Is God fair ?

Is God fair ?

Kwa nini mmakonde achonge kinyago (assume kinyago kinahoji vinyago vingine)

Mungu wako unamfananisha na Mmakonde?

Unafanana kanuni za kufananisha zinakataza kufananisha visivyofanana?

Mmakonde hana ujuzi wote, uwezo wala upendo wote.

Mungu wakonpia hana ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote?

Kinyago hakiwezi kuwa sawa na mimi, hakiwezi kuuliza maswali, mini naweza.

Mpaka hapo mfano wako usha fail.

Epic fail.
 
Kwa hiyo umeshindwa kuthibitisha uwepo wa roho?

wataka uthibitisho wa aina gani ? labda uanze wewe kunithibitishia kama unazo akili hata kama sio timamu ili nijifinze namna mnavyothibitisha visivyo matter.
twende kazi...
 
Hoja ipi ya msingi sijaijibu? Hebu niulize hapa kweupeeeee watu wanasoma.

Mimi hoja zangu za msingi ambazo hazijajibiwa hizi hapa.

1. Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu wenye kuwezekana mabaya na maovu wakati uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya na maovu hayawezekani alikuwa nao?

2. Kwa nini mungu mwenye ukamilifu wote aumbe chochote? Kutaka kuumba ni kukosa ukamilifu, utasemaje mungu mkamilifu kaona haja ya kuumba wakati haja ya kuumba ni kukosa ukamilifu?

3. Imekuwaje mungu mjuzi wa yote na muweza yote akapanga mambo halafu akaghairi? Alivyoanza kupanga si alijua yote, kaghairi vipi tena?

4. Imekuwaje mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote akakasirika? Kukasirika kunatokana na kujua kipya ambacho hukutegemea, huyu mungu mjuzi wa yote kipya kipi kitakachomtoa katika furaha na kumkasirisha?

5. Unaweza kuthibitisha kwamba mungu yupo bila kujichanganya mwenyewe?

6. Unaweza kuthibitisha roho ipo na kuhakikisha kwamba si hadithi ya uongo tu?

7. Kama mungu anajua kila kitu na anapanga kila kitu, wanaosemwa kufanya dhambi na watahukumiwa siku ya hukumu kwa nini wanahukumiwa na wanaosemwa wamefanya mazuri wanapewa thawabu kwa nini wakati vyote vimepangwa na mungu?

8. Kama nipo njia panda, nataka kuamua kwamba nichukue njia ya kulia au ya kushoto, mungu anajua nitachukua njia gani? Kama anajua mimi nina maamuzi kweli? Kama hajui, mungu anajua yote kweli?

9. Kwa nini mungu mjuzi wa yote na mwenye uwezo wote hajiweki wazi watu wote tumjue bila utata?

10. Je, mungu anaweza kuumba jiwe zito kiasi yeye mwenyewe ashindwe kulibeba? Kama anaweza, basi kuna kitu hawezi, nacho ni kubeba hili jiwe, kama hawezi, basi kuna kitu hawezi, nacho ni kuumba hili jiwe. Either way mungu muweza yote hayupo. Unaweza kubisha?

Mimi nishaweka wazi hoja zangu ambazo hazijajibiwa. Zijibu. Weka zako.Nitazijibu, hata kama ni kwa kusema sijui tu.

sasa ili ujibiwe lazima tuweke frequency zetu sawa.
1.-uwezo wote ni kitu gani na unapimwaje
-ujuzi wote ni nini na kipimo chake nini
-upendo ni nini na kipimo.chake nini ?
-Je ? kwanini unafikiri uwezo,ukamilifu na upendo ndivyo vitu vinavyohitajika kuumba ulimwengu mkamilifu ?

jibu ili tuondoe FALLACY OF DEFINITIONS.
2.Kwanini haja ya kuumba iwe ndicho kipimo cha kukosa ukamilifu ?

3.nini maana ya kughairi na uhusiano wale na ujuzi wote ukoje ?

4.kukasirikia ndiyo nini na nini kipimo chake kadri ya Mungu anavyohusika ?
5.inawezekana kabisa kama tutaondoa FALLACY OF DEFINITION zinazoathiri uwezo wako wa kufikiri.

6.Ndiyo baada ya kuondoa FALLACY OF DEFINITION. Roho unayohoji uwepo wake ni nini ?

