Is God fair ?

Is God fair ?

Kila kitu kina sifa zake,kwahiyo unapomzungumzia Mungu basi inabidi ukumbuke kuwa kati moja ya sifa zake ni kuumba.

Twende taratibu.

Kwa nini mungu kaumba?

Kwa nini mungu mwenye ujuzi wote na ukamilifu wote aone haja ya kuumba?
 
Mbona kulaumiana kumezidi zaidi ya hoja hii inamaana huwezo wenu wa kubishana kihoja umefika kimono..

Siwezi kubishana kihoja na mtu anayeuliza logic ni nini.

Unamuuliza mtu, imekuwaje mungu mkamilifu aone haja ya kuumba? Kuona haja ya kuumba kwenyewe tu si kukosa ukamilifu?

Mtu anakosa jibu, anskosa hoja, analeta viroja.
 
Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote atuumbe katika ulimwengu anbao mateso yanawezekana?

Sijaongekea starehe, nimeongekea tsunamis and Ebola.

A life guaranteed to be free of Ebola and tsunamis is not necessarily starehe.

Even if a case for starehe can be made.

But I don't expect you to get that through your head.

Msingi wa uumbaji wake ni upi?
 
1. Uwezo wote ni kutoshindwa kitu na unapimwa kwa mantiki. Ujuzi wote ni kutokosa kujua kitu na unapimwa kwa mantiki. Upendo wote ni kilele cha upendo na kipimo chake ni mantiki.

Nani kasema uwezo, ukanilifu na upendo ndio vitu vinavyohitaji (sic) kuumba ulimwengu mkamilifu?

2. Kilichokamikika hakihitaji kuumba, kuhitaji kuumba au kuhitaji kikote ni upungufu wa ukamilifu.

3. Kughairi ni kipanga kifanya kitu na baadaye kutengua usifanye. Mwenye kujua yote anayajua mambo yote mwanzo wake na mwisho wake, hivyo hawezi kughairi, mungu anayejua yote hawezi kughairi, mungu wenu inakiwaje aghairi mioango yake kama kweli anajua yote?

4. Kukasirika ni udhaifu wa kukosa kiweza kuhimili mhamaniko baada ya kugundua kukosa kupata unachotaka, mungu mwenye kujua yote, kuweza yote na upendo wote hawezi kukasirika kwa sababu hawezi kihamanika, hawezi kujua kipya cha kumkasirisha na hawezi kugundua kwani amejua yote, huyu mungu mnayesema anakasirika anakasirikaje?


5. Fallacy kubwa zaidi ni yako ya kusema fallacy by fiat bula kuitaja iko wapi na kivipi ni fallacy.

6. Wewe muamini mungu na roho unaniuliza mimi roho ni nini?

7. Ujuzi wa mungu wenu mnavyousema si utabiri wa hali ya hewa, au inataka kusema ujuzi wa mungu wenu ni wa kubahatisha kwamba anaweza kujua mvua itanyesha halafu isinyeshe? Ikiwa akijua itanuesha lazima itanyesha, tofauti ya ujuzi wake huo na kusababisha inyeshe ni nini? Hususan kwa sababu kila kitu kinaenda kwa command yake?

8. Ama mungu anajua yote na mwanadamu bana maamuzi, ama mwanadamu ana maamuzi na mungu hajui yote. You can't eat your cake and have it too.

9. Kama kajiweka wazi kabisa, mbona mimi sioni hivyo? Mbona ana contradictions kibao kama ya mungu mjua yote, muweza yote na mwenye upendo wote kuumba ulimwengu wenye mateso na mabaya? Hujajibu hili swali.

10. Hujajibu swali, umelikimbia tu.

mantiki ni nini na chanzo na kipimo chake hujajibu.
kutumia kitu chenye maana usiyoijua na kutaka ueleweke ni majanga.
jibu kwanza mantiki ni nini ? nini chanzo/asili yake na kipomo chake.
 
Kwa nini mungu kaumba?

Kwa nini mungu mwenye ujuzi wote na ukamilifu wote aone haja ya kuumba?

Nimekwambia kila kitu kina sifa zake,ukamilifu na ujuzi wote hizi ni sifa za Mungu na nikakwambia Mungu anayo pia sifa ya kuumba.kwahiyo unapo hoji kitu kwanza lazima ujue sifa za hicho kitu.
 
Aliyetundikwa ni mwili wa Yesu,Immanuel wa Nazareth,ila roho yake haikufa,na ndio maana alisema,mikononi mwako baba,naiweka roho yangu

Tena akamwambia yule mwizi aliyetubu kuwa,kwa hakika usiku wa leo tutakuwa wote peponi...need i say more Mr Kiranga?

Aisee, even more contradiction, kwa hiyo huyo jamaa naye si mungu pia (kwa maandiko yenu)? Sasa hiyo roho aliiweka wapi ilhali nao hao watatu mnadai kwamba ni mmoja?
 
God is always fair & everything happens 4 a reason,never loose hope & faith

Sijui utakuwa wa imani gani but try to read

1 Corinthians 10:13

Really?

Tell that to the Haitians and their earthquake;
Tel that to the victims of 2004 tsunami;
Tell that to the victims of Ethiopian famine of 1980s;
Tell that to the victims of Rwandan 1994 genocide;
etc., etc!

CC: Kiranga
 
Siwezi kubishana kihoja na mtu anayeuliza logic ni nini.

Unamuuliza mtu, imekuwaje mungu mkamilifu aone haja ya kuumba? Kuona haja ya kuumba kwenyewe tu si kukosa ukamilifu?

Mtu anakosa jibu, anskosa hoja, analeta viroja.

Lazy.. ukamilifu ni nini? 🙂
 
Ikawa mchana ikawa usiku ,siku ya kwanza!,Kisha mungu akaumba ardhi na mbingu,sijui na vitu gani,afu mwisho akaviona vyote ni vyema!.

Iwapo mungu(kama yupo)mwenye mamlaka yote anapata wazo la kuumba kitu kwa umbo flani basi lazima kuna mahala anapotoa wazo hilo.Mungu (kama yupo)hawezi akawa ama akaona haja ya kuumba.Yaan kitu /mtu mwenye uwezo wote aspend siku sita anaumba?.


There is NO god but only the Idea that there is god!.
 
Mimi kama mwanadamu ama kiumbe hai nikihitaji kunywa maji ni dalili kwamba sijakamilika kwa maana bila hivyo nitasafa kwa kiu.Nikihitaji kwenda mjini maana yake nitasafiri hadi mjini hiyo ni dalili kwamba sijakamilika kwa maana ningeweza kuwa mjini wakati ule ule kama ningekuwa n uwezo wote.

Kitendo cha mungu wenu kuona haja ya kuwa na viumbe hai na kuspend dayz akiviumba ni dalili ya kutokamilika kwake kama yupo.Kwa maana ile kuwaza tu kwamba nahitaji kuwa na ulimwengu wa aina hii ama viumbe wa aina hii ni kutokamilika kwenyewe.Kwa maana hiyo kwa uumbaji mungu wenu alidhani atakamilika ndio maana alikuwa anaona kila alichokiumba ni chema.Ile kuona tu kwamba ni chema ni udhaifu tayar.


Lakini pamoja na hivyo inasemekana kwamba bado mungu wenu (kama yupo)aliona haja ya kuwaletea mkombozi!(wale wa jumapili mnamwita yesu),na mitume kwamba aje kuwakumbusha eti mungu wenu anataka mfanye nini.


Hizi ni dalili kwamba HAKUNA mungu ila ni harakati tu za mwanadamu za kutaka kumuumba mungu.

Karibuni katika ulimwengu huru.
 
Mimi kama mwanadamu ama kiumbe hai nikihitaji kunywa maji ni dalili kwamba sijakamilika kwa maana bila hivyo nitasafa kwa kiu.Nikihitaji kwenda mjini maana yake nitasafiri hadi mjini hiyo ni dalili kwamba sijakamilika kwa maana ningeweza kuwa mjini wakati ule ule kama ningekuwa n uwezo wote.

Kitendo cha mungu wenu kuona haja ya kuwa na viumbe hai na kuspend dayz akiviumba ni dalili ya kutokamilika kwake kama yupo.Kwa maana ile kuwaza tu kwamba nahitaji kuwa na ulimwengu wa aina hii ama viumbe wa aina hii ni kutokamilika kwenyewe.Kwa maana hiyo kwa uumbaji mungu wenu alidhani atakamilika ndio maana alikuwa anaona kila alichokiumba ni chema.Ile kuona tu kwamba ni chema ni udhaifu tayar.


Lakini pamoja na hivyo inasemekana kwamba bado mungu wenu (kama yupo)aliona haja ya kuwaletea mkombozi!(wale wa jumapili mnamwita yesu),na mitume kwamba aje kuwakumbusha eti mungu wenu anataka mfanye nini.


Hizi ni dalili kwamba HAKUNA mungu ila ni harakati tu za mwanadamu za kutaka kumuumba mungu.

Karibuni katika ulimwengu huru.

mawazo haya hayawezi toka kwenye kichwa cha binadam...
Labda bado.linyani.linaevolve kulelekea kwenye sijui unini.
maana bin adam ni kutokana na adam aliyeumbwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom