Mkuu mimi ninawafahamu kiasi fulani hawa jamaa wanaotoa huduma ya umeme unaojulikana kama M-power. Kampuni inaitwa Offgrid Electric na makao yao makuu yako Arusha. Huduma zao naona zinapatikana katika baadhi tu ya mikoa na naweza kusema kwamba hawajawekeza sana katika kujitangaza zaidi kibiashara kama ambavyo pengine ilistahili kuwa. Kimsingi m-power hawana tofauti kubwa na pale mtu anapokwenda kununua vifaa vya solar dukani kama panels, inverter, battery, lights n.k ambapo vifaa kama hivi ubaki kuwa mali ya mteja wakati kwenye m-power vifaa vyote ubaki chini ya umiliki wa kampuni inayotoa hiyo huduma. Kampuni ufunga wenyewe vifaa husika kwenye nyumba baada ya mteja kulipa malipo kidogo (around Tshs 25,000/= as initial cost) kwa ile package ndogo ya taa tatu (bulb) na pia inayokuwezesha kuchaji simu (kama simu mbili hivi). Kwenye huduma hii kuna package kama tatu au nne hivi hivyo mteja uchagua package kulingana na mahitaji yake na pia uwezo wa kulipia kila mwezi. Kwa vile vifaa ubaki chini ya umiliki wa kampuni pale inapotokea tatizo kwenye vifaa basi kampuni ufanya utaratibu wa kuvibadilisha na kuweka vipya. Malipo ya huduma ufanyika kila mwezi na kwa njia ya simu kama ilivyo kwenye kulipia malipo kama Dstv, luku, star times n.k. Namba zao za simu kwa ajili ya customer care ambazo mteja ukipiga hauchajiwi chochote ni 0800752222. Pia kwa yeyote anaehitaji kufanya nao mawasiliano anaweza kuwaandikia kwa e-mail hii: info@offgrid-electric.com au kuangalia website yao ambayo ni www.offgrid-electric.com. Pengine kabla ya kuamua kutumia huduma hii ni vizuri mteja ajiulize faida na hasara za kununua kifaa kikawa chako moja kwa moja au kukodi kifaa hicho (Buy or Lease).
niliweka wa taa tatu.na kuna chaja pia kinachofurahisha umeme wao pamoja na kuwa wa soral ni mzuri haukatiki hauna usumbufu.ila tatizo lipo kwenye gharama.kwa mfano huo wa taa 3 ni 24000/= yaani 12000 ya kufungiwa na 12000 ya malipo ya mwezi tatizo lipo kwenye gharama ya 12000 mi naona ni kubwa sana wangefanya angalau elfu 5 hivi kwa mwezi ingekuwa vyema zaidi.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.