Wamachinga wanaondelewa je?
1. Je mazingira hayo wanayoambiwa waende yameandaliwa kibiashara?
2. Kama hayakuandaliwa vizuri, lengo ni kuwatoa tu mjini stand?
3. Na je mtawapiga mabomu na wateja waende huko?
4. Na kama hapatakuwa na biashara, hatima ya hao na maisha yao nini? Kwa sababu na uhakika wana familia na wanasomesha, wanalipa kodi za nyumba na vitu vingine kwa biashara hiyo.
5.Hamuoni mnawakosesha watu ajiri?
6. Je wakikosa ajira, mnataka mpambane nao kama majambazi kama sasa hivi mna pambana wakati wanafanya kazi halali hata kama kwa mazingira yasiyo ruhusiwa?
USHAURI WANGU NI KUWA MSIKURUPUKE KABLA YA KUTATHMINI KIPI KIKUBWA KATI YA FAIDA NA HASARA YA JAMBO.