IPI simu yenye camera nzuri kuliko zote?

IPI simu yenye camera nzuri kuliko zote?

Megapixels sio kila kitu kwenye kamera ya simu mkuu. Leo hii tunaangalia ubunifu/teknolojia iliyotumika kwenye camera unit nzima.
Mfano kama P20 Pro ilivyo'intergrate AI kwenye photo processing na kutumia Leica tech.
Hayo sio mimi nasema ni wao haohao wanaotengeneza hizo simu
 
Hapo ndio huwa nachoka, hivi ili picha iwe nzuri inatakiwa itoke na muonekano upi, coz kila siku tunaambiwa hii ndio inatoa picha bora ina maana bado hatujafikia ktk quality ya asilimia mia? Tuko asilimia ngapi kwa sasa?
 
Hii nayo ndo kampuni gan tena ya cm inauzwaje
Nashukuru umeuliza. One Plus 6 ni smartphone iliyotengenezwa na Kampuni ya One Plus toka China. Kama kampuni ilizinduliwa mwaka 2013.

Sifa mojawapo iliyoitenga kampuni ya One Plus ni kwamba imekuwa ikitoa simu zenye specifications kubwa (high-end premium devices) kwa bei nafuu zaidi kuliko washindani au makampuni mengine ya simu. Kutokana na style yao hiyo walijipatia jina la "the Flagship Killer".

Ni moja kati ya brand za simu bora zaidi na isiyojulikana na watanzania wengi kwa jinsi wengi wetu tulivyozoea simu ni either iPhone, Samsung, HTC, Motorola, Sony, Tecno, Itel, Xtigi, n.k.

Lakini kuna simu nyingi tu toka China ambazo zinafanya vyema kuliko hata hizo tulizozoea. One Plus ikiwa kinara katika hilo (kwani hata kwenye benchmark tests za karibuni imeshika nafasi ya juu kuliko hata Samsung Galaxy S9+.
Simu zingine kali ni kama Xiaomi, ZTE, Oppo, Razor (hii ni tip gaming phone).
 
Leo nimemfunika hadi Chief-Mkwawa kwa kutaja simu kali!
InShot_20180920_174739166.jpeg
 
Hapo ndio huwa nachoka, hivi ili picha iwe nzuri inatakiwa itoke na muonekano upi, coz kila siku tunaambiwa hii ndio inatoa picha bora ina maana bado hatujafikia ktk quality ya asilimia mia? Tuko asilimia ngapi kwa sasa?
Kwa jinsi teknolojia inavyozidi kukua hakuna kipimo cha mwisho wa uvumbuzi kwa kila kitu kitachoguswa na teknolojia.

Hivyo hata kwenye kamera za simu ni hivyo hivyo. Mwaka huu P20 Pro ndio kashikilia Namba moja kwenye Kipengele hicho. Lakini nakuhakikishia hata Huawei mwenyewe hajabweteka kwa hilo, tunavyotype hapa, team yake ya Utafiti na Maendeleo iko kazini kujua ni namna gani itaweza endelea kukamata usukani. Na hivyo hivyo makampuni mengine.
 
Back
Top Bottom