IPP punguzeni udini

IPP punguzeni udini

Status
Not open for further replies.
Vp NSSF ya Balozi Dau, shirika la umma ilikuwaje pale?! Itakuwa IPP ya Dr. Mengi?
 
Misimu ya krismass ofa za matangazo msimu wa sikukuu za krismass ni tofauti na Eid hivyo tofauti zinaonekana, vipindi vya nyimbo za injili vipo tofauti zinaonekana hakuna vipindi vya kaswida, Fatma Almasi alipokuwa ITV alikuwa havai hijabu sasa anavaa tofauti hiyo.
 
Na wakienda hvy au tukienda hvy kuna Dini itaathi`ka sana

Maana serikalini wakristo makampuni binafsi Waislam

Alisha liongelea sana ilunga enzi za uhai wake
 
Najua wengi mnafahamu hizi kampuni zinazosimamiwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Dr. Mengi, hii kampuni kwa waislam na wasabato kupata kazi ni vigumu sana iwe hata kazi ndogo ndogo. Imefikia hatua hata ukipata kwa bahati mbaya kama ni binti wa kiislam haurusiwi kuvaa ushungi.

Kumbukeni vituo na magezeti yenu wateja wake ni wa dini zote
Bhakhesa kila kiwanda chake,vituo vyake vya biashara vina misikiti,tena hataki kabisa makafili kufanya kazi kwake,ukifanya kazi kwa Azam group hutakiwi hata kuvaa msalaba au rozali
 
Nendeni kwa bakhresa mbona masikia nae wakristo hawapewi nafas
 
Hata alipoona jina la Tido Muhando, Charles, Ivona Kamuntu, Suzan na wengine pia aliwakosesha kazi, tena kibaya zaidi akawapa kazi za utawala wa juu... mna matatizo sana ndugu zetu wa upande wa kushoto (Shimali). Mlilalamika sana kuhusu Dau na udini pale NSSF mkafanya mpaka na statistics kujua waislam wangapi na wakirisito wangapi ! MATOKEO MPAKA LEO MMEYAKALIA mligundua nini kwani mpaka MSIYATOE TUONE MALALAMIKO YENU?

Ukienda BOT, CRDB IPP NA SEHEMU LUKUKI wenzetu wapo wengi, lakini wakizidi waislam kwenye kampuni fulani basi imekuwa wadini KWANI MNA NINI ENYI WAKIRISITO WA NCHI HII? hamuoni kwengine kukijaza wakirisito ila waislam wakijaa sehemu basi ni udini MNATAKA WAISLAM WAENDE WAPI NYIE VIUMBE !!!! HII NCHI NI YETU SOTE !!!!
hiyo ya dau ni ukweli bila chenga coz tuna ushahidi watu hawajasoma walipewa michongo na ndio maana palikuwa bweleleee
 
Najua wengi mnafahamu hizi kampuni zinazosimamiwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Dr. Mengi, hii kampuni kwa waislam na wasabato kupata kazi ni vigumu sana iwe hata kazi ndogo ndogo. Imefikia hatua hata ukipata kwa bahati mbaya kama ni binti wa kiislam haurusiwi kuvaa ushungi.

Kumbukeni vituo na magezeti yenu wateja wake ni wa dini zote
Lete copy ya mambo yako ya kazi ambatanisha vyeti vyako na CV J3 asubuhi tuvione. Kama kweli ulistahili na ukanyimwa kazi. Acheni kuzusha mambo
 
Hakuna habari nisizo zipenda JF kama za migongano ya kidini. Hili ni bomu la akiba la wazungu ambalo wamelitegesha kwetu. Siku wakitaka kutulipua watakachofanya ni kumtengeneza mtu akaenda kilipua ama nyumba ya ibada au rasilimali ya dini yoyote halafu inaundwa mitandao na inatangazwa kwa nguvu sana kua huyo kafanya hivyo kwa kua anaichukia dini husika. Kitakachofuata ni wafuasi wa dini iliyoshambuliwa kulipiza kisasi kwa maneno na vitendo. Mungu atunusuru

Kuja kwa thread hizi, ile ya alexielias kuhusu udini kwenye kampuni ya Bakhresa na hii ya byembalilwa kuhusu udini IPP ni mifano halisi na naona ni mkakati wa kuwamisha watu kutoka kwenye ajenda flani sijui ya tarehe ngapi mwezi wa nne(japo siiungi mkono) waanze kushambuliana wenyewe kwa wenyewe, na kupitia dini mkakati utafanikiwa
usiwasingizie wazungu mambo haya yapo bila chenga kama huyaoni basi wewe ni kipofu mwasese
 
Acha uzwazwa mbona waislamu wamewahi kuwepo na bado wapo wengi, mfano:
Abdalah Mwaipaya.
Fardiha Midhley(sina uhakika na spelling)
Aboubakar Sadick.
Faroouk Mohammed Kareem.
Maulid Kitenge.
 
Kila mtu akiamua atoe lake la rohoni hakuna atakaebaki salama , cha msingi ni kuvumiliana tu na maisha yaendelee , ukisema kampuni hii waislamu wengi , ni lazima ukumbuke kuna kampuni nyingine ina Wakristo wengi , ukisema sekta hii wamejaa kabila A , kuna sehemu utakuta wamejaa kabila B n.k , na hizi changamoto zinaanzia kwenye Private sector mpaka Public sector , lililobaki ni kuvumiliana tu , kila mtu anajua kama kaajiriwa sehemu anajua ameajiriwa kwa vigwzo vipi , kama ni competence yake , amechukuliwa kwasababu ya kabila lake , au dini yake hilo ni juu yake cha msingi aitetee nafasi aliyopewa , vinginevyo umma utamnyooshea kidole na ataonekana kama alipo anastahili au la , shukrani!
Kweli mkuu, Tuvumiliane
 
Kwanini wakristo wengi wakiona taasisi ina waislam wengi wanalalama sana lakini sijawahi kuona waislam wakilalamikia taasisi zenye wakristo wengi, kama CRDB, IPP, TMAA, TANESCO, na nyingine nyingi. Anzeni kufanya tafiti muone nani wanapaswa kulalamika.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom