Jack Cliff hatanyongwa wala kufungwa

Jack Cliff hatanyongwa wala kufungwa

Tupatie hiyo sheria inayosema kuwa atafungwa miaka 60 au kulipa faini ambayo hajulikani. Ni ajabu sheria kusema kuwa aliyekutwa na hatia atalipa faini bila kusema atalipa faini ya kiasi au hata kuweka kiwango cha juu au chini.

Kwa mujibu wa sheria Namba 17/2009 ya Macau, "punda" anayekutwa na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya nchini humo anatumikia kifungo cha miaka kati ya 3 na 15.

Ushauri wa bure na kwa faida yako: tafuta dissertation iliyoandikwa na Ho We Chong kama sehemu ya shahada yake ya uzamili Juni 2013 kwenye Chuo Kikuu cha Macau yenye kichwa cha habari: "A comparative study of punishment for drug trafficking crime in Greater China: With a historical overview and the current practices."

Then, soma zile sections zinazozungumzia sheria za Macau. Natumaini baada ya hapo utakuwa umepangusa vumbi kwenye ubongo wako.

Pia itakusaidia kutorukia na kuandika mambo ambayo hata huyajui. I doubt kama unajua adhabu ya kosa hilo kwa mujibu wa sheria za nchi yako.

Mkuu umetumia Gobore kuua mbu, kabla hujaja na ushauri wa juu ya kufuta vumbi kwenye ubongo wangu nadhani uanze na wa kwako.. nini maana ya Tetesi? Hizi ni tetesi tuu

Tanzania ukishikwa na madawa ya kulevya kwanza hatuna mdhamana na adhabu ya kifungo cha maisha itakuhusu. Nitashangaa sana kama Macau watakuwa na adhabu ya kizembe hivyo.

Nitapitia hiyo makala lakini nitafanya general overview sio kutumia muda wangu kutaka kujua sana kusiko kuwa na msingi.
 
Mkuu ahsante kwa elimu.

Naomba msaada kidogo. Wanaposema kifungo cha kati ya miaka mitatu hadi 15 hakimu huwa anatumia kigezo gani kukuchagulia miaka ya kifungo? Thamani ya madawa, kujitetea kwa mtuhumiwa, huruma ya hakimu au kígezo gani hasa?

Nimeshashuhudia kesi za aina moja lakini vifungo vikatofautiana...

Ntashukuru kwa kunitoa vumbi kwenye medula yangu.

Kwa mujibu wa kesi za nyuma zilizoamuliwa huko Macau waliokamatwa na kilo moja hadi mbili za dawa za kulevya walifungwa kati ya miaka 8 na 12.

Kwa hiyo, inaonekana kama vile adhabu inategemea na idadi kilo za dawa alizokutwa nazo mtuhumiwa. Pia nadhani aina ya dawa ina-matter pia maana kuna dawa nyingine zina madhara makubwa zaidi kulinganisha na nyingine.

Miaka ya nyuma waliokuwa wanakamatwa na dawa za kulevya huko Macau walikuwa ni Wafilipo. Walikuwa wanaenda China kwa gia ya kwenda kufanya kazi huko.

Kuona hivyo, Macau waaliamua ku-tight viza kwa Wafilipo na tokea wakati huo hali imekuwa nzuri kidogo. Hata hivyo, hivi karibuni kumekuwa na punda wapya kutokea nchi za Kiafrika.

Katika kuwahoji hao punda, wengi wao walisema waliamua kuwa punda kutokana na matatizo ya kifedha au kuwa na madeni.

Pia Macau walikuta kuwa "punda" wengine walikuwa HIV positive na kwamba hali hiyo ndiyo iliyokuwa inawafanya wa-take risk ya kuwa punda ili kutengeneza pesa kifastjet maana liwalo na liwe tayari limeshakuwa anyway.

Hii inaweza kuwa interesting kwa baadhi watafiti kutaka kujua kama kuna uhusiano wowote kati ya HIV na uamuzi wa mtu kuwa punda.
 
