Ipo siku mtaukumbuka huu uzi

Ipo siku mtaukumbuka huu uzi

"Jipeni moyo msichoke, ipo siku mtakuja kukomenti kwa furaha kwenye huu Uzi, hakuna jambo lisilo na mwisho, mark my words....". Mwisho wake utafika tu.

Hatujawahi kuishi maisha ya ajabu kama haya, mambo kama haya huwa tunayasikia somalia mwisho wake utafika tu ipo siku tu.

Pablo Blanco
Afte 4 years
 
Yaani huyu wanayemburuta kwenye hili lisanduku la mbao he once thought he is everything under the sun.. Alikuwa anaamrisha watu wauwawe na wanauwawa.. Watu wafungwe na wanafungwa.. Watu waporwe mali na wanaporwa..

Sasa hivi yuko wapi? MEKO habareeee ndugu yangu tena eeeh
FB_IMG_1616231221709.jpeg
 
Yaani huyu wanayemburuta kwenye hili lisanduku la mbao he once thought he is everything under the sun.. Alikuwa anaamrisha watu wauwawe na wanauwawa.. Watu wafungwe na wanafungwa.. Watu waporwe mali na wanaporwa..

Sasa hivi yuko wapi? MEKO habareeee ndugu yangu tena eeehView attachment 1729976
Hapo mwisho hapo
 
JPM, Chuma, Jiwe Kwelikweli. Hivyo ndivyo alivyopenda kujiita. Kuna wakati alilala juu ya mawe kuthibitisha kuwa ni kweli yeye ni JIWE KWELIKWELI. Hatupo naye tena.

Katika Uchaguzi wa mwaka jana alitumia mbinu zote kuhakikisha anarudi madarakani kwa kura za kutosha ambazo ni zaidi ya asilimia 80+. Aliiba kura akisadiana na wasaidizi wake husani Tume ya Uchaguzi, vyombo vya ulinzi na usalama na baadhi ya makada wa CCM. Kuna watu walikufa, walipigwa risasi, kuna watu ni vilema hadi leo ili tu mwamba aingie madarakani.

Wabunge zaidi ya asilimia 90 ni wana CCM. Baada tu ya kuapishwa wabunge hawa, Wabunge wengi wa CCM walianza kumpigia chepuo kuwa wabadilishe katiba ili aendelee kutawala kwa kile walicho kieleza kuwa amefanya mambo mengi na makubwa. Wengine wakasema ulikuwa ni mwanzo tu wa kubadilisha katiba ili atawale milele.

Lahaula, Mungu wetu hapangiwi. Damu zilizo mwagika hulia, na Mungu hujibu kwa wakati.

Katika utawala wake wateule wake walitishia watu risasi mchana kweupe, wengine walivamia vituo vya runinga na bunduki huku rais akiwaambia majangili hao wachape kazi na WASITISHWE.

Watu hatukuruhusiwa kuzungumza na kumkosoa mkuu, waliojaribu kuwa wakaidi watekwa na kupotezwa, miili kadhaa iliokotwa kwenye sandarusi jirani na Coco Beach, Simon Kanguye, Ben Sanane hawajulikani waliopo. Rais hakujali hata kidogo. Vyombo vya habari viliambiwa na mwamba visidhani vina fridomu ya namna hiyo, VIKAUFYATA MKIA.

Mitandao ya kijamii nayo ikapigwa pingu kwa kutungiwa sheria za makosa ya mitandaoni. Hata tulipojua mkuu anaumwa na kujaribu kusema kupitia mitandaoni ya kijamii, tuliambulia kuambiwa kuwa ni uzushi na tunahatarisha amani. Wengi wapo Korokoroni hadi sasa kwa kosa la kumuulizia rais Magufuli na kuandika kuwa huenda alikuwa anaumwa.

Tuseme nini basi?? Tumshukuru Mungu wa Mbinguni na tusherekee maisha yake hapa duniani huku tukiyasema mema aliyo lifanyia taifa hili na tukisema kwa nguvu zote mabaya yote aliyotutendea ili waliopo madarakani wasije kurudia tena mabaya aliyo yafanya.

Ameandika Kumbusho Dawson
 
Hawa jamaa wamefurahi sana, walimtukana magufuli kuwa ni mshamba aliyechanganyikiwa.karne ya 21 mtu unaendekeza ukabila na ukanda.sasa kama sio ushamba ni nini??huyu jamaa kasababisha wasukuma waonekane watu wa ajabu
tapatalk_1616243741631.jpeg
 
Nilikuwa naangalia video ya dereva wa tundu lissu akielezea tukio zima la kupigwa risasi.hahaaaaa NAKUSHUKURU SANA MUNGU TUNDULISSU AMEPONA
 
mapema tu magufuli hata hajazikwa tayari nchi ishapata rais.kanyaga twende mama samia magufuli tupilia kule ndege zote tunazipiga mnada uwanja wa chato tunawapa wasukuma wafugie ngo'mbe
Eti wanasema pengo halita zibika wakati Samia kasha apa masaa kadhaa baada ya tangazo la msiba
 
Hii dunia tusipuuze magumu wanayopitia wenzetu, bora uishi vizuri, duniani tunapita tu.
 
Kupitia kifo Cha jiwe ndio nimeamini watz sisi Ni watu wanafki Sana tena Sana ,watu walikuwa wanaomba usiku na mchana jiwe aliwe kichwa kwa kutesa Sana wananchi wake hasa wa chini ,Leo hii maombi yametiki mijitu huko istagram et inasikitika mingine had inajirekod inalia .
Binafsi huu msiba nimeuchukulia kawaida Sana Kama ambavyo naichukulia misiba mingine
Usiwaze kabisa kuhusu mitandao mkuu ukweli uko mioyoni mwetu ungeona nnavosikitika hadharani ungesema nimefiwa na baba yangu hahahahaaaa Watz unafki ni kipaji chetu madhubuti kabisaa
 
Back
Top Bottom