Mkuu
Janken jr
1. Unasema wayahudi wana IQ kubwa kisa kushinda Nobel?? Hivi Nobel inapima IQ au creativity tu?? Je creativity huwa inapimwa kwa IQ au inatokana na maarifa mbalimbali?? Kwanza hapo umepotosha kidogo Nobel wayahudi walioshinda ni 22% pekee tokea ianzishwe na Race ilioshinda zaidi ni Aryans so kama ni jamii yenye akili zaidi twaweza sema Aryans if at all tutatumia kigezo cha Nobel....
List of Jewish Nobel laureates - Wikipedia
Na kwenye IQ Jews ni 40 kwenye list sio top 3 na hiyo ni utafiti official kabisa wa IQ pitia hapa usome vigezo vilivotumika na sample yao
https://brainstats.com/average-iq-by-country.html
2. Unasema hawapigiki which is very truee lakini swali langu why 1948 na kuendelea??? Kama wayahudi wenyewe ndio hawapigiki bila msaada wa marekani swali langu bado ni kwanini wayahudi walikuwa wanatandikwa kila wakiingia vitani nimeshatoa mifano kwenye Crusades ya 1 na ya pili huko Ufaransa na Spain bado russia polanda na lithuania kote walikuwa wanatandikwa na hata walipoanzisha jeshi kujitetea kama huko poland 1943 huku wakipewa silaha na waingereza bado walichinjwa zaidi ya 80,000 kama kuku sasa kama hawapigiki je hapa waliwezaje kutandikwa?? Tusaidiane hapo
3. Kuhusu kuitwa taifa teule hapo mnapotosha maana Petro alisema wakristo waliomfuata Yesu na sio waliomkataa ndio taifa teule kwa mujibu wa Biblia ya agano jipya ambayo wewe unaimani sasa nauliza kuamini wewe au Petro???
1 Peter 2:7-10
7
Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini,Jiwe walilolikataa waashi,Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
8 Tena,Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha.Kwa maana hujikwaza kwa neno lile, wasiliamini, nao waliwekwa kusudi wapate hayo.
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.Ishini kama Watumishi wa Mungu