Bongo Haiwezekani!!!
- Haiwezekani kwa sababu Berlusconi amejiuzulu kwa ajili ya maslahi ya nchi yake, JK akijiuzulu maslahi yake, ya magamba wenzake, waliombeba kufikia hapo alipo pamoja na jamaa na marafiki zake, yatakwenda arijojo.
- Haiwezekani kwa sababu Berlusconi ni tajiri hata kabla ya Uwaziri Mkuu; sina hakika na utajiri wa JK, lakini kama ni tajiri, utajiri wake atakuwa ameupata kwa sababu ya nafasi yake.
- Haiwezekani kwa sababu ingawa Berlusconi ni kiwembe kama Vasco da Gama wetu, lakini yule mzee amebakiwa na angalau akali ya haya, da Gama hana haya hata za kuvalia nguo (the famous suti za kuhongwa - lol).
- Haiwezekani kwa sababu Wataliana sio waoga, Wabongo tuko waoga na tuna heshima na amani ya uoga.
HAIWEZEKANI! HAIWEZEKANI! BONGO HAWEZEKANI!!!!!!!!!!!!!!!!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.