ITV mmewakosea sana watanzania

ITV mmewakosea sana watanzania

Azam TV ndo Chanel ilobakia! Hawa wanaotegemea mikopo ya serkali na biashara haramu lazima wamtumikie bwana wao
 
mbona mm nimeona kwenye tv ya ccm star tv?labda ITV ilichelewa kufika msilaumu coz hamjui nn kilitokea?
 
Acheni lawama nyie Vyombo vya habari vimewabeba sana hususani ITV mmeishia kuwaletea matatizo hambebeki hawawezi kuacha habari muhimu za kijamii kwasababu ya Lema mbona kuna wakati hata za viongozi kitaifa huwa hazioneshwi jambo gani Lema la maendeleo aliongelea Lema watu wamechoka kasikia mivutano isio na tija upinzani jifunzeni kuongea mahitaji ya muhimu kwa mtanzania mbona hamjifunzi mkataba kushangiliwa upuuzi tu mnataka kujionesha mnaweza kushindana na serikali
 
Haya ni maamuzi. Subiri Tanzania Daima wasipomuweka front page ndo uone hawajatenda haki.
 
Mkuu Lema alivyopata dhamana habari yake iliwekwa ya kwanza kabisa mbele hata ya habari ya ziara ya Magufuli Mtwara. Jana Lema kafanya mkutano na wananchi wake wa Arusha mnataka iwe habari ya kitaifa pia? Hivi wabunge wangapi wanafanya mikutano huko majimboni kwao na hatuwaoni wakirushwa?

Tuache kuwa biased..
Tukubaliane kutokukubaliana. Simulizi ya waziri kivuli wa mambo ya ndani, aliyekuwa mahabusu kwa zaidi ya miezi minne kwangu haiwezi kukosa kuwa habari ya kitaifa, hata kidogo! Lakini ukisoma headline ya Nipashe ya leo kuhusu habari hiyo kwa watu wenye pua zenye uwezo mkubwa wa kunusa, wanaweza kunusa harufu fulani. Kwakuwa Nipashe na ITV ni dugu moja hebu tuendelee kufuatilia...
 
Ni Mwendo wa kuliridhisha tabaka tawala kama Wanafasihi tunavyojadili katika uhuru wa waandishi....

Wakubwa wanapenda kuona mambo yanayowafurahisha.
 
ITV siyo source tena ya habari. Halafu eti wanatangaza namna kudownload lTV kwenye smartphone yako! What a joke. Siku hizi naweza kumaliza hata mwezi bila kuangalia habari kwenye hii TV. Kuna nini kitakachokuwepo kwenye habari za mwanzo kabisa zaidi ya 'Rais amekwenda ......, Mkuu wa mkoa amesema ....., Mkuu wa Wilaya amewahimiza ......., n.k. Yaani shughuli za kwaida kabisa za watendaji wa serikali ndiyo zimegeuzwa kuwa 'NEWS!'.
 
.

Mkutano wa Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema (Mb) ambaye pia ni Waziri kivuli wa mambo ya ndani, habari yake sio tu kwamba haijapewa kipaumbele, Bali haijaoneshwa kabisa katika kituo cha televisheni cha ITV.Kuna taarifa kwamba kituo hicho na vingine vilionywa kutorusha taarifa hiyo.

Kituo cha televisheni cha ITV kimeonesha mapungufu makubwa mno kupata kutokea nchini Kwa Kutokuonesha habari ya Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani, ambaye alikuwa Magereza Kwa zaidi ya miezi minne kwasababu ya kesi za kisiasa.

ITV mmeitia doa tasnia ya habari, mmeonesha mapungufu makubwa katika kuiishi demokrasia ambayo watanzania wanaipigania, na mmesahau kwamba vyombo vya habari ni wadau wakubwa wa demokrasia kwani bila demokrasia hata uwepo wenu kama wanahabari utakuwa mashakani.

