Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,196
- 10,929
Marekani na Uiengereza pekee ndio wako mguu njiani mguu majanini kuhusu matendo ya Israel katika vita vyake Gaza.
Mwanamfalme wa Uiengereza. William ataka vita visitishwe. Rais Biden amepunguza sana urafiki na Benjamin Netanyahu japo nchi yake imepiga kura ya veta lakini haina imani na Israel.
Mataifa ya Ufaransa, Italy, Spain, China na Urusi yamejitokeza wazi wazi kutaka vita visitishwe na kuundwa kwa taifa la Palestina haraka.
Mchanganyiko wa uungwaji mkono kwa wapalestina kutoka pande zote za mashariki na magharibi ni kutokana na aina ya vita inavyopigana na Hamas. Ni vita ambavyo haviheshimu chochote kati ya kanuni za kimataifa wala ubinadamu.
Wale wenye ubinadamu katika nyoyo zao japokuwa hawawaungi mkono Hamas lakini wameingiwa na huruma kwa wale wanaoumizwa na Israel kwa kiwango ambacho hakina maelezo.
Miongoni mwa vitu ambavyo si vya kawaida kufanywa na majeshi yote yanapopigana na adui zao ni pamoja na kuua kwa makusudi walemavu, wanawake na watoto wao. Mambo mengine ni kubomoa mapipa ya maji na kuzuia chakula kuwafikia watu. Ukatili mwengine ni kufukua makaburi makongwe sana ya miaka mingi na kuondoka na mifupa ikisema inatafuta mateka.
Mengine ni kubomoa hospitali karibu zote kwa kisingizio hicho hicho kwama kuna Hamas wamejificha. Katika hospitali hizo umeme umekuwa ukikatwa hata unaotumika kwenye vyumba vya wagonjwa mahututi na kupelelekea vifo vya wagonjwa hao.
Kitendo cha kikatili cha karibuni kabisa ni kile cha kwanza kuzuia msafara wa vyakula kuwafikia watu wanaokaribia kufa kwa njaa kaskazini ya Gaza na pia kuwashambulia watu waliokuwa wakisubiri kupokea mgao wa chakula maeneo mengine ya Gaza.
Picha ya watoto waliokuwa wakiokota unga uliomwagika ardhini na kujaza mifukoni mwa suruali zao ndiyo imewaliza watu wengi na kuzidi kujitenga na ukatili wa Israel.
Mwanamfalme wa Uiengereza. William ataka vita visitishwe. Rais Biden amepunguza sana urafiki na Benjamin Netanyahu japo nchi yake imepiga kura ya veta lakini haina imani na Israel.
Mataifa ya Ufaransa, Italy, Spain, China na Urusi yamejitokeza wazi wazi kutaka vita visitishwe na kuundwa kwa taifa la Palestina haraka.
Mchanganyiko wa uungwaji mkono kwa wapalestina kutoka pande zote za mashariki na magharibi ni kutokana na aina ya vita inavyopigana na Hamas. Ni vita ambavyo haviheshimu chochote kati ya kanuni za kimataifa wala ubinadamu.
Wale wenye ubinadamu katika nyoyo zao japokuwa hawawaungi mkono Hamas lakini wameingiwa na huruma kwa wale wanaoumizwa na Israel kwa kiwango ambacho hakina maelezo.
Miongoni mwa vitu ambavyo si vya kawaida kufanywa na majeshi yote yanapopigana na adui zao ni pamoja na kuua kwa makusudi walemavu, wanawake na watoto wao. Mambo mengine ni kubomoa mapipa ya maji na kuzuia chakula kuwafikia watu. Ukatili mwengine ni kufukua makaburi makongwe sana ya miaka mingi na kuondoka na mifupa ikisema inatafuta mateka.
Mengine ni kubomoa hospitali karibu zote kwa kisingizio hicho hicho kwama kuna Hamas wamejificha. Katika hospitali hizo umeme umekuwa ukikatwa hata unaotumika kwenye vyumba vya wagonjwa mahututi na kupelelekea vifo vya wagonjwa hao.
Kitendo cha kikatili cha karibuni kabisa ni kile cha kwanza kuzuia msafara wa vyakula kuwafikia watu wanaokaribia kufa kwa njaa kaskazini ya Gaza na pia kuwashambulia watu waliokuwa wakisubiri kupokea mgao wa chakula maeneo mengine ya Gaza.
Picha ya watoto waliokuwa wakiokota unga uliomwagika ardhini na kujaza mifukoni mwa suruali zao ndiyo imewaliza watu wengi na kuzidi kujitenga na ukatili wa Israel.