Ndiyo athari ya kukariri hiyo.
Kati yangu ninayetoa maswali kwa habari za mapokeo na kukariri vitabu vya dini, na wewe unayeshindwa kuyajibu maswali hayo nani anakariri?
ambayo inakupunguzia hadi uelewa wa mambo.
Kama kweli una uelewa wa mambo mbona maswali yangu hunijibu?
Wapi nilipotaja mitihani ya Mungu?au nioneshe neno lenye kuashilia hivyo?
Hata mfano wako mwenyewe huuelewi. Ukishatoa habari ya kufananisha matatizo ya maisha kuwa sawa na habari ya mtihani kwa mwanafunzi, umeshafananisha aliyeruhusu matatizo hayo na aliyeruhusu mtihani kwa wanafunzi.
Kwa wanafunzi mtihani unaletwa nawalimu wasio na uwezo wote wala ujuzi wote wala upendo wote, hivyo ukiuliza kwa nini wanaleta mitihani, wanaweza kusema wanataka kufundisha.
Huyo mungu anayeleta matatizo (sawasawa na mitihani) kashindwa vipi kufundisha viumbe vyake bila matatizo wakati ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?
Wewe haukubali kwamba Mungu ndiyo aliyeumba huu ulimwengu,
Nitakubali vipi kabla ya kunijibu swali langu?
Imekuwaje mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aende kuumba ulimwengu ambao unawezekanika kufanyika mabaya ya kila aina?
lakini unakuja kuhoji kwamba mbona Mungu kafanya hivi mara vile kwenye huu ulimwengu,ilitakiwa kwanza tuthibitishiane kuhusu upatikanaji wa huu ulimwengu maana huko ndiyo kiini cha haya yote.
Kiini cha yote ni uwepo wa mungu.
Uwepo wa mungu unaweza kupimwa kwa kuangalia nature yake mungu na kuilinganisha na dunia iliyopo.
Nature yake mungu ni mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na mwenye upendo wote.
Mungu kama huyu ana uwezo wa kuumba ulimwengu wowote, hata ulimwengu ambao mabaya hayawezekaniki.
Ulimwengu tunaouona mabaya yanawezekanika.
Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kiasi kwamba aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekaniki, kwa nini hakuumba ulimwengu huo na kaumba huu ambao mabaya yanawezekanika?
Hujajibu swali hili.