malivawan10
JF-Expert Member
- Nov 22, 2012
- 541
- 310
Mtoto mdogo kazimia'na mwandish wa habari apigwa na kukamatwa na polisi wakat anajulikana anaitwa alfhan
Wa kulaumiwa ni maccm
![]()
POLISI YATUMIA NGUVU KUTAWANYA WANANCHI MTAA WA MASHINE TATU, WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO MAARUFU KWA JINA LA MACHINGA WAKIWA NA MBUNGE WAO,
Wananchi wafunga Barabara na kuchoma mataili Barabalani Polisi nao wazidi kupiga mabomu huku wananchi wa kisema Pigeni yaishe tumechoshwa kunyanyaswa kwa sheria ya kuwadhibiti wadogo huku wakubwa wakikosea Sheria haipo.
Ni fujo, mamlaka husika zimeshatoa maelezo ni sehemu gani za kufanyia biashara na ni sehemu gani haziruhusiwi! Kwanini wewe upingane na mamlaka? Kuna taratibu za kupinga lakini siyo kwa stahili hii ya CDM na ya mchungaji koko wao!
mkuu nashukuru kusikia kuwa wewe ni mwana Iringa ila hujajibu hoja yangu.mvutno haujaanza leo na machinga mlandege walishakwenda wakadai hakuna biashara na ndio maana wamerudi mjini,sasa kwa nn wasikae chini kuona wapi ni sehemu sahii mlandege c mbali kweli ila kwa mtazamo wa kibiashara mlandege ni mbali mkuu tena sana.vp kuhusu kuwapeleka hapo mwembetogwa pana ugumu gani?unadhani kulikua na sababu ya kutumia mabomu leo kwa issue iliyokua toka jana inajilikana tukifanya hivi iatakua hivi?
Msigwa mnamwonea bure maana kilichofanyika na viongozi wenu ni sawa na mtu kuomba ushauri huku unae mwomba ushauri unamwambia sitaki unishauri hivi.uwezi kutana na viongozi wa machinga na Mbunge alafu unawambia mimi ndio nasema itakua hivi asiefata ataona cha mtemakuni sasa hapo unatafuta suluhu au unatumia ubabe?unajua kunawatu wanaishi na kusomesha kwa biashara izo?tujifunze kufuata ushauri na kusikiliza nguvu azito tusaidia na hii ali itafika hatua itazoeleka sasa hapo ndipo utaja sikia usio yategemea maana watu wakishakua sugu na haya matukio tegemea hawatarusha tena mawe ila watajifunza kujiami iwe kwa mabomu ya kitengeneza ama la!tusipuuze ujinga wa viongozi wa chache wasiotaka kushaurika kisa tutampa Msigwa umaarufu kwa kufata ushauri wake.tukumbke tukifata ushauri wake na tukafanikiwa sifa ni ya mkoa wote na si yeye pekee mkuu.