naifahamu sana Iringa,nimezaliwa hapo,nimeishi hapo na bado nitaendelea kuwa na Iringa moyoni mwangu,mkuu hebu piga picha tu pale maeneo ya miyomboni jinsi ilivyo,halafu uende hapo mashine tatu na jinsi barabara za iringa zilivyo nyembamba,sasa leo hii ukisema uruhusu wamachinga wafanye biashara kila mahali kweli tutaweza kupita iwe kwa miguu hata magari?stendi ya pale miyomboni magari yanapata tabu sana kupaki na kutoka kutokana na msongamano wa hao machinga.Mlandege sio mbali sana na katikati ya mji tena ni eneo ambalo halina msongamano wakienda kule watapata tu wateja,tatizo lililopo hapa ni mazoea na wala si vinginevyo.