Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,195
- 10,929
Nguvu ya mashambulizi ya Israel imeonekana hapo jana na mapema leo, ambapo mashambulizi ya ndege za kivita yameendelea usiku kucha huko Gaza ambako tayari eneo kubwa limekuwa kifusi.
Sambamba na Gaza shambulio jengine limetokea tena leo huko ukingo wa Magharibi ambapo kombora limeua zaidi ya wapalestina 12 pamoja na uharibifu mkubwa wa msikiti na nyumba za jirani
Mashambulio mengine kama hayo yameendelea kule nchini Syria ambako Israel inasema nchi hiyo inaiunga mkono Hamas.
Wanadiplomasia wanaojihusisha na masuala ya Mashariki ya Kati wamesema mashambulizi hayo yanatoa mtihani mkubwa kwa mikataba iliyofanya Israel na mataifa ambayo wanaitetea Palestina,
Marekani nayo imeshusha shehena kubwa ya silaha kwa jeshi la IDF la Israel kutoka ndege za mizigo zisizopungua 45 katika kipindi cha siku 10 huku meli nyingine ya kivita ikiwa iko njiani kuelekea eneo hilo la vita.
Sambamba na Gaza shambulio jengine limetokea tena leo huko ukingo wa Magharibi ambapo kombora limeua zaidi ya wapalestina 12 pamoja na uharibifu mkubwa wa msikiti na nyumba za jirani
Mashambulio mengine kama hayo yameendelea kule nchini Syria ambako Israel inasema nchi hiyo inaiunga mkono Hamas.
Wanadiplomasia wanaojihusisha na masuala ya Mashariki ya Kati wamesema mashambulizi hayo yanatoa mtihani mkubwa kwa mikataba iliyofanya Israel na mataifa ambayo wanaitetea Palestina,
Marekani nayo imeshusha shehena kubwa ya silaha kwa jeshi la IDF la Israel kutoka ndege za mizigo zisizopungua 45 katika kipindi cha siku 10 huku meli nyingine ya kivita ikiwa iko njiani kuelekea eneo hilo la vita.