Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa humu jamiiforums.
Ndugu zangu watanzania;
UTANGULIZI
=====
Ndugu zangu, umasikini ni kitu kibaya sana. Umasikini unakatisha uhai wa watu wengi wangali wadogo sana kwa sababu tu wameshindwa kumudu gharama za matibabu.
Umasikini ndio chanzo cha matukio mengi sana ya uhalifu kama vile udokoaji, ulevi wa kupindukia wa pombe haramu kama vile gongo pamoja na ubakaji.
Ikitokea umejikuta umezaliwa katika familia ya kimasikini, ridhika kwa hali hiyo uliyonayo kwa wakati huo kisha pambana kujikwamua. Kama wewe ni mfanyakazi, basi fanya kazi zako kwa moyo mmoja, akili pamoja na nguvu zote.
Fanya kazi usiku na mchana kama inawezekana huku ukijua fika kwamba maamuzi yako ya leo ndio matokeo ya kesho. Kama ni mwanafunzi soma sana kwa maana elimu ndio mkombozi wako. Mimi huwa ninapenda kuwaambia watoto wa mama yangu mdogo kwamba "Elimu ndio mumeo wa kwanza"
MADA KUU
=====
Ipi ni njia sahihi ya kugawa mali/vitu vyako vya zamani kwa ndugu, jamaa au rafiki? Unasubiri akuombe kwanza au wewe ndiye unayeanza kumpa?
Jenga picha mimi nilikuwa mwembamba mwaka jana 2019 ila mwaka huu kutokana na mapishi moto moto ya wifi/shemeji yenu Bushmamy (I am joking) basi kitambi kikaja. Zile nguo zangu zote zilizokuwa zinapwaya mwaka jana, mwaka huu zote zinanibana kuanzia Jersey zangu za chama la wana MAN UTD pamoja na YANGA.
TATIZO LINAANZIA HAPA
===
Ukiwa na kitu chako cha zamani kisha ukataka kumpa ndugu, jamaa au rafiki utakutana na maneno haya: "Umeniona mimi ndio masikini sana wa kunipa vitu vilivyochakaa?
Ukiwa na vitu vyako vya zamani na ukaamua kiviweka ndani kwa kuogopa kuwapa watu vitu vilivyokwisha utakutana na kadhia hii: "Mbona unarundika sana vitu vya zamani, kwani hauna ndugu uwape?"
SWALI LA MSINGI: Ipi ni njia sahihi ya kugawa mali/vitu vyako vya zamani kwa ndugu, jamaa au rafiki? Unasubiri akuombe kwanza au wewe ndiye unayeanza kumpa?
Hii story sasa imekamilika na ipo kule JAMII INTELLIGENCE: Kulikuwa na dada mmoja mrembo sana "Female Assassin" wa idara ya ujasusi ya Soviet Union almaarufu kama KGB aliwahi kuficha risasi mbili ndani ya uuke wake alipoenda kumuua mfanyabiashara mmoja maarufu sana katika hotelini huko jijini Minsk mji mkuu wa nchi ya Belarus. Mfanyabiashara huyo alikuwa amepishana kauli na serikali ya USSR mwaka 1979.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Ndugu zangu watanzania;
UTANGULIZI
=====
Ndugu zangu, umasikini ni kitu kibaya sana. Umasikini unakatisha uhai wa watu wengi wangali wadogo sana kwa sababu tu wameshindwa kumudu gharama za matibabu.
Umasikini ndio chanzo cha matukio mengi sana ya uhalifu kama vile udokoaji, ulevi wa kupindukia wa pombe haramu kama vile gongo pamoja na ubakaji.
Ikitokea umejikuta umezaliwa katika familia ya kimasikini, ridhika kwa hali hiyo uliyonayo kwa wakati huo kisha pambana kujikwamua. Kama wewe ni mfanyakazi, basi fanya kazi zako kwa moyo mmoja, akili pamoja na nguvu zote.
Fanya kazi usiku na mchana kama inawezekana huku ukijua fika kwamba maamuzi yako ya leo ndio matokeo ya kesho. Kama ni mwanafunzi soma sana kwa maana elimu ndio mkombozi wako. Mimi huwa ninapenda kuwaambia watoto wa mama yangu mdogo kwamba "Elimu ndio mumeo wa kwanza"
MADA KUU
=====
Ipi ni njia sahihi ya kugawa mali/vitu vyako vya zamani kwa ndugu, jamaa au rafiki? Unasubiri akuombe kwanza au wewe ndiye unayeanza kumpa?
Jenga picha mimi nilikuwa mwembamba mwaka jana 2019 ila mwaka huu kutokana na mapishi moto moto ya wifi/shemeji yenu Bushmamy (I am joking) basi kitambi kikaja. Zile nguo zangu zote zilizokuwa zinapwaya mwaka jana, mwaka huu zote zinanibana kuanzia Jersey zangu za chama la wana MAN UTD pamoja na YANGA.
TATIZO LINAANZIA HAPA
===
Ukiwa na kitu chako cha zamani kisha ukataka kumpa ndugu, jamaa au rafiki utakutana na maneno haya: "Umeniona mimi ndio masikini sana wa kunipa vitu vilivyochakaa?
Ukiwa na vitu vyako vya zamani na ukaamua kiviweka ndani kwa kuogopa kuwapa watu vitu vilivyokwisha utakutana na kadhia hii: "Mbona unarundika sana vitu vya zamani, kwani hauna ndugu uwape?"
SWALI LA MSINGI: Ipi ni njia sahihi ya kugawa mali/vitu vyako vya zamani kwa ndugu, jamaa au rafiki? Unasubiri akuombe kwanza au wewe ndiye unayeanza kumpa?
Hii story sasa imekamilika na ipo kule JAMII INTELLIGENCE: Kulikuwa na dada mmoja mrembo sana "Female Assassin" wa idara ya ujasusi ya Soviet Union almaarufu kama KGB aliwahi kuficha risasi mbili ndani ya uuke wake alipoenda kumuua mfanyabiashara mmoja maarufu sana katika hotelini huko jijini Minsk mji mkuu wa nchi ya Belarus. Mfanyabiashara huyo alikuwa amepishana kauli na serikali ya USSR mwaka 1979.
USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.