Siijui fizikia coz mara ya mwisho kuisoma nilikua form 4 ila labla nikuulize we mwanafizikia, kwa nini majengo marefu yanajengwa na steel? Ni saruji au steel kinachosimamisha jengo? Je moto wa kawaida tu ambao ni tofauti na ule wa kuyeyushia chuma unaweza kuporomosha jengo kama hiyo ya 9/11? Mbona kuna majengo mengi yashawaka sana kama lile la kule Spain lilowaka kwa zaidi ya masaa 20 lakini halikuanguka na lilikua strong enough to hold a crane on top of it? Infact hata wakandarasi wa hayo majengo(twin towers) wanasema waliyajenga waki-invision kuwa yanaweza kuhimili ajali ya kugongwa na ndege? Hilo tower 7 ni kweli liliporomoshwa na kifusi? Real? Mbona Meya wa New York aliamuru watu watoke kwenye hilo jengo kwa sababu aliambiwa " they gonna pull it down", je aliota kwamba litaangukiwa na kifusi?
Wakati wanaenda kuipiga Iraq walisema kuna weapons of mass destruction, cjui mwenzetu unaweza kutupa report yoyote inayoweza kuprove kwamba walizikuta hizo W.O.M.D? If not,kwa nini tuamini sana kile wanachosema wao ili hali kinapingana kabisa na reasoning pamoja na laws of physics ambazo wewe unaziadvocate?
Unauliza maswali ya maana. Tangu zaidi ya miaka 100 nyumba ndefu zote za aina skyscraper hutengenezwa kwa kutumia fremu ya feleji. Nguzo na boriti za feleji zinaunganishwa , kwa kawaida kimraba, kutengeneza fremu yenye umbo la jengo linalokusudiwa. Ni fermu ya feleji inayosimamisha jengo ndefu (kama unajenga bila fremu nyumba ndefu inawezekana lakini ghali mno; maana ungehitaji kutumia kuta nenenene mno zinazoweza kubeba uzito wa ghorofa za juu...)
Sakafu kila ghorofa na misingi kwa kawaida ni mchanganyiko wa saruji na feleji maana saruji ya pekee si imara vile inavyotakiwa (imara sana dhidi shindikizo lakini hafifu dhidi nguvu za mvutano; hii sababu hutumiwa pamoja yaani nyavu ya feleji ndani ya ganda za saruji).
Hatari ya moto kwa majengo ya fremu za feleji ni tabia ya chuma kupokea joto haraka (tofauti na jiwe au saruji) na kupanuka. Kama vyuma vya mchanganyiko wa saruji-feleji vinashika joto na kupanuka vinaweza kupasua saruji (sawa na tatizo la kawaida kama unyevu unaweza kuingia ndani ya saruji na kufikia vyuma na kusababisha kutu maana chuma cha kutu kinachukua nafasi kubwa kushinda chuma kitupu, hivyo kuta hizi zinaanza kupasuka).
Tatizo ingine (na WTC tatizo kuu) ni sehemu ambako boriti za feleji zinaunganishwa. Kama boriti moja inashika joto inaanza kupanuka na kupinduka kidogo. Hii inaweza kuvunja (au kusababisha kuachana) bolti, skrubu au rivets zinazoshika maboriti pamoja. Kama boriti muhimu zinaachana hatari ya kuporomoka imeshafika maana makdirio ya uimara inategema fremu yote.
Tatizo la minara za WTC lilikuwa kutokea kwa moto kali ambayo haikukadiriwa wakati wa kupanga na kujenga. Katika minara mirefu ukali wa moto iliyoanzishwa na petroli ya ndege ilisababisha kulainika (si kuyeyuka!) kwa sehemu za boriti na kuachana kwa viungo. Ghorofa za juu zilianza kuteleza na kuongeza mzigo kwa sehemu za chini zisizokadiriwa kwa mzigo huu; mwishowe viungo vilianza kuvunjika.
Katika jengo na. 7 WTC tatizo lilikuwa muda wa moto iliyosababishwa na vipande vva kuwaka kutoka minara mirefu na uhaba wa maji. Hapo walinzi moto walijaribu kwa masaa kupambana na moto ndani ya jengo lakini waliona mabadiliko katika umbo la jengo kutokea polepole na kusikia sauti za feleji wakati viungo vilianza kuachana na kupinda. Hapo walitoka nje kwa sababu walitambua hatari.
Huo mfano wa Hispania sijui labda lete chanzo.
Unaweza kujisomea kuanzia hapa
7 World Trade Center - Wikipedia, the free encyclopedia, akuendelea na taarifa ya mamuhandisi wa ujenzi Marekani hapa
WTC Disaster Study
Ile kuhusu WMD za Iraq sidhani ya kwamba kuna haja la kujadili. Leo hii imekubaliwa hata Markani na wanasiasa ya kwamba dai hili lilikuwa ama uwongo wa kusudi au kosa tu. Hazikupatikana wala hazikuwepo wakati wa vita.