Weeee vipi umerogwa nini,sasa sitini unaona sawa na wiki.babu seya hata kumi hajafika kabaki kichwa tuh
Kama nimemwelewa mtoa mada suala hapo ni kwamba kuna faini....ukilipa faini maaana yake hufungwi.
 
Najiuliza huu mzigo aliubebea dar???if so Dakitari Mwaki-embe juhud zake zinazaa matunda?
 
Kwa mujibu wa kesi za nyuma zilizoamuliwa huko Macau waliokamatwa na kilo moja hadi mbili za dawa za kulevya walifungwa kati ya miaka 8 na 12.

Kwa hiyo, inaonekana kama vile adhabu inategemea na idadi kilo za dawa alizokutwa nazo mtuhumiwa. Pia nadhani aina ya dawa ina-matter pia maana kuna dawa nyingine zina madhara makubwa zaidi kulinganisha na nyingine.

Miaka ya nyuma waliokuwa wanakamatwa na dawa za kulevya huko Macau walikuwa ni Wafilipo. Walikuwa wanaenda China kwa gia ya kwenda kufanya kazi huko.

Kuona hivyo, Macau waaliamua ku-tight viza kwa Wafilipo na tokea wakati huo hali imekuwa nzuri kidogo. Hata hivyo, hivi karibuni kumekuwa na punda wapya kutokea nchi za Kiafrika.

Katika kuwahoji hao punda, wengi wao walisema waliamua kuwa punda kutokana na matatizo ya kifedha au kuwa na madeni.

Pia Macau walikuta kuwa "punda" wengine walikuwa HIV positive na kwamba hali hiyo ndiyo iliyokuwa inawafanya wa-take risk ya kuwa punda ili kutengeneza pesa kifastjet maana liwalo na liwe tayari limeshakuwa anyway.

Hii inaweza kuwa interesting kwa baadhi watafiti kutaka kujua kama kuna uhusiano wowote kati ya HIV na uamuzi wa mtu kuwa punda.

very interesting,,,shukran jazzira
 
Mkuu umetumia Gobore kuua mbu, kabla hujaja na ushauri wa juu ya kufuta vumbi kwenye ubongo wangu nadhani uanze na wa kwako.. nini maana ya Tetesi? Hizi ni tetesi tuu

Tanzania ukishikwa na madawa ya kulevya kwanza hatuna mdhamana na adhabu ya kifungo cha maisha itakuhusu. Nitashangaa sana kama Macau watakuwa na adhabu ya kizembe hivyo.

Nitapitia hiyo makala lakini nitafanya general overview sio kutumia muda wangu kutaka kujua sana kusiko kuwa na msingi.

weweee,Tanzania hiyo adhabu una uhakika watu wanaipata???,maana juzi tu watuhumiwa wa dawa za kulevya mtu na mumewe wamepewa dhamana
 
Mkuu umetumia Gobore kuua mbu, kabla hujaja na ushauri wa juu ya kufuta vumbi kwenye ubongo wangu nadhani uanze na wa kwako.. nini maana ya Tetesi? Hizi ni tetesi tuu

Unaruka hata ulichoandika? Umeandika kuwa na nakunukuu "Macau alipokamatwa Jack Cliff hawana adhabu ya kifo ila kwa kuwa imethibitika atafungwa jela kwa muda wa miaka 60 AU faini (not mentioned)..."

Hata hivyo kama ilikuwa ni tetesi, tokea lini sheria ikawa ni tetesi? Kwa nini usiitafute hiyo sheria na kuisoma ili kujua adhabu yenyewe?

Tanzania ukishikwa na madawa ya kulevya kwanza hatuna mdhamana..."

Mbona kwenye ile kesi ya Fred William Chonde na wenzake ambao walikutwa na kilo 179 za Heroine yenye thamani ya shilingi Bilioni 6.5. walipewa dhamana?

na adhabu ya kifungo cha maisha itakuhusu.

Unaweza kutuwekea hiyo sheria hapa? Ilipitishwa mwaka gani? Nilimsikia Lukuvi akiikandia sheria ya sasa akisema kuwa "adhabu iliyopo ni faini ya Sh. milioni 10 au kifungo cha maisha jela, huku ikimpa uhuru jaji au hakimu kutoa uamuzi wa kifungo au kumtoza faini mtuhumiwa kadri anavyoona inafaa." Home.

