ITV mmewakosea sana watanzania

ITV mmewakosea sana watanzania

UKAWA hamna tofauti na mwanamke mlalamishi ambaye nyumba yake imemshinda kwa udhaifu wake mwenyewe kisha anaanza kulaumu ndugu, jamaa na majirani zake. Poor you!
 
ITV huko nyuma walijenga imani kubwa sana kwa RAIA, lakini kwa mwenendo huu mlioonesha karibuni hapa mnatia mashaka sana. Sasa sijui watz tukimbilie wapi.jifunzeni kusimamia mnachoamini!
 
Hivi kwanini vyama vya siasa msianzishe vituo vyenu ili muwe mnarusha matangazo mnayoyapenda nyinyi.

Sizani kama kuna chama kina hisa pale ITV.

Acheni kulialia.

.

Mkutano wa Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema (Mb) ambaye pia ni Waziri kivuli wa mambo ya ndani, habari yake sio tu kwamba haijapewa kipaumbele, Bali haijaoneshwa kabisa katika kituo cha televisheni cha ITV.Kuna taarifa kwamba kituo hicho na vingine vilionywa kutorusha taarifa hiyo.

Kituo cha televisheni cha ITV kimeonesha mapungufu makubwa mno kupata kutokea nchini Kwa Kutokuonesha habari ya Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani, ambaye alikuwa Magereza Kwa zaidi ya miezi minne kwasababu ya kesi za kisiasa.

ITV mmeitia doa tasnia ya habari, mmeonesha mapungufu makubwa katika kuiishi demokrasia ambayo watanzania wanaipigania, na mmesahau kwamba vyombo vya habari ni wadau wakubwa wa demokrasia kwani bila demokrasia hata uwepo wenu kama wanahabari utakuwa mashakani.

Watanzania hawajawahi kukata tamaa, jua liwake, mvua inyeshe, mabadiliko ya kisiasa tutayafikia lazima, ambayo ndiyo msingi wa maendeleo yote.
 
.

Mkutano wa Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema (Mb) ambaye pia ni Waziri kivuli wa mambo ya ndani, habari yake sio tu kwamba haijapewa kipaumbele, Bali haijaoneshwa kabisa katika kituo cha televisheni cha ITV.Kuna taarifa kwamba kituo hicho na vingine vilionywa kutorusha taarifa hiyo.

Kituo cha televisheni cha ITV kimeonesha mapungufu makubwa mno kupata kutokea nchini Kwa Kutokuonesha habari ya Waziri Kivuli wa Mambo ya ndani, ambaye alikuwa Magereza Kwa zaidi ya miezi minne kwasababu ya kesi za kisiasa.

ITV mmeitia doa tasnia ya habari, mmeonesha mapungufu makubwa katika kuiishi demokrasia ambayo watanzania wanaipigania, na mmesahau kwamba vyombo vya habari ni wadau wakubwa wa demokrasia kwani bila demokrasia hata uwepo wenu kama wanahabari utakuwa mashakani.

Watanzania hawajawahi kukata tamaa, jua liwake, mvua inyeshe, mabadiliko ya kisiasa tutayafikia lazima, ambayo ndiyo msingi wa maendeleo yote.
Wapenzi wa chadema bana....Unadhani mkutane wa Lema ni muhimu sana kwa maendeleo yetu?
 
Hamna shida ammeongea na watu wake ,wamemuona,amewasalimia,wameshukuru yupo salama na tayari kuwatumikia.VIVA ARUSHA VIVA LEMA,ALUTA CONTINUA.
 
mengi anaogopa wakimfanya km manji atashindwa kumhudumia mtoto mzuri kylnn
Mengi si wa mchezo mchezo.. Kama watoto wa mjini kama JK & Manji & Rostam and company walimshindwa unafikiri nani anaweza kumsumbua. Mengi is always smart..
 
Wakati mwingine ukikaa kimya inasaidia kuto expose umbumbumbu wako! Hata kama una chuki na Lema ile habari ilikuwa ni muhimu sana kwa taifa!
Mkuu Lema alivyopata dhamana habari yake iliwekwa ya kwanza kabisa mbele hata ya habari ya ziara ya Magufuli Mtwara. Jana Lema kafanya mkutano na wananchi wake wa Arusha mnataka iwe habari ya kitaifa pia? Hivi wabunge wangapi wanafanya mikutano huko majimboni kwao na hatuwaoni wakirushwa?

Tuache kuwa biased..
 
Wanajamvi habari,

Takribani mwaka mmoja na nusu vimepita sasa tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka2015, Tangu kumalizika kwa uchaguzi huu, Mwenendo wa vyombo vingi vya habari inchini niwakutiliwa mashaka,Vyombo vingi vya habari achilia mbali vile vinyemrengo wa chama tawala (TBC,Star TV,Clous Media) vimekumbwa na kigugumizi cha kuripoti habari na matukio mbalimbali ya wapinzani.

Kitendo ambacho kimeifedhesha sana sekta ya habari hapa inchini kiasi cha Waziri wake kuomba vyombo hivi viikosoe Serikali baada ya kuona nyendo zake zinatia shaka!take me ukiangalia taarifa ya hapari kila siku utasikia yafuatayo, Raisi wa Tanzania amesema…….,Waziri mkuu wa Tanzania amesema….., Mkuu wa Mkoa/Wilaya x amesema …! Hatuhitaji kujua wanachofanya kwani ni majukumu yao ya kila siku sawa Mwl kwenda Shuleni kila siku na ndio maana tukazuia Bunge live! We want news not information, Raisi kufanya ziara hilo ni jukumu lake na SI HABARI ila NI TAARIFA TU!

ITV miaka ya nyuma mlijizolea umaarufu mkubwa na mkaitwa “The super Brand station” kwa sababu ya kutopendelea upande wowote(The neutral station), Kwa sasa nawaona na nyinyi mkiweka taaluma zenu pembeni kitu ambacho ni hatari kwenu kama shirika binafsi,(a competitive medial station)

Mfano: Haiwezekani taarifa muhimu kama ya Mbunge wa Arusha Mjini Mh Godbless Lema kuongea na wananchi wake baada ya kukaa miezi minne jela bila kuwa nao hairipotiwi kabisa , Habari inayogonga vichwa vya habari duniani kote wewe huripoti? Eti ni Super Brand ( Asimamaye na aangalie asianguke)

Badala yake eti habari za akina Mzee Waryoba na Polepole waongo wakubwa hawa kuwahi kutokea Tanzania ndio zinaoneshwa, Walisema ukuu wa mkoa/wilaya hauna maana yeyote,wakateuliwa wakakubali tena kwa bashasha, Tena eti wanatuambia mchakato wa katiba utaanza upya ! Uanze upya kwa pesa za nani!?, Wamezoea kula pesa zetu hawa kwa kisingizio cha katiba NO!

ITV jirekebisheni haraka kabla hatujawaharakatia kama TBC, Mkitaka kujifunza nguvu ya wanachi ulizeni TBC pamoja na channel yake kuwa ya bure still watu hawaangalii, Be smarter, Be professional acheni ushabiki hao mnaowashabikia mkikosa wafuasa hata wao hamtawaona, So stand at your line. tunataka “ check and balances of story”



Msemakweli Mpenzi wa Mungu

Mungu ibariki Tanzania na watu wake
 
Lema anamsaidiaje mtu wa Mwanza
huyo mropokaji ana lipi mpaka iwe habari kubwa!!
Hizo kick ziliisha 2015
Kama alitoka Kisongo akitegemea kupata Kick
imekula kwake
 
Hyo habar ina manufaa gani kwa wananchi wa kawaida...?
 
Hivi ukiona hiyo habari ni muhimu kwako unadhani ni kwa kila mtu watu wanao angalia taarifa za kisiasa Tanzania hii ni wachache mno unaweza kudhani kila mtu anamjua Lema kumbe ni wewe tu na wapiga kura wewe na marafiki zako na chama chake uzito wa habari unaangaliwa sana na vyombo vya habari msiwalaumu itv otherwise anzisheni Lema Tv.
 
kwahiyo unataka waandike unayoyapenda wewe? so shameful kwa MTU mwenye akili hawezi kuzungumzia hicho ulichokipresent hapa. uchadema unakutesa.
 
Back
Top Bottom