dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 22,121
- 49,371
Wakuu Heshima;
Kuna kitu kinaitwa Benki ya Kiislamu (ISLAMIC BANKING). Tafadhali naomba mwenye habari jinsi hiki chombo kinavyofanya kazi atupashe habari. Ni muda kidogo umepita tangu NBC na KCB (T) Ltd. waanzishe akaunti za kiislamu lakini inawezekana wengi wetu, wakiwepo baadhi ya waislamu, hatuko well informed na hiki kitu.
Leo katika Gazeti la Raia Mwema nimeona tangazo la BoT - ISLAMIC BANKING TRAINING PROGRAM ambapo BoT kwa kushirikiana na taasisi moja ya ushauri kutoka Jordan itaendesha mafunzo juu ya Benki ya Kiislamu. Nimewahi pia kusikia kutoka kwa baadhi ya watu kwamba mikopo yao haina riba, n.k. Naomba tujuzane yafuatayo:-
1. Je, ni kweli kwamba akaunti za mfumo huu wa kiislamu hazina riba?
2. Je, ni kila raia anaruhusiwa kuwa na akaunti ya aina hii au ni kwa ajili ya waislamu tu?
3. Je, kama kila raia anaruhusiwa kuwa na akaunti kuna sharti lingine lolote lenye mwelekeo wa kidini ambalo wasio waislamu wanatakiwa kulitimiza?
4. Je, benki ya kiislamu nayo ni ibada kama inavyodaiwa kwa mahakama ya kadhi?
5. Hili suala limekaaje Kikatiba?
Nawasilisha.
Kuna kitu kinaitwa Benki ya Kiislamu (ISLAMIC BANKING). Tafadhali naomba mwenye habari jinsi hiki chombo kinavyofanya kazi atupashe habari. Ni muda kidogo umepita tangu NBC na KCB (T) Ltd. waanzishe akaunti za kiislamu lakini inawezekana wengi wetu, wakiwepo baadhi ya waislamu, hatuko well informed na hiki kitu.
Leo katika Gazeti la Raia Mwema nimeona tangazo la BoT - ISLAMIC BANKING TRAINING PROGRAM ambapo BoT kwa kushirikiana na taasisi moja ya ushauri kutoka Jordan itaendesha mafunzo juu ya Benki ya Kiislamu. Nimewahi pia kusikia kutoka kwa baadhi ya watu kwamba mikopo yao haina riba, n.k. Naomba tujuzane yafuatayo:-
1. Je, ni kweli kwamba akaunti za mfumo huu wa kiislamu hazina riba?
2. Je, ni kila raia anaruhusiwa kuwa na akaunti ya aina hii au ni kwa ajili ya waislamu tu?
3. Je, kama kila raia anaruhusiwa kuwa na akaunti kuna sharti lingine lolote lenye mwelekeo wa kidini ambalo wasio waislamu wanatakiwa kulitimiza?
4. Je, benki ya kiislamu nayo ni ibada kama inavyodaiwa kwa mahakama ya kadhi?
5. Hili suala limekaaje Kikatiba?
Nawasilisha.