ISSA Salumu Makale (35) afungwa miaka 30 jela kwa hatia ya kukutwa na vipande 13 vya meno ya tembo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,810
11,978
MENO YA TEMBO YAMPELEKA GEREZANI MIAKA 30.
Na Steven Augustino, Tunduru

Hakimu Mkazi mwandamizi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma Honorus Kando amemhukumu mkazi wa Kijiji Cha Nalasi Bw. ISSA Salumu Makale (35) kutumikia kifungo Cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na vipande 13 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 35.25 vyenye Thamani ya shilinngi za Kitanzania 104,041,350,000 Mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .

Hukumu hiyo imetolewa April 18 mwaka huu baada ya Mahakama kujiridhisha bila kutia shaka yoyote na ushahidi uliotolewa na mashahidi 7 wa upande wa Jamhuri.

Akisoma shauri hilo la uhujumu uchumi namba 30/2022 Mbele ya Hakimu Kando Mwendesha Mashtaka Mkaguzi msaidizi wa Polisi Bw. Ernest Machiya alisema kuwa mtuhumiwa huyo alinashwa na mtego ulio andaliwa na maafisa wanyama pori waliojifanya wanunuzi wa meno hayo Mey 27/2022.

Alisema kwa kufanya hivyo mtuhumiwa huyo alitenda kosa kinyume Cha kifungu namba 86(1) na (2)(c)(1) Cha sheria ya uhifadhi wa wanyama pori namba 5 ya mwaka 2009 ikisomwa pamoja na paragraph ya 14 ya Jedwali la kwanza na kifungu namba 57 (1) na 60 (2) Cha sheria ya uhujumu uchumi na makosa yaliyo angaliwa sura ya 200.
 
kuna kipindi huko nyuma nilisikia kuna container zima limejaa hizo pembe za ndovu sijui huyo jamaa alifungwa miaka mingapi. Ujangiri umerejea tena sasa hivi tembo watahama kujisalimisha kama hapo awali walipohamia Msumbiji
 
Huyu mwamba "plea bargain" haimuhusu!? Kwa maana wahujumu uchumi na mafisadi wao wana upenyo maalum wa kisheria wa ku "negotiate" na kuachiwa tena huru.

Biashara ya vipusa, madawa ya kulevya, silaha za magendo, " human trafficking", na ubadhirifu wa mali za umma hufanywa na mitandao ya watu maarufu. Na ukiona mmoja wao akitiwa hatiani, basi ujue ni kama hadaa tu ya muda ili kupotezea jambo hilo lipite vinywani mwa wakuda.

Baada ya hapo, kila kitu kitakwenda kama kawaida. Jela haiwahusu hawa miamba, bali isipokuwa vibaka na majambazi ambao hawapo katika mitandao iliyokuwa rasmi ya wajanja na watoto wa mjini.
 
Yule Malkia wa Tembo Mchina alikutwa na mzigo wa kutosha mbona hakufungwa??
Jela miezi 5 na mzawa jela miaka 30,hii nchi kama sio royal families, hauna fedha hata mahakimu wanakutolea mfano ili wauze majina yao,ndio maana judiciary imedharaulika na CJ ndio kwanza anaelekea kupata evening tea na no 1,escorted na blue lights!!!
 
Back
Top Bottom