Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,918
Katika miaka hii ya karibuni inaonekana taifa dhalimu la Israel limezidi kiburi chake, linapiga linapotaka bila kumuogopa yeyote na hakuna anayeilaumu kwa matendo yake haya isipokuwa wale wanaopigwa.
Imekuwa ni habari za kawaida kusikia imepiga hapa na pale Syria na hivi karibuni inakwenda mbali mpaka Iran na Lebanon. Kuna siku wamefika mpaka Libya na hata Urusi imewahi kuonja kipigo cha Israel pale ndege yake ya kijeshi ilipotunguliwa na kuuwa askari kadhaa takriban 50.
Kwa upande wa miji ya Palestina ikiwemo Gaza ndio kabisa wanapiga na hata kufanya kama sehemu za kujaribia silaha zake.
Kinachoshangaza ni kuwa hakuna kulaaniwa kwa wazi kutoka kwa jumuiya ya kimataifa na hata ikifanyika basi huwa ni kwa juu juu basi na hakuna natija inayopatikana kabla hawajarudia kupiga pale pale walipopiga mwanzo.
Jambo linalotisha na kusikitisha zaidi ni kuona mataifa ya kiarabu ambayo yana udugu wa karibu zaidi na Palestina pamoja na jeuri hiyo ya Israel yapo yanayorejesha uhusiano na Israel na kupuuza wazi wazi yale yanayotendwa na Israel kwa ndugu zao wakati huo huo wanapofanya makubaliano ya kurejesha uhusiano.
Imekuwa ni habari za kawaida kusikia imepiga hapa na pale Syria na hivi karibuni inakwenda mbali mpaka Iran na Lebanon. Kuna siku wamefika mpaka Libya na hata Urusi imewahi kuonja kipigo cha Israel pale ndege yake ya kijeshi ilipotunguliwa na kuuwa askari kadhaa takriban 50.
Kwa upande wa miji ya Palestina ikiwemo Gaza ndio kabisa wanapiga na hata kufanya kama sehemu za kujaribia silaha zake.
Kinachoshangaza ni kuwa hakuna kulaaniwa kwa wazi kutoka kwa jumuiya ya kimataifa na hata ikifanyika basi huwa ni kwa juu juu basi na hakuna natija inayopatikana kabla hawajarudia kupiga pale pale walipopiga mwanzo.
Jambo linalotisha na kusikitisha zaidi ni kuona mataifa ya kiarabu ambayo yana udugu wa karibu zaidi na Palestina pamoja na jeuri hiyo ya Israel yapo yanayorejesha uhusiano na Israel na kupuuza wazi wazi yale yanayotendwa na Israel kwa ndugu zao wakati huo huo wanapofanya makubaliano ya kurejesha uhusiano.