Watanzania hawajawahi kukata tamaa, jua liwake, mvua inyeshe, mabadiliko ya kisiasa tutayafikia lazima, ambayo ndiyo msingi wa maendeleo yote.

Hivi we mwana habari huru. Naomba kukuuliza. Wewe ni Mkurugenzi. Mhariri au nani hasa kwa ITV. Huoni unavuka mipaka. Je habari ya Lema unadhani ni muhimu kwa kila mtu. Au ulitaka kumwona wema. Embu kuweni makini na biashara za watu. Maswali mnatunga wenyewe na majibu mnajipa wenyewe. Tena unaanza na majibu afu unaweka maswali. Kwanini usilalamike watu hawapati elimu ya kilimo bora,afya bora na elimu bora itakayowafanya watu kama wewe mkaelimika kuliko kusoma tu. Anzisha Media yako utoe pumba zako. Taifa halika kazi ni siasa tu. Nani ssa ataingia kazini. Gharama ya upumbavu ya watu kama nyinyi inawagharimu sana vijana wanaowategemea. Nani jana alikuamulia nyumbani ule nini. Elimu kama unayo haijakusaidia. By the way i am neither a party member nor ITV employee Ni mtu huru tu nayeona mob inazidi kuharibu nchi hii kwa kudhani insta na JF itaongoza nchi. Watu busy wapo wanachakarika. Eti Mandela wa Tanzania. Ndo hapo najiuliza ndo habari ulitaka watangaze.
 
Huko tuendako watu watutumia zaidi mitandao ya kijamii kupashana habari kuliko vyombo hivi vya habari ambavyo vinaonekana kutokizi malengo.

Media hizi zitaathirika kama jinsi mashirika ya Posta dunani yalivyoathiriwa na ujio wa simu za mikononi kiasi kwamba utumaji wa barua siku hizi umepungua sana na wamebakiwa na kazi ya kushughulikia barua za kikazi tu(za maofisi,n.k) .

Huko tuendako watu watatumia zaidi clip za mitandaoni na maandishi kupitia mitandao kupashana habari kama ilivyo sasa.
Nina miezi mutano sasa toka niache kuangalia vyombo vya habari Tz..wanafiki Tu.hawana lolote.
 
Wewe waziri kivuli ndiyo nini Kwanza!! Hiyo speech yake ilikuwa ni kujijenga kisiasa tu na ndiyo maana haikurushwa bwana.
 
Energizer yenu-kiroba kimefutwa sijui maandamano yenu itakuwaje. Andaaeni gongo muwe mnakunywa.
 
.

Mkutano wa Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema (Mb) ambaye pia ni Waziri kivuli wa mambo ya ndani, habari yake sio tu kwamba haijapewa kipaumbele, Bali haijaoneshwa kabisa katika kituo cha televisheni cha ITV.Kuna taarifa kwamba kituo hicho na vingine vilionywa kutorusha taarifa hiyo.

Kituo cha televisheni cha ITV kimeonesha mapungufu makubwa mno kupata kutokea nchini Kwa Kutokuonesha habari ya Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani, ambaye alikuwa Magereza Kwa zaidi ya miezi minne kwasababu ya kesi za kisiasa.

ITV mmeitia doa tasnia ya habari, mmeonesha mapungufu makubwa katika kuiishi demokrasia ambayo watanzania wanaipigania, na mmesahau kwamba vyombo vya habari ni wadau wakubwa wa demokrasia kwani bila demokrasia hata uwepo wenu kama wanahabari utakuwa mashakani.

Watanzania hawajawahi kukata tamaa, jua liwake, mvua inyeshe, mabadiliko ya kisiasa tutayafikia lazima, ambayo ndiyo msingi wa maendeleo yote.




Acha blahblah ile ni mali binafsi anahaki kurusha hewani taarifa anazoona za maana kama mkutano wa ccm .
 
Kupumzishwa tu na kuishi kama yupo ahela anajiita Mandela je angepigana Vita kama ya kagera naona tusingekunya kabisa.
 
Back
Top Bottom