Mkuu Hekimatele, hoja yangu imetokana na mtazamo wangu kuhusu hizi nchi mbili based on their geographical location, size, population na war strategy. Iran ina ukubwa wa 1,648 km2 na Popn. ya takribani watu Miliono 80. Israel in ukubwa wa 20, 770 km2 na Popn. ya watu milioni 8. Kwa akili ya kawaida nadhani unaweza kuona kwamba, kivita, hizi nchi mbili haziwiani hata kidogo.
Ukiangalia ramani hapo chini, utaona kwamba kutoka Israel mpaka Teheran, kuna umbali wa takriban kilometa 1500. Ili Israel aishambulia Iran na kutoa pigo takatifu, inabidi ndege zake zicross anga ya nchi kama 4, ambazo zote ni za Kiarabu. Sidhani kwamba hili ni jambo rahisi.
Technologically, Israel hana ndege za kivita zinazoweza kwenda km 1500 kupiga target (na kutoa pigotakatifu in order to destroy Iranians Nuclear facilities). Mwenye hizo ndege za ku refill ndege juu kwa juu ni Marekani, na mbaye kwa sasa hivi hayupo tayari kuanzisha vita nyingine ndani ya Ghuba ya Uajemi. Anajitayarisha kuondoka Iraq na Afghanistan.
On June 7th, 1981, Israel destroyed Iraq's Osirak Nuclear Plant, shambulio ambalo liliungwa mkono na Iran, ambaye alikuwa adui mkubwa wa Iraq kipindi hicho. Lakini shambulio hilo ndilo lilomfungua macho Iran. Sasa hivi Iranian Nuclear plants zote zipo Underground and scattered kiasi kwamba ni vigumu kwa Israel, peke yake kushambulia successfully six targets at once. Uncle Sam assistance is necessary, kama ikibidi kufanya hivyo, tena sana tu.
Most likely, shambulio lolote la Israel kwa Iran litazaa vita kati ya hawa wababe wawili. Na hapa tena Uncle Sam lazima aweke kifua. Maana yake ni kwamba, kwenye strategy za kivita, hauwezi kuziweka hizi nchi mbili kwenye ulingo moja. Its unrealistic. Kama Saddam Hussein angekuwa hai angetoa ushuhuda.
Vita vya Iraq/Iran vilichukua miaka karibia 8. Na pamoja na misaada aliyopata Iraq kutoka kwa U.S.A, Britain, Germany na France lakini Iraq alishindwa kuwin ile vita. Ni kama nilivyosema hapo mwanzo, size na population ni moja ya vigezo muhimu kwenye vita (TAFADHALI TUSIANGALIE CONGO).
Kwa sababu ya popn. size ya Iran (WATU MILIONI 80), kupoteza raia million kadha kwenye vita kwao sio big deal. Pengine hata kwa Israel itakuwa sio big deal, hosusani inapokuja kwenye suala la UTAIFA NA KUILINDA NCHI YAO.
Huu ni mtizamo wangu tu. Inawezekana nikawa wrong kwenye assessment zangu. Lakini kila ninapoangalia kasheshe ya Ghuba ya Uajemi, huwa nabaki mdomo wazi.