Jack Cliff hatanyongwa wala kufungwa

Jack Cliff hatanyongwa wala kufungwa

Macau alipokamatwa Jack Cliff hawana adhabu ya kifo ila kwa kuwa imethibitika atafungwa jela kwa muda wa miaka 60 AU faini (not mentioned) hivyo tutegemee Lady Boss kurudi mtaani..

Boss Lady ndio nani?
 
Weeeeeee mtoto mzr hvyo anyongwe? Subr uone sinema mkuu! Naunga mkono hoja

Kweli kabisa.. tusubiri hii sinema, tatizo episode 2 inaweza isitoke kama ile ya Kapuya.
 
Jela miaka 60!!
Na miaka 28 aliyonayo atatoka akiwa na umri wa miaka 88.
 
Aheri mademu wa shule ya msingi wao wanataka ubuyu tu
 
Nifahamisheni jamani, huyu Jack ni yule super model aliyecheza video ya 'She got a gwan' ya marehemu Albert Mangwea?
 
Ndo huyo huyo

Lakini picha za mitandaoni zinaonyesha Demu aliyefunikwa sura, sasa hii kwamba ni Jack huyu sijui watu wamekisia au,
lakini kama si kweli ni yeye binafsi kama Jack uko mjink hapa ningependa ujitokeze!
 
Lakini picha za mitandaoni zinaonyesha Demu aliyefunikwa sura, sasa hii kwamba ni Jack huyu sijui watu wamekisia au,
lakini kama si kweli ni yeye binafsi kama Jack uko mjink hapa ningependa ujitokeze!

Mkuu husomi alama za nyakati tuu, msichana huyo hajaonekana instagram week na masiku ilhali allikuwa kila siku anatupia picha. Ndugu mmoja/mtu wa karibu amethibitisha ni yeye na sauti ipo mtandaoni. Angekuwa sio yeye angeshajitokeza.. Chief Rocka amethibitisha ni yeye.
 
Sheria ifuate mkondo wake mtu anaendesha ben z lake ukweli ni kuwa hadi drug lod anakamatwa wapo wengi wanaotAABIKA KWA AJILI YA HUYU DADA
 
Macau alipokamatwa Jack Cliff hawana adhabu ya kifo ila kwa kuwa imethibitika atafungwa jela kwa muda wa miaka 60 AU faini (not mentioned) hivyo tutegemee Lady Boss kurudi mtaani..

Tupatie hiyo sheria inayosema kuwa atafungwa miaka 60 au kulipa faini ambayo hajulikani. Ni ajabu sheria kusema kuwa aliyekutwa na hatia atalipa faini bila kusema atalipa faini ya kiasi au hata kuweka kiwango cha juu au chini.

Kwa mujibu wa sheria Namba 17/2009 ya Macau, "punda" anayekutwa na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya nchini humo anatumikia kifungo cha miaka kati ya 3 na 15.

Wadau wa huko wanadai kuwa sheria siyo kali na wanapendekeza adhabu iongezwe maana sheria ya sasa imeifanya Macau kutumia kama "portal" ya dawa za kulevya za kulevya.

Ushauri wa bure na kwa faida yako: tafuta dissertation iliyoandikwa na Ho We Chong kama sehemu ya shahada yake ya uzamili Juni 2013 kwenye Chuo Kikuu cha Macau yenye kichwa cha habari: "A comparative study of punishment for drug trafficking crime in Greater China: With a historical overview and the current practices."

Then, soma zile sections zinazozungumzia sheria za Macau. Natumaini baada ya hapo utakuwa umepangusa vumbi kwenye ubongo wako.

Pia itakusaidia kutorukia na kuandika mambo ambayo hata huyajui. I doubt kama unajua adhabu ya kosa hilo kwa mujibu wa sheria za nchi yako.
 
Tupatie hiyo sheria inayosema kuwa atafungwa miaka 60 au kulipa faini. Ni ajabu sheria kusema kuwa aliyekutwa na hatia atalipa faini bila kusema atalipa faini ya kiasi au hata kuweka kiwango cha juu au chini.

Kwa mujibu wa sheria Numba 17/2009 ya Macau, "punda" anayekutwa na hatia ya kusafirisha dawa za kulevya nchini humo anatumikia kifungo cha miaka kati ya 3 na 15.

Ushauri wa bure na kwa faida yako: tafuta dissertation iliyoandikwa na Ho We Chong kama sehemu ya shahada yake ya uzamili Juni 2013 kwenye Chuo Kikuu cha Macau yenye kichwa cha habari: "A comparative study of punishment for drug trafficking crime in Greater China: With a historical overview and the current practices."

Then, soma zile sections zinazozungumzia sheria za Macau. Natumaini baada ya hapo utakuwa umepangusa vumbi kwenye ubongo wako.

Pia itakusaidia kutorukia na kuandika mambo ambayo hata huyajui. I doubt kama unajua adhabu ya kosa hilo kwa mujibu wa sheria za nchi yako.

Mkuu ahsante kwa elimu.

Naomba msaada kidogo. Wanaposema kifungo cha kati ya miaka mitatu hadi 15 hakimu huwa anatumia kigezo gani kukuchagulia miaka ya kifungo? Thamani ya madawa, kujitetea kwa mtuhumiwa, huruma ya hakimu au kígezo gani hasa?

Nimeshashuhudia kesi za aina moja lakini vifungo vikatofautiana...

Ntashukuru kwa kunitoa vumbi kwenye medula yangu.
 
Fine equivalent na miaka 60 ni nyingi sana!!! Mapede wa sembe bongo lazima wamchangie wamtoe ila navyowajua claus efeme akitoka lazima wamsafishe kwamba alisingiziwa ule sio mzigo wake!!
 
Macau wanahongeka ikiwa vibosile wake waliomtuma kweli watasimama kidete basi tutamuona mitaani baada ya muda si mrefu.
 
Back
Top Bottom