Nitashangaa sana kama Macau watakuwa na adhabu ya kizembe hivyo.

Kati ya nchi yako na Macau ipi yenye sheria ya kizembe?

Nitapitia hiyo makala lakini nitafanya general overview sio kutumia muda wangu kutaka kujua sana kusiko kuwa na msingi.

Kama suala siyo la msingi, then usingepoteza muda wako kuanzisha huu uzi. You should have other important things to spend your time on them.
 
Unaruka hata ulichoandika? Umeandika kuwa na nakunukuu "Macau alipokamatwa Jack Cliff hawana adhabu ya kifo ila kwa kuwa imethibitika atafungwa jela kwa muda wa miaka 60 AU faini (not mentioned)..."



Mbona kwenye ile kesi ya Fred William Chonde na wenzake ambao walikutwa na kilo 179 za Heroine yenye thamani ya shilingi Bilioni 6.5. walipewa dhamana?



Unaweza kutuwekea hiyo sheria hapa? Ilipitishwa mwaka gani? Nilimsikia Lukuvi akiikandia sheria ya sasa akisema kuwa "adhabu iliyopo ni faini ya Sh. milioni 10 au kifungo cha maisha jela, huku ikimpa uhuru jaji au hakimu kutoa uamuzi wa kifungo au kumtoza faini mtuhumiwa kadri anavyoona inafaa." Home.



Kati ya nchi yako na Macau ipi yenye sheria ya kizembe?



Kama suala siyo la msingi, then usingepoteza muda wako kuanzisha huu uzi. You should have other important things to spend your time on them.

mkuu huu uzi nimeuanzisha sio kwa mashindano kama ambavyo wewe unataka. sheria zetu sio za kizembe bali watu ndiyo wazembe, ukweli ni kwamba watu wanaojihisisha na biashara hii wana nguvu sana.

Kama unaona una wazo au maoni tofauti unatoa pasipo kutaka kufananisha na ambacho mtu anaandika tena kwa ku-criticize

Sawa nimekuelewa! Tusubiri tuone hii filamu ya Jack Cliff
 
mkuu huu uzi nimeuanzisha sio kwa mashindano kama ambavyo wewe unataka.

Nishindane na wewe kwani kuna nini cha kushindania hapa? Ukishinda utalipwa nini?

Kabla ya kuanzisha hoja, get your facts right.

Otherwise, habari itakuwa ni ya kiudaku na kuna jukwaa mahususi kwa ajili ya habari kama hizo.
 
Naomba msaada kidogo. Wanaposema kifungo cha kati ya miaka mitatu hadi 15 hakimu huwa anatumia kigezo gani kukuchagulia miaka ya kifungo? Thamani ya madawa, kujitetea kwa mtuhumiwa, huruma ya hakimu au kígezo gani hasa?

Nimeshashuhudia kesi za aina moja lakini vifungo vikatofautiana...

Ntashukuru kwa kunitoa vumbi kwenye medula yangu.

Kwa uzoefu wangu mimi, kama adhabu inatoa range ya muda kama inavyosemwa hiyo ya Macau, Jaji au Hakimu anaweza kuangalia mambo kama; hiyo ni mara yako ya ngapi wewe kukamatwa kwa kosa hilo, kukiri kwako kutenda kosa na kuonyesha majuto ya kosa lako na kuomba msamaha, kutaja wahusika - waliokutuma na unaowapelekea, afya ya akili yako, na kadhalika.

Kwa hiyo, kama utapewa fursa ya kujitetea na kuwasilisha mitigating circumstances/ factors, unaweza kutaja mambo kama hayo kwa matumaini ya kwamba bwana au bibi jaji au hakimu atakuhurumia na hivyo kupunguza ukali wa adhabu dhidi yako.

Hivyo ndivyo nidhaniavyo mimi. But what do I know.....mi mbeba mabox tu.
EMT atanisahihisha kama nimekosea.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
Back
Top Bottom