ITV na Channel 10 zaungana na TBC?

ITV na Channel 10 zaungana na TBC?

Exaud Mamuya

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2011
Posts
403
Reaction score
243
Katika hali ambayo imenishangaza ni vituo hivi vya habari yaani ITV na Channel 10 kutoonyesha habari za press iliyoitishwa na Chadema makao makuu kuhusiana na sakata la katibu wa Chadema kanda maalumu ya Dar es salaam bwana Henry Kileo pamoja na makamanda wengine wanaoshikiliwa na polisi kwa wanachodai kummwagia kada wa ccm tindikali. Imenishangaza sana kuona habari hii ikirushwa na kituo cha Star tv peke yake.

Angalizo langu katika vyombo hivi vya habari ni kwamba wajitathmini na kufanya kazi zao kwa uhuru pasipo kukubali mashinikizo ya ccm na vyombo vyake la sivyo tutavisusia kama ilivyo kwa TBC.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mkuu heshima kwako,

Sijawahi kujiuliza sana kuhusu Channel 10, lakini ITV wameanza kunitumbukia nyongo tangu ile siku ya Juni 15, wakati bomu limelipuka Arusha wao hawakuipa hiyo habari kipaumbele. Ilitangazwa kama habari ya katikati (siyo kama breaking news ama taarifa ya kwanza), na alisoma tu Albert Nitwa kwa sentensi moja. Hapakuwa hata na mwandishi wa habari wa ITV kutujuza zaidi, wala hata kuhoji (hata kwa simu tu kama hali haikuruhusu mwandishi kuwepo sehemu ya tukio) kutoka kwa mashuhuda kama hawakuweza kumpata kiongozi yeyote kwa wakati ule. Ikumbukwe wakati huo walikuwepo waandishi wa habari kadhaa wakifuatilia kampeni za uchaguzi pamoja na kina Asraji Mvungi ambao ni watangazaji wa ITV walioko Arusha.

Labda wanaogopa kutia kitumbua mchanga...
 
Mungu endeleakuwapa Mwanga na busara zaidi STAR TV.....Mungu anajua wapi awaanike wanafiki ..Kwani STAR TV iko kiataifa zaidi....
 
Katika hali ambayo imenishangaza ni vituo hivi vya habari yaani ITV na Channel 10 kutoonyesha habari za press iliyoitishwa na Chadema makao makuu kuhusiana na sakata la katibu wa Chadema kanda maalumu ya Dar es salaam bwana Henry Kileo pamoja na makamanda wengine wanaoshikiliwa na polisi kwa wanachodai kummwagia kada wa ccm tindikali. Imenishangaza sana kuona habari hii ikirushwa na kituo cha Star tv peke yake.

Angalizo langu katika vyombo hivi vya habari ni kwamba wajitathmini na kufanya kazi zao kwa uhuru pasipo kukubali mashinikizo ya ccm na vyombo vyake la sivyo tutavisusia kama ilivyo kwa TBC.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

mamuya, hiyo press ina faida gani kwa Taifa?.
kila siku kulalamika tu?.
tumeshawachoka na hizo press zao?.
mbona wewe ulipofanya press kuwaunga mkono madiwani waliotimuliwa ulionyeshwa?. shame on you. liar
 
Mkuu heshima kwako,

Sijawahi kujiuliza sana kuhusu Channel 10, lakini ITV wameanza kunitumbukia nyongo tangu ile siku ya Juni 15, wakati bomu limelipuka Arusha wao hawakuipa hiyo habari kipaumbele. Ilitangazwa kama habari ya katikati (siyo kama breaking news ama taarifa ya kwanza), na alisoma tu Albert Nitwa kwa sentensi moja. Hapakuwa hata na mwandishi wa habari wa ITV kutujuza zaidi, wala hata kuhoji (hata kwa simu tu kama hali haikuruhusu mwandishi kuwepo sehemu ya tukio) kutoka kwa mashuhuda kama hawakuweza kumpata kiongozi yeyote kwa wakati ule. Ikumbukwe wakati huo walikuwepo waandishi wa habari kadhaa wakifuatilia kampeni za uchaguzi pamoja na kina Asraji Mvungi ambao ni watangazaji wa ITV walioko Arusha.

