Is God fair ?

Is God fair ?

Mimi naamini Mungu lakini sijawahi hata siku moja kuona mwamini Mungu mwenzangu akijibu hoja zako kwa ufasaha hapa JF.

Ni afadhari mimi ninayeamini Mungu yupo kwani siku ya mwisho hata kama kweli hayupo i will lose nothing.

Mkuu kama hoja ipi?
 
Sasa mbona unakanyaga matapishi yako mwenyewe!
Lete hoja za kupinga Mungu nje ya vitabu vya dini.

Katika ulichonukuu, wapi kumetajwa kitabu cha dini?

Matapishi gani hayo unayoyasema?

Bill Gates kanywa maji yaliyochujwa kutoka mavi, wewe unaona hatari kula matapishi tu?
 
Kwanza kabisa objection si kwamba ulimwengu unanikera, bali ni kwamba ilimwengu inapingana na nature yake ya mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na mwenye upendo wote.

Pili ingekuwa vizuri unaposema nilishajibiwa unipe link.

Maana unaweza kufikiri umejibu muafaka kwa kusema :mungu haulizwi kwa nini kafanya hiki au kile", mimi nikakwambia hilo si jibu, ni kukinali kwamba hujui jibu.

Unaposema mungu katofautisha viymbe vyake, wengine kawapa akili ya kufikiri, wengine hayawani, huyu mungu gani ana ubaguzi?

Kwa nini wengine kawapa akili na wengine kawafanya hayawani wakati alikuwa na uwezo wa kuwapa akili wote bila ya kipungukiwa na kitu?

Kwa nini hawa hayawani kawabania? Wamemkosea nini? Yeye si mungu wa upendo wote? Mbona anapendelea viumbe wake wengine anawapa akili ya kichambua mema na mabaya, wengine anawafanya hayawani?

Huyu mungu ana upendo wote kweli?

Huyu mungu yupo kweli?

kwa mantiki hiyo hiyo huu mjadala hauna mwisho
kwa kuwa wewe kila utachoambiwa utahoji kwanini isipokuwa wewe ukisema sababu ni nguvu za uvutano so and so waona umejibu.
yatizo ni ubongo wako umeghoshiwa hauwezi kukubali elimu mpya.
unawaza kisayansi ambapo unahusika na matter pekee ndiyo sababu huishiwi maswali ya majinga majinga yanayoonyesha kiwango cha juu sana cha upumbavu.
dunia na viluvyomo matter and spirits ni mfumo mmoja unaotenda kazi pamoja. kuumba vyenye akili ilikuwa ni kuweka utambulisho wa visvyo na akili sawa na vingine malengo na madhumuni ya Mungu kuweka hivi vilivyo na namna wenye maarifa sawia ya kibinadam wanavyoelewa ni tofauti na wanadam wasio na maarifa ya mfumo kama Kiranga et al
hivyo contradiction unayoiona wewe ni mind illusion yako na waliokosa maarifa wenzako.
umelumbushwa mara nyingi juu ya FALLACY OF DEFINITION ambayo ndiyo msingi wa illusion inayokukabili lakini hustuki hata...
 
Last edited by a moderator:
Upepo ni mwendo wa hewa kwa mawimbi kutoka eneo lenye presha kubwa kwenda kwenye presha ndogo, unapimwa kwa kipimo kinachoitwa anemometer kinachoweza kupima upepo unaelekea wapi na kwa kasi gani.

Anemometer - Wikipedia, the free encyclopedia

Roho ni nini na inapimwa kwa kipimo gani?

Roho ni uwezo unaomuewezesha kiumbe kuwa na uhai,kwahiyo kiumbe hata kiwe na viungo vyote lakini bila roho kinakuwa hakina uhai.
 
Tatizo unanipa ushahidi wa maandiko ya mungu badala ya kunipa ishahidi wa uwepo wa mungu.

Sababu unajengea hoja kwa kutumia maneno ya Mungu,hivyo jenga hoja nje ya maneno ya Mungu.
 
Sababu unajengea hoja kwa kutumia maneno ya Mungu,hivyo jenga hoja nje ya maneno ya Mungu.

