Wanajamvi, Uzi huu umekaa kisiasa na kwa maana hiyo mwanzilishi wake ni shabiki mkubwa wa Makonda aka DAB.
Anachofanya JF Member ni kuwananga ITV kijanja, kwa maneno mengine anasema "Nyie ITV, mmetii agizo la Jukwaa la Wahariri kususia kutangaza habari za Makonda, ona sasa wananchi wanakosa habari njema kama hii kutokana na msimamo wenu!"
Matukio haya na uzi huu viko coordinated sana. Kuanzia tukio la JPM kumuita DAB amuombe radhi Ruge huko Tanga, DAB kutoa agizo linalopingana na Kampeni ya Jeshi la Polisi na sasa uzi huu unaletwa.Haukuletwa kwa bahati mbaya.
Jambo la kusikitisha ni kwamba upendeleo anaopata DAB kutoka kwa mkuru ni kero na kikwazo kwa watendaji wengine kama jeshi la polisi ambalo kwa nia njema kabisa liliamua kudhibiti uhalifu. Inasikitisha kwamba JPM anajenga mnara Mnara wa Babeli bila kujijua. Fikiria Jeshi ambalo lina wataalamu wamebaini kwamba tinted ni tatizo, halafu anakuja mtu aliyefeli darasa la saba anetengua agizo la kitaalamu kabisa. Kilangila.