ITV angalieni maadili kwenye kipindi cha watoto

MAKULUGA

JF-Expert Member
Jan 21, 2011
7,171
9,390
Vyombo vya habari vina nguvu sana katika jamii. Vinaweza kuelimisha na kupotosha. Kwa msingi huu, vyombo vya habari vinatakiwa kuwa makini pale wanapoelimisha jamii.

Hapa nilipo naangalia kipindi cha watoto cha ITV. Katika eneo la watoto kujifunza mafumbo, kuna mtoto ametoa fumbo "Mama yake anaumwa dawa yake ni karoti"

Watoto wote pale studio wamenyoosha mkono wakimaanisha kuwa wanalijua jibu. Matokeo yake walipoambiwa wajibu, wakatririka mashairi ya wimbo. Jibu lake ni "nipe karoti maharage sijazoea kiokote"

Cha kushangaza, wale watangazaji walicheka, fumbo limepata jibu. Kwa kuwa huwa nawajenga watoto kufuatilia vipindi vya TV nikiwa nyumbani, hii si mara ya kwanza watoto kuibuka na vitu vya hatari wakiwa live.

Kuna wakati wanaimba nyimbo zisizo na chembe ya maadili. Chonde ITV, wekeni utaratibu wa kulinda maadili. Kama hamuwezi ombeni ushauri, la sivyo ondoeni vipindi mubashara.

Leo nimemwambia mwanangu hali ikiendelea hivi hatutaangalia tena hiki kipindi. Hii inanikumbusha sehemu fulani, mbele ya Mkuu wa Wilaya, kwenye sherehe, watoto walikuwa wanaigiza athari za ulevi kwa familia alafu kuna mtoto aliigiza mzazi mlevi 😉 akiporomosha matusi ya uchi.

Watu walipigwa ganzi. Kabla ya kuchukua hatua, mtoto akayapiga mengine makali zaidi, ikabidi MC aweke muziki na igizo likaishia hapo!

Sijui Afisa Elimu walimbebea mbeleko gani DC!
 
Hahahaha hiyo story ya mtoto aliyeigiza kama mlevi imenifurahisha sana,

Nimekumbuka enzi ya primary kwenye kipindi cha michezo tupo nje na mwalimu wetu tunaimba na kucheza mwalimu akasema mwanafunzi mmoja aimbe wimbo wowote ule basi akajitokeza mmoja akaanza kuimba wimbo wa Nyambizi wa Dully Sykes, wanafunzi acha tushangilie, mwalimu kila akinyamazisha yule mwanafunzi ndio mzuka unazidi anashusha tu mistari.... Naikumbuka mpaka leo.
 
Mkuu, watoto wanadaka, mie huwa nasikia wanaimba kiokote, huu wimbo sijui jaimba nani na una ujumbe gani. Wanangu wanaujua, sijui wanejifunza wapi. Kwangu sina nyimbo hizo
 
Mleta mada uko sahihi kabisa.
Ila niseme tu, pamoja na nguvu ya vyombo vya habari, kwangu mimi naona hiyo ni matawi tu. Shina na mizizi ya uharibifu huu wa maadili ni huku majumbani/mitaani kwetu.

Huo wimbo wa kiokote hawakufundishwa hapo studio..na ajabu wametoka maeneo mbalmbali lakini wote wanaujua.
Mfano mwingine aliotoa mdau hapo juu kuhusiana na mtoto aliyeporomosha matusi, huyo mtoto amelitendea haki nano 'IGIZA/IGIZO'. Alichofanya ni kuigiza kamili kama wafanyavyo akina baba nyumbani/mtaani alikotokea.

Hivyo basi, hawa ndugu zetu wa tv hawana tatizo sana ila wawe tu makini maana hiki kizazi ni cha nyoka.
Wazazi tumejishindwa ni lazima watoto nao watushinde kattika malezi.
 
Lakini tafsida aliyoikusudia maua sama,ndiyo hiyo inafanya kazi.

Mtoto yeye anadhani ni karoti ile ya jikoni ndio inaimbwa,kumbe ni ujinga mwingine.
 
Mleta mada uko sahihi kabisa.
Ila niseme tu, pamoja na nguvu ya vyombo vya habari, kwangu mimi naona hiyo ni matawi tu. Shina na mizizi ya uharibifu huu wa maadili ni huku majumbani/mitaani kwetu.

Huo wimbo wa kiokote hawakufundishwa hapo studio..na ajabu wametoka maeneo mbalmbali lakini wote wanaujua.
Mfano mwingine aliotoa mdau hapo juu kuhusiana na mtoto aliyeporomosha matusi, huyo mtoto amelitendea haki nano 'IGIZA/IGIZO'. Alichofanya ni kuigiza kamili kama wafanyavyo akina baba nyumbani/mtaani alikotokea.

Hivyo basi, hawa ndugu zetu wa tv hawana tatizo sana ila wawe tu makini maana hiki kizazi ni cha nyoka.
Wazazi tumejishindwa ni lazima watoto nao watushinde kattika malezi.
Hili sikutaka kuliandika,ukisikiliza utambulisho wa watoto wanaotoaga vibomu hivyo....utajua tofauti kubwa ya makuzi na malezi iliyopo nchini.Wengi. Utasikia nasoma Drs la tatu D ,Tandale au nasoma la Sita E Kawe Ukwamani ,Hawa walioendelea kutoka St ....wao huimba nyimbo za kina Beyonce,!
 
Waendeshaji wa Kipindi washakomaaa hawafai tena wanatakiwa waweke watoto. Sasa umeweka watu ambao wanafurahia watoto wakiimba nyimbo na ngono ngono kitakuwa kipindi cha watoto hicho
 
Hilonalo neno,wale watangazi ni watoto kwa maana ya Sheria😂😂
 
Back
Top Bottom