Itasemaje najengea hoja maneno ya mungu kabla hujathibitisha kwamba mungu yupo?

Umejuaje maneno haya ni ya mungu na si ya binadamu tu kabla hujathibitisha kuwepo kwa mungu?
 
Upepo ni mwendo wa hewa kwa mawimbi kutoka eneo lenye presha kubwa kwenda kwenye presha ndogo, unapimwa kwa kipimo kinachoitwa anemometer kinachoweza kupima upepo unaelekea wapi na kwa kasi gani.

http://en.m.wikipedia.org/wiki/Anemometer

Roho ni nini na inapimwa kwa kipimo gani?

Hewa ni nini ?
presha kubwa na presha ndogo ni nini ?
kwanini iwe ni presha inasababisha na sio kitu kingine ?
 
Kama mungu yupo, muweza yote, mjuzi wa yote, mwenye upendo wote, kwa nini kaumba dunia ambayo ina uwezekano wa kuwa na mabaya, mateso, dhiki, etc wakati alikuwa na iwezo wa kuumba dunia ambayo hivyo haviwezekani?

Narudia tena kusema kwamba
Mungu angetaka kuumba ulimwengu ambao watu
hawafanyi maovu,basi yeye angejua kila kitu kuhusu hivyo viumbe kabla hata hayajatokea mwanzo hadi mwisho(sababu ni mjuzi wa yote).Na pia yeye ndiyo angepanga kila kitu kuhusu hao viumbe,hakuna ambacho
kingetokea pasina yeye kukitaka
kutokea,hivyo Mungu anaumba na
hufanya vile atakavyo sababu ndiyo mwenye nguvu na muweza yote. Sasa tunapokuja kwenye ulimwengu wetu ambao tunafanya maovu na mambo mengine,ni vilevile tu kwamba Mungu
anayajua yote ambayo tunayoyafanya na ambayo bado kuyafanya,Yote ambayo yanatokea ktk ulimwengu basi ni yeye(mwenye uwezo wa yote)
ndiyo ametaka yatokee hakuna
kinachotokea ambacho hakikuwa ni matakwa yake. Matakwa yake yapo aina:yapo ya aina mbili,kuna mipangilio ya kiulimwengu ambayo kama kuchomoza kwa jua na kuzama,mvu n.k(na ndiyo ktk dalili za uwepo wake), hayo yote ni matakwa yake..halafu matakwa ya aina ya pili ndiyo haya tunayofanya sisi kama hayo maovu na mengineyo,ametuacha tufanye
tutakavyo lakini ni ndani ya matakwa yake,kwa maana hiyo ambalo hatolitaka hatutoweza kulifanya.Ndiyo maana anasema kuwa anaumba na kufanya atakavyo. Nalaiti angependa hao wanaofanya maovu kutokufanya hayn maovu basi wasingefanya,kama alivyowafanya malaika.
 
Katika ulichonukuu, wapi kumetajwa kitabu cha dini?

Matapishi gani hayo unayoyasema?

Bill Gates kanywa maji yaliyochujwa kutoka mavi, wewe unaona hatari kula matapishi tu?

Unahoji upendo wa Mungu,sasa huo upendo wa Mungu umeusikia wapi wewe kama sio vitabu vya dini(maneno ya Mungu ambaye hauamini kama yupo)?
 
Hewa ni nini ?
presha kubwa na presha ndogo ni nini ?
kwanini iwe ni presha inasababisha na sio kitu kingine ?

Hewa ni mchanvanyiko wa gas mbalimbali.

Presha kubwa na ndogo ni matokeo ya mtiririko wa uzito wa molekyuli za hewa.

Ni presha inayosababisha na si kitu kingine kwa mujibu wa second law of thermodynamics.

Maswali yenu nawajibu, swali langu hamjajibu.

Unaweza kuyjibitisha roho ipo? Kwa kipimo gani?
 
Narudia tena kusema kwamba
Mungu angetaka kuumba ulimwengu ambao watu
hawafanyi maovu,basi yeye angejua kila kitu kuhusu hivyo viumbe kabla hata hayajatokea mwanzo hadi mwisho(sababu ni mjuzi wa yote).Na pia yeye ndiyo angepanga kila kitu kuhusu hao viumbe,hakuna ambacho
kingetokea pasina yeye kukitaka
kutokea,hivyo Mungu anaumba na
hufanya vile atakavyo sababu ndiyo mwenye nguvu na muweza yote. Sasa tunapokuja kwenye ulimwengu wetu ambao tunafanya maovu na mambo mengine,ni vilevile tu kwamba Mungu
anayajua yote ambayo tunayoyafanya na ambayo bado kuyafanya,Yote ambayo yanatokea ktk ulimwengu basi ni yeye(mwenye uwezo wa yote)
ndiyo ametaka yatokee hakuna
kinachotokea ambacho hakikuwa ni matakwa yake. Matakwa yake yapo aina:yapo ya aina mbili,kuna mipangilio ya kiulimwengu ambayo kama kuchomoza kwa jua na kuzama,mvu n.k(na ndiyo ktk dalili za uwepo wake), hayo yote ni matakwa yake..halafu matakwa ya aina ya pili ndiyo haya tunayofanya sisi kama hayo maovu na mengineyo,ametuacha tufanye
tutakavyo lakini ni ndani ya matakwa yake,kwa maana hiyo ambalo hatolitaka hatutoweza kulifanya.Ndiyo maana anasema kuwa anaumba na kufanya atakavyo. Nalaiti angependa hao wanaofanya maovu kutokufanya hayn maovu basi wasingefanya,kama alivyowafanya malaika.

Sasa kama hakuna kinachotokea ambacho si matakwa yake, wanaofanya dhambi watahukumiwa kwa nini na wanaofanya mema watapewa thawabu kwa nini?

Si mambo yote kapanga mungu?

Mungu atamhukumu vipi mwanadamu kwa kufanya mabaya wakati yote kayapanga yeye mwenyewe?
 
Unahoji upendo wa Mungu,sasa huo upendo wa Mungu umeusikia wapi wewe kama sio vitabu vya dini(maneno ya Mungu ambaye hauamini kama yupo)?

Vitabu vya dini si hoja.

Hoja ni mantiki.

Kama una maelezo kutika kitabu cha dini yenye mantiki yalete hapa, mimi sina matatizo na kitabu.

Tatizo langu ni pale utakapofanya kile kisicho na mantiki kina mantiki kwa kuwa tu kinatoka katika kitabu cha dini.
 
Kwanza kabisa objection si kwamba ulimwengu unanikera, bali ni kwamba ilimwengu inapingana na nature yake ya mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na mwenye upendo wote.

Pili ingekuwa vizuri unaposema nilishajibiwa unipe link.

Maana unaweza kufikiri umejibu muafaka kwa kusema :mungu haulizwi kwa nini kafanya hiki au kile", mimi nikakwambia hilo si jibu, ni kukinali kwamba hujui jibu.

Unaposema mungu katofautisha viymbe vyake, wengine kawapa akili ya kufikiri, wengine hayawani, huyu mungu gani ana ubaguzi?

Kwa nini wengine kawapa akili na wengine kawafanya hayawani wakati alikuwa na uwezo wa kuwapa akili wote bila ya kipungukiwa na kitu?

Kwa nini hawa hayawani kawabania? Wamemkosea nini? Yeye si mungu wa upendo wote? Mbona anapendelea viumbe wake wengine anawapa akili ya kichambua mema na mabaya, wengine anawafanya hayawani?

Huyu mungu ana upendo wote kweli?

Huyu mungu yupo kweli?

Hiyo sio hoja kabisa tena ni vichekesho.
Hivi hawa masikini waliyopo duniani na wakati kuna matajiri kibao na wanahela nyingi kupitiliza, Je tunaweza kuwalaumu na kusema wanaroho mbaya kwa kutokuwapa hizo hela zao masikini?
 
Hewa ni mchanvanyiko wa gas mbalimbali.

Presha kubwa na ndogo ni matokeo ya mtiririko wa uzito wa molekyuli za hewa.

Ni presha inayosababisha na si kitu kingine kwa mujibu wa second law of thermodynamics.

Maswali yenu nawajibu, swali langu hamjajibu.

Unaweza kuyjibitisha roho ipo? Kwa kipimo gani?

gas ni nini ? gas inasababishwa na nini/nani ?
molekyuli ni nini na zinasababishwa na nini / nani ?
second law of thermodynamics nani aliitengeneza au kuiweka ?
nani kakwambia umemaliza kujibu maswali yetu ?
 
Hiyo sio hoja kabisa tena ni vichekesho.
Hivi hawa masikini waliyopo duniani na wakati kuna matajiri kibao na wanahela nyingi kupitiliza, Je tunaweza kuwalaumu na kusema wanaroho mbaya kwa kutokuwapa hizo hela zao masikini?

Huwezi kuwalaumu matajiri.

Matajiri hawana ujuzi wote, hawana uwezo wote wala hawana upendo wote.

Unachekesha wewe unayefananisha mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote na matajiri.

Na hata hao matajiri tunawaona wanatoa kusaidia maskini. Bill Gates anasaidia mitadi ya kutokomeza maradhi, Zuckerberg kagoa dola milioni 25 kutokomeza Ebola.

Mungu ambaye anaweza kutokomeza Ebola kwa fikra tu mbona hatokomezi?

Ndio upendo wote huu?
 
Itasemaje najengea hoja maneno ya mungu kabla hujathibitisha kwamba mungu yupo?

Umejuaje maneno haya ni ya mungu na si ya binadamu tu kabla hujathibitisha kuwepo kwa mungu?

Ndiyo maana nikakwambia jenga hoja ya kupinga Mungu nje ya vitabu vya dini.
 
gas ni nini ? gas inasababishwa na nini/nani ?
molekyuli ni nini na zinasababishwa na nini / nani ?
second law of thermodynamics nani aliitengeneza au kuiweka ?
nani kakwambia umemaliza kujibu maswali yetu ?

Nimejibu maswali mara ai chini ya nne mfululizo.

Kabla ya kuendelea kujibu, ili nisiuelemee sana upande wako kwa kujibu maswali yenu sana bila ya yangu kujibiwa, nakupa nafasi ujibu swali langu.

Roho ni nini? Unathibitishaje kwamba ipo na si hadithi ya uongo tu? Kwa kipimo gani?
 
Ndiyo maana nikakwambia jenga hoja ya kupinga Mungu nje ya vitabu vya dini.

Hoja yangu ni logic.

Kwamba ukweli una logical consistency.

Maelezo yenu ya mungu (regardless ya yalipotoka) hayana logical consistency.

Nje ya vitabu vya dini hakuna suala la kuwapo kwa mungu unayemsema.
 
Itasemaje najengea hoja maneno ya mungu kabla hujathibitisha kwamba mungu yupo?

Umejuaje maneno haya ni ya mungu na si ya binadamu tu kabla hujathibitisha kuwepo kwa mungu?

Ndiyo maana nikakwambia jenga hoja ya kupinga Mungu nje ya vitabu vya dini.


Ila Uwezo wa kukuthibitishia kuwa ni maneno ya Mungu ninao na huwezi kupinga hata chembe.
 
Nimejibu maswali mara ai chini ya nne mfululizo.

Kabla ya kuendelea kujibu, ili nisiuelemee sana upande wako kwa kujibu maswali yenu sana bila ya yangu kujibiwa, nakupa nafasi ujibu swali langu.

Roho ni nini? Unathibitishaje kwamba ipo na si hadithi ya uongo tu? Kwa kipimo gani?

tumalize maswali yangu then tuhamie kwenye unayotaka kujibiwa...
angalizo sisi hutajaathiriwa ubongo na sayansi; hivyo mimi najua binadamu ni mwili pamoja na viuongo vyake vitendavyo kazi,nafsi na roho.
mwili ni matter ambao unamaelezo ya lisayansi kwa kuwa sayansi inauwezo wa kujua mattera pekee.
hivyo ukitaka kupewa jibu la kisayansi itakuwa ni swala la lugha gongana.
sina hakika kama waelewa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom