IRINGA: Vurugu, Machinga na Polisi wapambana

IRINGA: Vurugu, Machinga na Polisi wapambana

haki itashinda no matter how long it will take,for they say theways of truth are the ways of victory the ways of lies are the ways of defeating yourself.
 
Serikali yetu mbona hawasomi alama za nyakati!!!!!
Dodoma machinga hawajahama mjini na wanaendelea bila fujo, Dar machinga walitaka kuwahamisha maeneo ya tazara kongo na mwenge lakini yote yaligonga mwamba baada ya fujo kibao na baadae wakaona wajenge machinga complex ambayo nayo ilishindwa kuzaa matunda na machinga kuendelea maeneo ya mwanzo, Mwanza yale yale.
wanawahadaa machinga wa iringa tu kwa sasa NINACHOAMINI SUBIRI UCHAGUZI UKARIBIE UONE KAMA KUNA CHINGA ATAFUKUZWA.
Ni vyema viongozi wetu kufikiria kwa kina kabla ya kuanza kusema na kufanya hayo yanayoendelea.

yani wanalazimisha gari zote za abiria zipite machinga complex ,kibarabara hakitoshi,huko ni kulazimisha mambo marahisi. Kwanini machinga complex haikujengwa karume? Na kwanini wameshindwa kuwahamisha machinga pale karume waende machinga complex? Kwanini wameshindwa kuwaondoa kwenye mitaa ya k'koo? Serikali legelege, Rais dhaifu ,watendaji wake anawachagua kwa fadhira..
 
Tatizo wabunge wao wanapenda vurugu na umaarufu wa kijinga
 
Wanacho kifanya poliCCM hapo Iringa mjini, mie nachukulia poa tu, kwani wana tujengea chama chetu (CHADEMA) kwa kasi ya ajabu tena kwa gharama nafuu.

Hivi Iringa nayo imekuwa kasikazini ?
Kamanda tatizo mnanyanyaswa hivyo siku ya kampeni zikianza mkishapewa pilau na kofia mnasahau kila kitu, jifunzeni sasa.
 
kweli ccm inasaidia kuijenga cdm bila ya wao kujijua. Tuwaulize swali dogo tu: huko mlikopanga wamachinga waende kufanya biashara kuna miundo mbinu gani? kuna vyoo? kuna barabara ya uhakika na kunafika kwa urahisi? Mmeweka mikakati gani ya kulitangaza eneo hilo na kuwavuta wateja waende huko kama hatua za awali za kuwazoesha wananchi eneo jipya la biashara za wamachinga
 
Mungu atusaidie, alete tu BUSARA kwa viongozi wote wanaohusika na haya yote. Msiwasukume watu kuichukia serekali yao. Tunaipenda lakini hao vibaraka wa machafuko ndio wanaiingiza kwenye chuki na raia wake. Mmachinga ni mtu sio UCHAFU WA TAKA ukatupwe porini jamani wenzangu WATANANIA. Lukuvi Baba yetu, tutetee huko Bungeni. Unasikilizwaga.
 
kama walikowahamishia hakuna miundo mbinu,means no wateja,hawa vijana wanatafuta rizki yao wakale polisi?
 
Tatizo wabunge wao wanapenda vurugu na umaarufu wa kijinga
Umaarufu upi,hivi unaweza goma au andamana kwa kudai 1000 ili hali mfukoni una 50000,wamachinga wanadai kile wasichokuwa nacho,wangekuwa nacho wasingemsikiliza Msigwa kama ndio umaarufu...
 
Tatizo hawa ccm na serikali yake wanakaa na kufikiri kuwa watawazuiaje cdm,wanashindwa kufikiri watawasaidiaje wananchi waliotopea kwenye umasikini.NA TUNAOMBA UONGOZI WA CDM 2015 WASIMAMISHE MGOMBEA WA UBUNGE JIMBO LA ISIMANI.
 
Wangeweka mpango wa kuwaruhusu machinga kufanya biashara angalau mara moja kwa wiki yani kila jumapili. Kwani jumapili inakuwa sio siku ya kazi ivyo ni vizuri wakawa wanakuja mjini kufanya biashara zao halafu siku za kawaida wanarudi walipo kwa sasa. Duniani kote mfano Marekani, Uingereza wamachinga wanatambuliwa na hurusiwa hata mara mbili kwa wiki kufanya biashara zao kati kati ya miji. Lakini kwa Tanganyika ni tofauti wao badala ya kupanga mikakati ya kuwasaidia wanatumia nguvu. Wakati wa kutumia mabavu imepitwa na wakati, kinahotakiwa ni kukaa nao au hata kabla ya kukaa nao unapopanga mji wako panga ukijua kuwa kuna wafanyabiashara ndogo ndogo yaani machinga. Kwani leo mpaka wanawapiga mabomu walishindwa nini kuwatangazia kuwa kuanzia kesho hatuitaji kuwaona machinga eneo hili kungetokea yote hayo
 


May 19, 2013





[TABLE="align: center"]
[TR]
[TD] [/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Mbunge mchungaji Peter Msigwa[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="align: center"]
[TR]
[TD]
IMG_4649.JPG
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Polisi waliotoka kumkamata mbunge Msigwa leo[/TD]
[/TR]
[/TABLE]





[TABLE="align: center"]
[TR]
[TD="align: center"]
E84A4617.JPG
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]Gari ya mbunge Msigwa kabla ya kukamatwa leo kwa kuhusishwa na vurugu

..........................................................................................


Na Francis Godwin, Iringa
MASAA zaidi ya 6 ya mapambano kupiga mabomu ya machozi na kurushiana mawe kati ya wafanyabiashara ndogo ndogo (machinga ) na askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoani Iringa yaishia pabaya kwa jeshi la polisi kumkamata mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (chadema) na watu wengine zaidi ya 60




Polisi watumia mabom ya machozi kutawanya machinga wapiga mabomu hadi stendi kuu ya mabasi abiria walazimika kutimua mbinu na kuacha mizigo yao katika magari huku machinga hao wakitumia mawe na kuchoma mataili moto barabarani kuvunja vioo vya gari la Zimamoto na kuharibu mali mbali mbali kama njia ya kupambana na polisi
Tukio hilo la Mapambano kati ya machinga na polisi lilitokea leo kuanzia muda wa saa 3 asubuhi na kuendelea hadi saa 8 mchana katika eneo la Mashine tatu mjini Iringa na maeneo mbali mbali ya mji wa Iringa .


Mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com nawww.matukiodaima.com ambao ulikuwepo eneo la tukio toka saa 12 za asubuhi ya jana alishuhudia kundi kubwa la askari wa FFU wakiwa na gari la maji ya kuwasha ambao wakesha wakilinda eneo hilo .


Askari huo walilazimika kukesha wakilinda eneo hilo kufuatia kauli ya mbunge Msigwa aliyoendelea kuitoa katika mikutano yake ya hadhara mjini hapa kuwhamasisha machinga hao ambao Halmashauri ya Manispa ya Iringa iliwahamisha eneo hilo la mashine tatu na kuwapeleka eneo la Mlandege kabla ya mbunge Msigwa kuwahamasisha kurejea tena eneo hilo.


Kabla ya mbunge Msigwa kufika eneo hilo majira ya saa 3 asubuhi machinga hao ambao walikuwa wamejikusanya makundi madogo madogo bila kupanga biadhaa zao walisikika wakidai kumsubiri mbunge Msigwa kama alivyopata kuwaahidi kuwa atafika eneo hilo kuungana nao kwa kuwa machinga mpya .


Hata hivyo baada ya mbunge huyo kufika akiwa na gari lake la kibunge ambalo lilikuwa lilikokota tela la kuhifadhia mizigo alisimama eneo hilo na kuendeleza msimamo wake wa kuwataka machinga kupambana na baada ya muda alitoweka eneo hilo kabla ya polisi kuanza kuwatawanya machinga hao kwa mabomu ya machozi .


Wakizungumzia hali hiyo ambayo ni ya kwanza kutokea katika mji wa Iringa wakazi wa mji wa Iringa walisema kuwa mbunge na viongozi wengine wa serikali wanapaswa kulaumiwa kwa kushindwa kutumia njia nzuri ya kukutana kwa ajili ya kumaliza mvutano huo ambao unaendeshwa kisiasa zaidi.


Festo Sanga alisema kuwa hali ilipofikia ni mbaya zaidi na hivyo busara zinahitajika kwa ajili ya kutatua tatizo hilo ikiwa ni pamoja na kutazama eneo zuri kwa ajili ya machinga bila kuendelea kuonyeshana ubabe .


Sanga alisema kuwa machafuko yaliyojitokeza leo ni machafuko ambayo wakazi wa mji wa Iringa walikuwa wakishuhudia katika vyombo vya habari katika mikoa mingine ukiacha lile la Septemba 2 mwaka jana lililotokea kijiji cha Nyololo kati ya wafuasi wa Chadema na polisi na kupelekea kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Iringa marehemu Daud Mwangosi.


“Kweli katika hili mbunge wetu hapaswi kuendelea kulazimisha machinga kuvunja sheria ila anayo nafasi ya kukutana na viongozi wenzake ili kutafuta suluhu ya jambo hilo vinginevyo wanaoteseka na machinga na wale waliokamatwa kwa vurugu hizo ujue wengi waliopigwa mabomu ya machozi si machinga wengine walikuwa wasafiri na badhi yao walikuwa wakielekea makanisani ”


KUhusu kukamatwa kwa mbunge huyo na kuhojiwa na polisi juu ya vurugu hizo Sanga alisema kwa upande wake analipongeza jeshi la polisi kwa kutumia busara zaidi ya kumkamata mbunge kama mhusika mkuu na kuliomba jeshi la polisi kuwaachia wananchi waliokamatwa kwa vurugu hizo.


Huku Sarah Kalinga alidai kuwa chanazo cha machafuko hayo ni mvutano kati ya CCM na Chadema na kuwa ilipaswa vyama vyote viwili kukutana na kuwasaidia machinga badala ya kuwanyanyasa kwa kutumia nguvu kuwabana .


Hata hivyo alisema wao kama walalahoi wanampongeza mbunge wao kwa kuonyesha kuwapigania japo haungi mkono njia inayotumiwa na mbunge ya kuwahamasisha kuvunja sheria na kuwa matatizo na majeraha wanapata wao wananchi na sio mbunge.


Awali mbunge mchungaji Msigwa kabla ya kukamatawa na jeshi la polisi alitoweka katika mazingira tata katika eneo hilo la mashine tatu na kuibukia eneo la chuo kikuu cha Tumaini Iringa ambako kulikuwa na harambee ya kuchangia Kanisa na mgeni rasmi akiwa waziri mkuu mstafu Frederick Sumaye na mara baada ya shughuli hiyo kumalizika ndipo alipokamatwa na polisi na kufikishwa kituo cha polisi.


Kabla ya kukamatwa kwake mbunge Msigwa alizungumza na mwandishi wa habari hizi na kuwa yupo tayari kukamatwa wakati wowote na kuwa kamwe ataendelea na msimamo wake wa kuwataka Machinga kufanya biashara eneo hilo.


Mbali ya kukamatwa kwa mbunge Msigwa kwa kuhusishwa na vurugu hizo pia jeshi la polisi mkoani Iringa linawashikilia watu wengine zaidi ya 60 akiwemo aliyekuwa kampeni meneja wa Chadema jimbo la Iringa mjini na mgombea udiwani kata ya kwa Kilosa Abuu Changawa Majeck.


Huku idadi ya majeruhi waliojeruhiwa kwa kupigwa mawe na machinga na badhi ya machinga waliokamatwa kwa vurugu hizo pia wakijeruhiwa vibaya wakati wakipambana na polisi hao.


Taarifa kutoka jeshi la polisi zilizothibitishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda zinadai kuwa watu zaidi ya 60 ndio wamekamatwa hadi sasa na jitihada za kuwasaka wengine waliohusika katika vurugu hizo ambazo zimesababisha uharibifu mkubwa wa mali za wananchi unaendelea.


Huku akidai mali mbali mbali zimeharibiwa likiwemo gari hilo la zimamoto mjini Iringa pamoja na uharibifu mwingine mdogo mdogo wa mali za wananchi .


Jeshi hilo la polisi limesema kamwe halipo tayari kumwachia mbunge Msigwa kwa leo hadi hapo atakapofikishwa mahakamani Kesho


MWISHO

[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Imewekwa na Francis Godwin ni Iringa na matukio No comments: Links to this postEmail ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook




[TABLE="width: 100%"]
[TR]
[TD]UNAMAONI GANI ? [/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]




FFU KUTOKA MBEYA KUWASILI MJINI IRINGA WAKATI WOWOTE KUANZIA SASA ..............




IMG_4643.JPG

Habari ambazo zimetua hivi punde katika mtandao huu zinadai kuwa msafara wa askari wa FFU pamoja na gari la zimamoto kutoka jiji la Mbeya upo njiani kuja mjini Iringa kuongeza nguvu zaidi .



Imewekwa na Francis Godwin ni Iringa na matukio No comments: Links to this postEmail ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook




[TABLE="width: 100%"]
[TR]
[TD]UNAMAONI GANI ? [/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]





mbunge Msigwa (kulia)akizungumza na msaidizi wa askofu wa KKKT dayosisi ya Iringa
Mbunge Msigwa akisalimia katika harambee iliyoendeshwa na Sumaye leo katika chuo cha Tumaini Iringa

Watalii wakiogopa kuendelea na safari baada ya kutokea machafuko mjini Iringa

Jeshi la polisi mkoa wa Iringa limemkamata mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kufuatia kuhusishwa na vurugu za machinga eneo la mashine tatu hii leo

Hivi sasa mbunge huyo yupo katika kituo kikuu cha polisi mjini Iringa akihojiwa na polisi kufuatia vurugu hizo ambazo kwa sasa zimetulia na wananchi wameanza kuendelea na biashara zao.

Ulinzi makali waimarishwa eneo la kituo cha polisi huku wananchi wakiwa nje ya kituo hicho kuona kinachoendelea
habari kamili itakujia hivi punde................



Imewekwa na Francis Godwin ni Iringa na matukio No comments: Links to this postEmail ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook




[TABLE="width: 100%"]
[TR]
[TD]UNAMAONI GANI ? [/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]




BAADHI YA VIONGOZI NA WAFUSI WA CHADEMA 50 IRINGA WAKAMATWA



Hili ni eneo la National moto ukiwaka katikati ya barabara

Maeneo ya Makorongoni yakiwa yametanda moshi mzito
POlisi wakilinda barabara ya Iringa - Dodoma ambayo ilitekwa na wamachinga hao na kuchoma mataili barabarani

Wananchi wakiwa juu ya nyumba zao kushuhudia matukio



Hali bado yaendelea kwenda kombo katika Manispaa ya Iringa baada ya askari polisi kukamata watu zaidi ya 50 akiwemo aliyekuwa mgombea udiwani kata ya Kwakilosa na kampeni meneja wa Chadema jimbo la Iringa mjini Abuu Majeck

Hadi sasa biashara katika mji mzima zimesimama na polisi wameendelea kuweka sawa ulinzi katika mitaa mbali mbali .

Kwa sasa baadhi ya mitaa ya mji wa Iringa imetanda moshi uliotokana na mataili yaliyochomwa na machinga hao.

Taarifa za sasa kutoka jeshi la polisi ni kwamba mbunge wa jimbo hilo mchungaji Peter Msigwa (Chadema) ambae anadaiwa kuwa chanzo cha vurugu hizo anasakwa japo mtandao huu nusu saa iliyopita ulimshuhudia akiwa eneo la chuo cha Tumaini katika harambee inayoendeshwa na waziri mkuu wa zamani Mh. Sumaye .

Nipo njiani kuelekea Tumaini niliko mwacha mbunge Msigwa undani wa ukweli wa mambo utaupata hapa endelea kutembelea...



Askofu wa KKKT Dayosisi ya Iringa Dkt Mdegella ,waziri mkuu mstaafu Bw Sumaye na mkuu wa mkoa wa Iringa Dkt Ishengoma wakiwa katika harambee hiyo


MBUNGE MSIGWA ATINGA ENEO LA VURUGU ATOWEKA KIAINA






mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akiwasili eneo la vurugu kabla ya kuanza kwa vurugu hizo

Mbunge Msigwa akiondoka eneo la mashine tatu

Machinga wakisukuma gari ya mbunge Msigwa

Polisi wakimfuatilia mbunge Msigwa kwa nyuma baada ya kufika eneo hilo bila kufanya biashara kama alivyoahidi

Polisi wakianza kufukuza wananchi eneo hilo








Polisi wakipita eneo la Mashine tatu asubuhi hii

Abiria na wapiga debe stendi kuu wakinawa maji baada ya kupigwa mabomu na kumwagiwa maji ya kuwasha na askari wa FFU leo

Mmiliki wa mtandao huu mzee wa matukio daima akinawa maji baada ya kupigwa bomu la machozi



Hali ikiendelea kuwa tete kwa machinga kufunga barabara kuu ya Iringa Dodoma na ile ya mashine tatu

Ni Machafuko Iringa hivi leo
















Imewekwa na Francis Godwin ni Iringa na matukio
 
Big up Msigwa,hao vilaza wasikutishe muda sio mrefu watafata amri yako...
 
Nguvu mnayoitumia policcm kwa kupiga Wamachinga mngekuwa mnaitumia kuwakamata wanaoua Tembo kila siku nadhani Tanzania tungekuwa mbali kimaendeleo. Haya matokeo yake ninyi mnaangalia ile kauli ya ndio mkuu na kuendelea kupambana na Machinga. Hivi majimbo ya ccm hakuna Wamachinga mkawpige?
 
Sasa mbunge anakamatwa hovyo hovyo hivi?mbona sijawahi kusikia mbunge wa ccm amelala ndani sababu ya kutetea walala hoi?na lizaa ya sgika alipewa huyu kamuhanda?mbona thamani ya bunge inachezewa sana na mapolisi?imebaki nukta moja tupachimbe this time kwa kweli hapana
 
Back
Top Bottom