7.kuna husiano gani kati ya kujua kila kitu na kuenfluence uchaguzi wa binadam mwenye free will ?
tiondoe kwanza FALLACY OF DEFINITION ili utibiwe ipasavyo.

8.kujua na kumfanya mtu aamue ni vitu viwili tofauti...
lakini tuondoe kwanza msingi wa tatizo linalokukabili ndiyo tukufundishe...

9.Mungu kajiweka wazi kabisa kwa wenye nia ya kumjua rejea zipo.
labda Mungu ni.nini au ni nani ?
Tuondoe FALLACY OF DEFINITION.

10. Swali lako limejibiwa mara nyingi sana japo kulariri kunakufanya ushindwe kujitambua na kuona jibu.
kuunda jiwe kubwa na kuweza kulibeba ni sehemu ya mwenye uwezo wote.
lakini kuumba jiwe kubwa na kushindwa kulibeba ni hoja ya kichaa maana uwezo wote ni kinyume cha kukosa uwezo.

Safisha uwanja kwa kuondoa hizo FALLACIES then upelekwe jando.
 
wataka uthibitisho wa aina gani ? labda uanze wewe kunithibitishia kama unazo akili hata kama sio timamu ili nijifinze namna mnavyothibitisha visivyo matter.
twende kazi...

A construct that is logically consistent.
 
A construct that is logically consistent.

ANZA KWA KUELEZA LIGIC NI NINI ? imetokana na nini/nani; then
thibitisha kwamba wewe unazo akili hata kama sio timamu kwa kuweka "A construct that is logically consistent "
 
sasa ili ujibiwe lazima tuweke frequency zetu sawa.
1.-uwezo wote ni kitu gani na unapimwaje
-ujuzi wote ni nini na kipimo chake nini
-upendo ni nini na kipimo.chake nini ?
-Je ? kwanini unafikiri uwezo,ukamilifu na upendo ndivyo vitu vinavyohitajika kuumba ulimwengu mkamilifu ?

jibu ili tuondoe FALLACY OF DEFINITIONS.
2.Kwanini haja ya kuumba iwe ndicho kipimo cha kukosa ukamilifu ?

3.nini maana ya kughairi na uhusiano wale na ujuzi wote ukoje ?

4.kukasirikia ndiyo nini na nini kipimo chake kadri ya Mungu anavyohusika ?
5.inawezekana kabisa kama tutaondoa FALLACY OF DEFINITION zinazoathiri uwezo wako wa kufikiri.

6.Ndiyo baada ya kuondoa FALLACY OF DEFINITION. Roho unayohoji uwepo wake ni nini ?

7.kuna husiano gani kati ya kujua kila kitu na kuenfluence uchaguzi wa binadam mwenye free will ?
tiondoe kwanza FALLACY OF DEFINITION ili utibiwe ipasavyo.

8.kujua na kumfanya mtu aamue ni vitu viwili tofauti...
lakini tuondoe kwanza msingi wa tatizo linalokukabili ndiyo tukufundishe...

9.Mungu kajiweka wazi kabisa kwa wenye nia ya kumjua rejea zipo.
labda Mungu ni.nini au ni nani ?
Tuondoe FALLACY OF DEFINITION.

10. Swali lako limejibiwa mara nyingi sana japo kulariri kunakufanya ushindwe kujitambua na kuona jibu.
kuunda jiwe kubwa na kuweza kulibeba ni sehemu ya mwenye uwezo wote.
lakini kuumba jiwe kubwa na kushindwa kulibeba ni hoja ya kichaa maana uwezo wote ni kinyume cha kukosa uwezo.

Safisha uwanja kwa kuondoa hizo FALLACIES then upelekwe jando.

1. Uwezo wote ni kutoshindwa kitu na unapimwa kwa mantiki. Ujuzi wote ni kutokosa kujua kitu na unapimwa kwa mantiki. Upendo wote ni kilele cha upendo na kipimo chake ni mantiki.

Nani kasema uwezo, ukanilifu na upendo ndio vitu vinavyohitaji (sic) kuumba ulimwengu mkamilifu?

2. Kilichokamikika hakihitaji kuumba, kuhitaji kuumba au kuhitaji kikote ni upungufu wa ukamilifu.

3. Kughairi ni kipanga kifanya kitu na baadaye kutengua usifanye. Mwenye kujua yote anayajua mambo yote mwanzo wake na mwisho wake, hivyo hawezi kughairi, mungu anayejua yote hawezi kughairi, mungu wenu inakiwaje aghairi mioango yake kama kweli anajua yote?

4. Kukasirika ni udhaifu wa kukosa kiweza kuhimili mhamaniko baada ya kugundua kukosa kupata unachotaka, mungu mwenye kujua yote, kuweza yote na upendo wote hawezi kukasirika kwa sababu hawezi kihamanika, hawezi kujua kipya cha kumkasirisha na hawezi kugundua kwani amejua yote, huyu mungu mnayesema anakasirika anakasirikaje?


5. Fallacy kubwa zaidi ni yako ya kusema fallacy by fiat bula kuitaja iko wapi na kivipi ni fallacy.

6. Wewe muamini mungu na roho unaniuliza mimi roho ni nini?

7. Ujuzi wa mungu wenu mnavyousema si utabiri wa hali ya hewa, au inataka kusema ujuzi wa mungu wenu ni wa kubahatisha kwamba anaweza kujua mvua itanyesha halafu isinyeshe? Ikiwa akijua itanuesha lazima itanyesha, tofauti ya ujuzi wake huo na kusababisha inyeshe ni nini? Hususan kwa sababu kila kitu kinaenda kwa command yake?

8. Ama mungu anajua yote na mwanadamu bana maamuzi, ama mwanadamu ana maamuzi na mungu hajui yote. You can't eat your cake and have it too.

9. Kama kajiweka wazi kabisa, mbona mimi sioni hivyo? Mbona ana contradictions kibao kama ya mungu mjua yote, muweza yote na mwenye upendo wote kuumba ulimwengu wenye mateso na mabaya? Hujajibu hili swali.

10. Hujajibu swali, umelikimbia tu.
 
Kwa nini Blackman anauliza maswali anayouliza ?

Wewe mjani kabla yabkula itakuharibu ibo go huo, umevamia maji marefu sasa umeshindwa kujibu maswali unabaki kuuliza utaukiza moaka "Kwa nini Nkwesa Makambo anaukiza maswali anayouliza?".

Ushathibitisha kwamba roho ipo? Inapimwa kwa kipimo gani?
 
Last edited by a moderator:
Kuhitaji kuumba kitu ni kukosa ukamilifu.

Unahitaji kujenga nyumba kwa sababu unaona kuna hitaji la makazi.

Unahitaji kupika chakula kwa sababu kuna njaa.

Unahitaji kufuma labda pengine uko bored, kuna kitu kina miss, unaumba kitu.

Huyu mungu mkamilifu imekuwaje mpaka akahitaji kuumba?

Alikuwa lonely akataka tumpe kampani?

Kila kitu kina sifa zake,kwahiyo unapomzungumzia Mungu basi inabidi ukumbuke kuwa kati moja ya sifa zake ni kuumba.

Twende taratibu.
 
Kwa sababu si kipimo chake, kipimo chake decidel.

Roho kipimo chake nini? Hujajibu swali.

Sijauliza kuhusu hicho kipimo cha decidel, mie nimeuliza kwanini sauti iwe haiwezi kupimwa rangi?haijalishi kipimo gani
 
Hahaha, dunia ina ma tsunami yanaua mpaka vitoto vichanga, ma Ebola ma vita ya kila aina.

Halafu mtu anakwambia imeumbwa na mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote.
'
What a sick joke!

Nilikuuliza msingi anaotumia Mungu kuumba ni upi?ulikosa jibu,sasa mie navyojua Mungu hakutuumba ili tuje kustarehe hapa duniani,laiti angesema hivyo basi kweli tungeshangaa ni vp kuna tsunami na majanga mengine.
 
Mbona kulaumiana kumezidi zaidi ya hoja hii inamaana huwezo wenu wa kubishana kihoja umefika kimono..
 
Nilikuuliza msingi anaotumia Mungu kuumba ni upi?ulikosa jibu,sasa mie navyojua Mungu hakutuumba ili tuje kustarehe hapa duniani,laiti angesema hivyo basi kweli tungeshangaa ni vp kuna tsunami na majanga mengine.

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote atuumbe katika ulimwengu anbao mateso yanawezekana?

Sijaongekea starehe, nimeongekea tsunamis and Ebola.

A life guaranteed to be free of Ebola and tsunamis is not necessarily starehe.

Even if a case for starehe can be made.

But I don't expect you to get that through your head.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom