiyo hivyo mkuu....

Ila basi hawa jamaa wangekuwa na huruma kwa watanzania wenzio. Na labda wangetakia kukumbuka kuwa kuna siku nchi inatachukuliwa na watu wengine kutoka kwenye timu ya sasa!
CCM itatawala daima. hakuna mwingine zaidi ya ccm
 
kweli mkuu wanapaswa kuchukuliwa hatua watu kama hawa kwani kwa nafasi aliyonayo anaweza kuwa agent wa watu wabaya kwa nchi yetu i.e RWANDA na akatuuza kiurahisi tu huyu jamaa..uzalendo kwanza

sana tu mkuu. Hata mie nimeliona hilo. Hawa ndo wale wanaoropoti kwa watu na si kwa manufaa ya nchi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom