Point of correction;
"Sijauliza nani anaamua,kwa nini anaamua hivyo "
Ungeaandika;sijauliza nani amemuamulia...
"Kwa nini anaamua hivyo"
Ni kinyume na swali lako la msingi ambalo unahoji " mungu mwenye uwezo wote, Upendo wote na nguvu zote kwa nini hakuumba ulimwengu unaotaka wewe.
Kimsingi unahoji kwa nini hakutumia sifa zake kuumba ulimwengu uutakao wewe.
Maana ukiuliza kwamba "kwa nini anaamua hivyo" Mimi nitakujibu kwa sababu alitaka na sisi tushiriki uumbaji kwa kutumia changamoto zilizomo kwenye ulimwengu huu ambao ni kutokana na kazi yake njema kwa kutumia hekima na utashi aliotupa.
Sasa hapo hamna set theory sijui Kama utaelewa....
Nimeuliza kwa nini mungu kaamua hivi na si vile.
Nimejibiwa mungu anaamua tu.
Hence my quipping.
Ukinijibu mungu anaamua tu, hujajibu swali langu la kwa nini mungu kaamua.
Umejibu swali jingine, la nani kaamua, ambalo sijauliza.
Umejibu swali ambalo hujaulizwa, uliloulizwa hujajibu.
Sijahoji uumbaji wake kwa kutaka ulimwengu ninaoutaka mimi.
Nimehoji kwa nini uumbaji wake hauna logical consistency?
Huku ana uwezo wote na upendo wote, huku anaumba ulimwengu ambao maovu yanawezekana.
Kwa nini?
Mwenye uwezo na upendo wote haumbi ulimwengu ambao mabaya yanawezekana kwa viumbe wake.
Ulimwengu ungekuwa hauwezekani mabaya, ungekuwa logically consistent na mungu anayeweza yote na mwenye upendo wote.
Lakini kwa sababu ulimwengu unawezekana kuwa na mabaya, hauko logically consistent.
Kwa nini?
Doesn't the world contradict your god?