ITV na Channel 10 zaungana na TBC?

ITV na Channel 10 zaungana na TBC?

Mengi naye ashamalizwa hamna kitu lazima ITV iongelee habari za magamba tu
 
kesho nayo mtaiona haina maana.

umesahau StarTV inamilikwa na kada na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza??? chadema waache kulia lia, wafungue station zao ili wapige propaganda huko
 
Magamba siasa hawawezi ndo maana sasahv hata kwa waganga wa kienyeji wanaenda kama chama ilimradi wajinusuru na hili janga.Mfunge Mbowe,Slaa n.k,nunua media zote lkn chadema ni mioyo ya watz sio miili.
 
umesahau StarTV inamilikwa na kada na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza??? chadema waache kulia lia, wafungue station zao ili wapige propaganda huko
Dah ila kaka yangu Revocatus kutumika kwa jinsi yako ni kubaya sana.unaokoelekea utakuwa kama Mwampamba aliyeacha ualimu akaenda kubeba na kula makombo ya Savimbi.
 
Kwani kuna ulazima gani kutangaza habari za chama cha kigaidi? Yaani mpange kuua wahariri wao kisha wawatangaze unadhani wao ni ndondocha wasiojua walifanyalo
 
nimewahi ona hm hata kwenye majukwa cdm wakiisia itv na kuita ni tv ya taifa,,,,cdm wajinga sana akili ndogo kuongoza akili kubwa hkn tv itakayoendelea tangaza ujinga na ugaidi wenu

JF tv itatangaza ugaidi??,we kweli umebemendwa,eti akili ndogo za CDM ziongoze akili kubwa,CCM ndio akili kubwa eeeh??,umevurugwa kweli wewe,upo timamu wewe??,acha kunywa maji ya bendera mkuu,mtoto mdogo unazeeka kisa kushabikia chama kinachozidi kututia umasikini watz,funguka wewe,fikiria na nje ya box achakuwa na mawazo mgando!!
 
Katika hali ambayo imenishangaza ni vituo hivi vya habari yaani ITV na Channel 10 kutoonyesha habari za press iliyoitishwa na Chadema makao makuu kuhusiana na sakata la katibu wa Chadema kanda maalumu ya Dar es salaam bwana Henry Kileo pamoja na makamanda wengine wanaoshikiliwa na polisi kwa wanachodai kummwagia kada wa ccm tindikali. Imenishangaza sana kuona habari hii ikirushwa na kituo cha Star tv peke yake.

Angalizo langu katika vyombo hivi vya habari ni kwamba wajitathmini na kufanya kazi zao kwa uhuru pasipo kukubali mashinikizo ya ccm na vyombo vyake la sivyo tutavisusia kama ilivyo kwa TBC.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
hivi kila utumbo utakaongelewa na kiongozi yeyote wa chadema lazima itangazwe?mbona unataka kuwa dikteta acha kutazama sisi hatutasusia
 
Mkuu heshima kwako,

Sijawahi kujiuliza sana kuhusu Channel 10, lakini ITV wameanza kunitumbukia nyongo tangu ile siku ya Juni 15, wakati bomu limelipuka Arusha wao hawakuipa hiyo habari kipaumbele. Ilitangazwa kama habari ya katikati (siyo kama breaking news ama taarifa ya kwanza), na alisoma tu Albert Nitwa kwa sentensi moja. Hapakuwa hata na mwandishi wa habari wa ITV kutujuza zaidi, wala hata kuhoji (hata kwa simu tu kama hali haikuruhusu mwandishi kuwepo sehemu ya tukio) kutoka kwa mashuhuda kama hawakuweza kumpata kiongozi yeyote kwa wakati ule. Ikumbukwe wakati huo walikuwepo waandishi wa habari kadhaa wakifuatilia kampeni za uchaguzi pamoja na kina Asraji Mvungi ambao ni watangazaji wa ITV walioko Arusha.

Labda wanaogopa kutia kitumbua mchanga...

"Waandishi wa habari watakaowaandika vibaya viongozi ( hapa nadhani hata watakao ripoti habari za mbinu mbaya za CCM) watakufa" mwisho wa kunukuu- Mh. Mulongo Mkuu wa Mkoa wa Arusha!
 
Katika hali ambayo imenishangaza ni vituo hivi vya habari yaani ITV na Channel 10 kutoonyesha habari za press iliyoitishwa na Chadema makao makuu kuhusiana na sakata la katibu wa Chadema kanda maalumu ya Dar es salaam bwana Henry Kileo pamoja na makamanda wengine wanaoshikiliwa na polisi kwa wanachodai kummwagia kada wa ccm tindikali. Imenishangaza sana kuona habari hii ikirushwa na kituo cha Star tv peke yake.

Angalizo langu katika vyombo hivi vya habari ni kwamba wajitathmini na kufanya kazi zao kwa uhuru pasipo kukubali mashinikizo ya ccm na vyombo vyake la sivyo tutavisusia kama ilivyo kwa TBC.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

ITV haina tofauti na TBC siku hizi. Kama Star TV ni ya kada wa CCM lakini wanakuwa objective, je ITV mnajikomba nini?
 
Wapenda coverage, watu wameshachoka hamuishi malalamiko, mlitaka iyo press conference irushwe live who r u? Mtalipia? Wapenda attention wakubwa na mkome kujilipua arusha tena kajilipueni kwenye familia zenu ndan muone kama ni raha kumwaga damu
 
Wazee wa nitoke vipi hawaishiwi yaani kumbe tukio walilitengeneza ili liwe break news ITV, taratibu tu chuya na mchele zitapembuliwa.
 
Mkuu heshima kwako,

Sijawahi kujiuliza sana kuhusu Channel 10, lakini ITV wameanza kunitumbukia nyongo tangu ile siku ya Juni 15, wakati bomu limelipuka Arusha wao hawakuipa hiyo habari kipaumbele. Ilitangazwa kama habari ya katikati (siyo kama breaking news ama taarifa ya kwanza), na alisoma tu Albert Nitwa kwa sentensi moja. Hapakuwa hata na mwandishi wa habari wa ITV kutujuza zaidi, wala hata kuhoji (hata kwa simu tu kama hali haikuruhusu mwandishi kuwepo sehemu ya tukio) kutoka kwa mashuhuda kama hawakuweza kumpata kiongozi yeyote kwa wakati ule. Ikumbukwe wakati huo walikuwepo waandishi wa habari kadhaa wakifuatilia kampeni za uchaguzi pamoja na kina Asraji Mvungi ambao ni watangazaji wa ITV walioko Arusha.

Labda wanaogopa kutia kitumbua mchanga...
..ukiona hivi wanjua mengi zaidi so wanogopa...
 
nimewahi ona hm hata kwenye majukwa cdm wakiisia itv na kuita ni tv ya taifa,,,,cdm wajinga sana akili ndogo kuongoza akili kubwa hkn tv itakayoendelea tangaza ujinga na ugaidi wenu

nyie ndo wale wale WEZI wa nchi hii,hamuwezi kutuelewa tunachokitaka watz kwa sababu mnafaidika na huo WIZI wenu n hamuwezi kukemea,ila ipo siku mtasanda na kuikimbia nchi hii na mtaelewa tunachokiongea,mtazijutia hizo posho zenu za buku saba za Lumumba,njaa kali halafu mnatetea upuuzi wakati ndugu zenu wanakula msoto
 
Wabongo tunajua sana kubwabwaja tuuuu
MIMI SIAMINI KWELI CHAMA PINZANI KIPO TANZANIA DHIDI YA CCM!! CHADEMA BADO SAANAAAAAAA
 
ila tusishangae sana, hata kipindi cha mkoloni vyombo vya habari vilikuwa ni kwa ajili ya kusifia yote waliyokuwa wakifanya watawala, yawe mabaya/mazuri all mean the same!
 
Back
Top Bottom