IRINGA: Vurugu, Machinga na Polisi wapambana

IRINGA: Vurugu, Machinga na Polisi wapambana

Katikati ya mji kuna magari yakitangaza hali ya hatari. Kwenye eneo la tukio kuna moshi utadhani jiko la kuni. Mungu saidia damu isimwagike, pia maafa yasiwe makubwa.
 
Polisi waache kutumiwa na CCM kama condom . Wamachinga wana haki ya kufanya biashara hapo.

Acha umbumbumbu wewe, hakuna mwenye akili timamu ataafiki machinga kufanya biashara eneo hilo. Barabarani no way. Hizi siasa hizi zinatupeleka kusiko.
 
kwa nn majimbo yanayoongozwa na CHADEMA mabomu ni kitu cha kawaida? kuna siku majimbo ya CHADEMA tutaandamana kwa pamoja tuone kama hawa polisi wataweza kudhibiti hali ya maandamano kwani naamini kuwa polisi ni wachache mno nchi hii.
 
Kutoka Iringa vurugu kubwa muda huu, Polisi wapiga mabomu ya machozi kutawanya machinga. Hii ni kufuatia machinga kurudi kwenye maeneo yaliyokatazwa kufanyia biashara.

Hii imetokana na Machinga kuruhusiwa na mbunge wao Mchg Msigwa ambaye pia alikuwepo eneo hilo na Machinga kusukuma gari lake.


Sasa ulitaka waende wapi? Hukumsikia ahat Dr.Abdallah Kigoda akisema wamachinga waachwe wafanye biashara zao
Mnakuaga dunia ipi na ninyi????
 
Hivi hata hilo halizungumziki mpaka watu wapambane?
1.Hakuna ubaya wa kuwa na Eneo zuri la kufanya biashara,lakini
2.Serikali iweke miundombinu ya kutosha kama vyoo
3.Kituo cha Dala dala kihamishiwe karibu na hilo soko jipya,
Hivi ukitaka kuanzisha biashara si lazima uanzishe sehemu yenye wateja?hii haihitaji hata degree kufikiria suala hili.
Magamba wanatafuta mwanya wa kupata kodi za nyumba za mwezi wa sita kwa kuunda Tume ya Kuja kuhesabia marehemu watakaokufa leo!
 
Nyumba inawaka moto mwenye nyumba kalala watoto wanahangaika bila msaada.
 
Tanesco wamezima umeme baada ya mlipuko kuanza kuunguza nyumba za wakazi,
hali bado si shwari, watu wanaonekana kukatiza m1 m1 hasa eneo la makorongoni na stend kuu
 
Leo ni jumapili, nilikuwa nategemea huyo mchungaji awe kanisani sasa hivi!! Lakini matokeo yake yupo busy kuhatarisha usalama na amani ya nchi.

Poor mchungaji, poor chadema!!
 
Nimesikia radio maria muda sio mrefu,wanasema police wanawamwagia maji ya kuwasha hata wazee na watoto waliotoka kanisani.Najua hapo yupo kamuhanda hakuna busara itakayotumika,ukizingatia majuzi alisifiwa bungeni na lukuvi kwa 'kazi'nzuri anayoifanya.
 
Barabara kama ya mashine tatu imefungwa, mawe yanarushwa kuelekea gari la polisi eneo la barabara ya uhuru.
 
Kwani Iringa pana nini hasa! Mbona Dar hawa watanzania wenzetu wameruhusiwa kutafuta riziki; na hivi sasa wanauza bidhaa zao mpaka lango la Magogoni; au macho yangu niwapo Dar yanakuwa na makengeza!
Pana jengo la 10bln nasema TShs 10bln; lakini halitumiki na vijana wanatafuta riziki ktk ya jiji mpaka kwenye koridal za wizara. Huko Iringa vipi? Njooni Dar ziara ya mafunzo; weka bajeti ya TShs 150mln; mje kujifunza jinsi ya kuishi na watz wanaofanya biashara ndogo ndogo. Napendekeza ndani ya wanatakiwa kuja kwenye hiyo ziara wawe ni madiwan; RPC; mkuu wa mkoa na mkuu wa Wilaya.
 
Hapo busara itumike..kutumia maguvu hatima yake si nzuri pande zote. Me nadhani hata polisi wadogo ni kama wanawekwa chambo tu kuhatarisha usalama na uhai wao
 
Back
Top Bottom