Gang Chomba
JF-Expert Member
- Feb 29, 2008
- 20,301
- 4,681
Alipo ulizwa kuhusu Diego Armando Maradona maarufu kama El Pibe di Oro yaani Golden Boy, Mzee Berlusconi alisema:
Nilitaka saana kumleta Maradona ili aje AC Milan akamilike na hata abebe mataji makubwa na yenye hadhi kwa mchezaji kama yeye.
Nilitaka pia aje na acheze kwenye Timu yenye wachezaji wa hadhi yake huku akilindwa na Nyota kama Costacurta, Baresi, Maldini, na kiungo mkabaji Demetrio Albertini.
Pia nilitaka aje apikiwe magoli na viungo kama Roberto Donadoni, Carlo Ancelotti, na Frank Riijkard. Kule mbele nilitaka ajumuike na Ruud Gullit, Marco Van Basten na Daniele Massaro.
Pia nilitaka kipaji chake kije kinolewe na Mwalimu wa Walimu, nilitaka saana Maradona afundishwe na Arigo Sacchi.
Nilikwenda kupiga hodi Klabuni Napoli na kueleza kuwa ninahitaji huduma ya Nyota wao. Lakini kabla sijajibiwa nilipokea taarifa toka Hospitali nyingi za Mji huo zikieleza kupokea wagonjwa wengi wa mshtuko wa Moyo.
Rafiki yangu na msaidizi wangu Adriano Galiani alinifuata na kunikataza mara moja kuendelea na mpango huo. Nilipomuuliza Galiani kwanini amekuja na hoja hio wakati mwanzo alinipa sapoti kubwa ili kufanikisha mpango huo?!
Galiani aliniambia kuwa Maradona ameshikilia mioyo ya washabiki weengi wa Napoli, na kama tukifanikisha kumng’oa Klabuni hapo basi wapo Watu ambao watakufa na hilo litakuwa laana kubwa maishani mwetu.
Endeleeni kupumzika kwa amani Hayati Silvio Berlusconi na Hayati Diego El 10 Peruso El Diaz Armando Maradona.
Watu wa Soka tutazidi kuwakumbuka kwa mchango wenu.