Labda wanaogopa kutia kitumbua mchanga...
pelekeni CHADEMA TV iripoti.
 
Mimi mwenyewe nimeshuhudia hicho unachokisema.
ITV ni kituo kinachofanya kazi kwa woga sana, Nahisi habari zao mara kadhaa serikali na makada wa CCM wanazi-screen kwanza.

Ni muhimu CHADEMA kuwa na Media zake kuliko kutegemea hizi za wajanjawajanja.
 
Chadema anzisheni TV yenu lasivyo mtalalamikia kila mtu,pia mmezidi sana Matamko kuwe na Utaratibu wa kutoa matamko!
 
Kwani ni lazima ionyeshwe?kama kuna habari za muhimu kuliko hiyo?
Alafu watu wanapokukataa usiishie kuwalaumu bali jitafakari mwenyewe kwanini watu hawakutilii maanani?
msitake kilamfanyalo lisemwe na kila chombo cha habari,kwni mnahisa?
 
nadhani ni vizuri chama kikawa na tv yake na hili tumezungumza saana hizi tv stations zote zimejaa magamba na wengine akina mr machache hawalipi kodi ndio maana wakitingishwa kidogo wananyweaa.
 
Kwani ni lazima ionyeshwe?kama kuna habari za muhimu kuliko hiyo?
Alafu watu wanapokukataa usiishie kuwalaumu bali jitafakari mwenyewe kwanini watu hawakutilii maanani?
msitake kilamfanyalo lisemwe na kila chombo cha habari,kwni mnahisa?

Chadema akili zao fupi sana wanajua kila TV ipo responsible kurusha matamko yao! Utasikia tutahamasisha wananchi wasusie kuangalia TBC,ITV na Channel Ten! Matamko kila siku!
 
mi naona bora pia ianzishwe JF TV,itatuhabarisha vizuri sana,ujue mm wala huwa siangalii hyo miTV yenu,habari nyingi current huwa nazipakuwa huku JF
 
Mtalaumu kila kituu kama magamba walivyo

"To know the enemy is half the victory"
 
Mkuu heshima kwako,

Sijawahi kujiuliza sana kuhusu Channel 10, lakini ITV wameanza kunitumbukia nyongo tangu ile siku ya Juni 15, wakati bomu limelipuka Arusha wao hawakuipa hiyo habari kipaumbele. Ilitangazwa kama habari ya katikati (siyo kama breaking news ama taarifa ya kwanza), na alisoma tu Albert Nitwa kwa sentensi moja. Hapakuwa hata na mwandishi wa habari wa ITV kutujuza zaidi, wala hata kuhoji (hata kwa simu tu kama hali haikuruhusu mwandishi kuwepo sehemu ya tukio) kutoka kwa mashuhuda kama hawakuweza kumpata kiongozi yeyote kwa wakati ule. Ikumbukwe wakati huo walikuwepo waandishi wa habari kadhaa wakifuatilia kampeni za uchaguzi pamoja na kina Asraji Mvungi ambao ni watangazaji wa ITV walioko Arusha.

Labda wanaogopa kutia kitumbua mchanga...
Dah, ukiona chama kinakimbiwa na vyombo vingi vya habari basi ujue kuwa mwisho wao umekaribia. Nawashauri chadema waanzishe vituo vya kwao vya tv na si kuishia kwenye youtube tu
 
Hivi mlikuwa hamjui kuwa kituo bora ni star tv pekee hapa tz!ndiyo maana huwa naangalia mieleka tu kupitia etv na picha za nigeria tu basi
 
Dah, ukiona chama kinakimbiwa na vyombo vingi vya habari basi ujue kuwa mwisho wao umekaribia. Nawashauri chadema waanzishe vituo vya kwao vya tv na si kuishia kwenye youtube tu
Enzi zenu hata akina chiluba zambia walikuwa wanatamba baada ya kuondoka wakalisoma jiji,inajulikana vyombo vyote munavidhibiti lakini ndio kama hivyo mitandao ipo na watu wanajua kwamba munaendekeza propaganda kaka yana mwisho tamba leo kesho majuto
 
Back
Top Bottom