kwanini wasingekaa kutafuta njia nzuri na muafaka wa kutatua tatizo la wafanyabiashara hawa,Mchungaji Msigwa una mamlaka gani ya kuamuru wamachinga kurudi kwenye maeneo ambayo yamekatazwa?Hivi ubunge ni kufanya kile unachojisikia na kinyume na taratibu na sheria tena ambazo wewe kama mbunge na diwani umeshiriki kuzitunga?.Polisi waache wafanye kazi yao na wala wasilaumiwe wa kulaumiwa hapa ni mchungaji msigwa kwa kuwa chanzo cha tatizo.
Ifike wakati lazima watanzania tuwe tunasapoti mambo ya msingi na si kushabikia kila jambo hata kama ni hatari kwa mustakabali wa taifa letu.Mimi na wewe tumekaa nyuma ya pc zetu na kuandika kila aina ya maneno wakati wale ambao tunawajaza ujinga wana taabika kwa kupigwa mabomu,wengine kufariki na hata wale wasio na makosa wanaingia katika adha hii.Wito wangu kwa Mbunge Msigwa aache kufanya mambo yeye kama kiongozi hapaswi kuyafanya,kuchochea watu kufanya vurugu huo si uongozi,kiongozi makini ni yule atakayeumiza kichwa kutafuta njia muafaka ya kuwajengea wananchi wake misingi ya kujikomboa kutoka katika lindi la umasikini.
Watu wanasifia humu kwamba wamachinga wanaelekea kuwashinda polisi,hivi hao polisi wakiona hali inakuwa mbaya si wataamua kutumia nguvu kubwa kudhibitihali hiyo?mwisho wa siku ikitokea watu/mtu kadhuriwa vibaya utasikia humuhumu kwenye jukwaa watu wakisema ooh polisi wanatumia nguvu kubwa,mara wametumwa...jamani tusiwe watu wa kupenda mambo ya ajabu.
Kwangu mimi madhara yoyote yatakayotokea Iringa leo mtun wa kwanza kumlaumu itakuwa Mchungaji Msigwa (Mb.Iringa Mjini)
(IRINGA MY DREAM LAND)