ITV mmempandisha Daladala Mkurugenzi Wangu

ITV mmempandisha Daladala Mkurugenzi Wangu

JF Member

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2014
Posts
8,201
Reaction score
11,350
Kama tunavyojua jana Makonda alitengua agizo la polisi kuhusu Magari ya tinted.

Gari ya mkurugenzi wangu ina -Tinted na alikuwa anajiandaa kutii agizo la police la kuondoa tinted.
Mkurugenzi wangu huwa anaangalia taarifa ya habari ya ITV peke yake kwa vile anaamini huwa kinatangaza habari za uhakika na kwa kuwa yuko busy pia.
Bahati mbaya jana hakuona hilo agizo la Mkuu wa mkoa hivyo leo ameliacha gari nyumbani ili fundi aje akalitoe tinted.

Alipopanda daladala njiani anashangaa kuona tinted ziko kibao na watu wakaanza kuliongelea hilo agizo alishangaa yeye hakuona kwenye taarifa ya habari.

Sasa hapa ofisini watu wanamwambia wao waliona Chanel ten na wengine TBC wengine Startv n.k.. Bahati nzuri mi binafsi niliona Channel ten.

Kwa niaba ya mkurugenzi wangu nimeona nifikishe ujumbe huu kwa ITV.
 
ina maana mkurugenzi wko hafatilie hata habari kupitia mitandao ya ki jamii

G.O.M.D
 
Huyo mkurugenzi wako mwambie aache ushamba, kwa utanzawazi huu huhitaji hata kuangalia taarifa ya habari kujua dunia na nchi inakwendaje.
Huyo hana sifa za kuwa Mkurugenzi kama anashindwa kupita hata kwenye social networks kabla ya kulala kupata mawili matatu pamoja na kuangalia kama kuna email zozote maana kuna nafasi zingine kila dakika unatakiwa uwe updated na email na vitu vingine haijalishi ni weekends au week days though weekend unafanya japo kwa 5% ya muda wako wa kazi
 
Mie sijaangalia Tv ila nimesikia... na huyo Mkurugenzi hana hata network na wana ndugu wengine wakamrushia breaking news..vinginevyo huyo Mkurugenzi atakuwa ni wa Mgahawa mdogo maana hata ukiwa na duka la viatu ukaajiri vijana wawili wa kuuza duka wewe ni Mkurugezi ukiamua kujiita hivyo na ni rukhsa
 
Wakuu kama nilivyo sema. Ni kweli kwamba mkurugenzi wangu alikuwa yuko busy sana week iliyo pita hadi hapa anamalizia kuandaa taarifa. Hivo yuko busy sana.
Hakuweza hata kupitia mitandao ya kijamii hata sisi tulijua ameshaoa ila kwa kuwa alikuwa busy habari hiyo imempita.
 
Wakuu kama nilivyo sema. Ni kweli kwamba mkurugenzi wangu alikuwa yuko busy sana week iliyo pita hadi hapa anamalizia kuandaa taarifa. Hivo yuko busy sana.
Hakuweza hata kupitia mitandao ya kijamii hata sisi tulijua ameshaoa ila kwa kuwa alikuwa busy habari hiyo imempita.
Dereva wake hakupata taarifa?
Hana watoto vijana wajanja?
Ofisi yenu haina Motor Transport Officer amjulishe dereva?
Office ya Deci hiyo.
 
Mie sijaangalia Tv ila nimesikia... na huyo Mkurugenzi hana hata network na wana ndugu wengine wakamrushia breaking news..vinginevyo huyo Mkurugenzi atakuwa ni wa Mgahawa mdogo maana hata ukiwa na duka la viatu ukaajiri vijana wawili wa kuuza duka wewe ni Mkurugezi ukiamua kujiita hivyo na ni rukhsa
Alikuwa busy sana japo alitenga mda wa kuangalia taarifa ya habari ITV - Update zote ziko kwenye magroup yake hata group la kazini kwetu tulituma ila hakupata mda wa kupitia hizo habari.
 
Dereva wake hakupata taarifa?
Hana watoto vijana wajanja?
Ofisi yenu haina Motor Transport Officer amjulishe dereva?
Office ya Deci hiyo.
Ana drive mwenyewe.. Dereva anaye ila kwa sasa anapenda kudrive mwenyewe akiwa na safari za hapa mjini. Na dereva humtumia tu akiwa anatoka nje ya jiji.
 
Kama tunavyojua jana Makonda alitengua agizo la polisi kuhusu Magari ya tinted.

Gari ya mkurugenzi wangu ina -Tinted na alikuwa anajiandaa kutii agizo la police la kuondoa tinted.
Mkurugenzi wangu huwa anaangalia taarifa ya habari ya ITV peke yake kwa vile anaamini huwa kinatangaza habari za uhakika na kwa kuwa yuko busy pia.
Bahati mbaya jana hakuona hilo agizo la Mkuu wa mkoa hivyo leo ameliacha gari nyumbani ili fundi aje akalitoe tinted.

Alipopanda daladala njiani anashangaa kuona tinted ziko kibao na watu wakaanza kuliongelea hilo agizo alishangaa yeye hakuona kwenye taarifa ya habari.

Sasa hapa ofisini watu wanamwambia wao waliona Chanel ten na wengine TBC wengine Startv n.k.. Bahati nzuri mi binafsi niliona Channel ten.

Kwa niaba ya mkurugenzi wangu nimeona nifikishe ujumbe huu kwa ITV.
Mbona mimi nililiona tangazo humuhumu JF?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom