IRINGA: Vurugu, Machinga na Polisi wapambana

IRINGA: Vurugu, Machinga na Polisi wapambana

Sasa ulitaka waende wapi? Hukumsikia ahat Dr.Abdallah Kigoda akisema wamachinga waachwe wafanye biashara zao
Mnakuaga dunia ipi na ninyi????
Unamuuliza nani swali hili? Au ndio ugeni na JF?
 
Machinga wanataka barabara zifungwe wao wafanye biashara katika barabara hizo na mbunge msigwa anasuport hili, je sheria inaruhusu kufunga barabara kwa ajili ya wamachinga kufanya biashara?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mkuu wa wilaya anasema kua wamachinga waendelee kukaa eneo la mlandege ambako wamekaa huko kwa zaidi ya miezi 6, pia anasema Msigwa hakua na kibali, mtangazaji anaongeza kusema kua watu watakaokamatwa wasimlaum mtu kwa kua hawakua sahihi.
 
Kwahiyo kuwaambia watu wafanye biashara hapo mpaka watakapo wekewa mazingira mazuri ya biashara wanapowahamishia,hizo ni fujo!?umefelili.
Ni fujo, mamlaka husika zimeshatoa maelezo ni sehemu gani za kufanyia biashara na ni sehemu gani haziruhusiwi! Kwanini wewe upingane na mamlaka? Kuna taratibu za kupinga lakini siyo kwa stahili hii ya CDM na ya mchungaji koko wao!
 
Back to the topic,
maeneo ya stend kuu hali si shwari mabomu yameanza tena, vurugu zinaendelea, vijana wanakamatwa na kupigwa, barabara zimefungwa tena.
 
Kwa yule ambae hajui MABOSO ni nini? Atajua huyu jamaa ana akili ya namna gani... Teh teh..nimekubali kuwA jina huakisi matendo sometimes.....shule za mulugo in action nowwwww
Maboso ni mapovu yanayotokana na ulanzi...ambayo kwa kawaida huwa ni uvundo unaobaki kwenye mianzi hasa asubuhi na huwa ni chakula cha nzi na nyuki. Kule Iringa ni kitu maarufu sana
 
Kuna kijana aitwae Edward alikua anafunga duka lake kutokana na vurugu lakini ghafla amekamatwa na ffu
 
SUGU nenda kwa msigwa ukaongee na vijana tafadhali.yale ya mbeya uliyaweza nenda kwa msigwa tafadhali
 
hivi watanzania mnafikiri kuishi kufanya shughuli bila utaratibu ndiyo kutenda haki?
Hivi kuuza bidhaa katikati ya barabara ndo haki tunayopigania?
Hatufiiiiiiiki!

wewe ndio unaema hivyo hujui lolote,waziri wako Abdalah Kigoda anawatambua inaonyesha ni jinsi gani uelewa wako ni mdogo.Usipende kukaririii....
 
Maeneo ya stend kuu hakuna gari linaloingia wala kutoka, maduka yote yamefungwa, abiria walioko kwenye magari wamejawa na taharuki.
 
Gari la zima moto limeshambuliwa sana kwa mawe eneo la hall fare, gar la polisi limebondwa sana, matairi yamewashwa barabarani
Huo sasa ni ujuha, sasa gari la zimamoto linahusika vipi na matatizo yao? Saa hizi wanaliponda, halafu baadaye moto unaunguza mali zao na wanaanza kulitafuta tena kwa ajili ya kuzima moto. Wehu huu jamani!
 
hapa moshi wamachingwa wamejipanga mbele ya kituo kikuu cha policy kwa raha zao
 
Mbunge wa Iringa mjini Mch Msigwa amekatwa na Polisi

Hili jeshi la polisi inapotokea majambazi wamevamia eneo hawaji kwa haraka, kwa mfano mwezi uliopita kuna mwanamke aliuawa maeneo ya kariakoo Dar, lakn polisi hawakuja kwa wakati muafaka, ila cha kushangaza leo wananchi wamekaa kujitaftia riziki yao ndo wanakuja kulipua mabomu na kutesa raia.
 
Huo sasa ni ujuha, sasa gari la zimamoto linahusika vipi na matatizo yao? Saa hizi wanaliponda, halafu baadaye moto unaunguza mali zao na wanaanza kulitafuta tena kwa ajili ya kuzima moto. Wehu huu jamani!

Maoni yako yamefika kunakohusika.
 
Back
Top Bottom