INTELIJENSIA: Ziara ya Waziri Mkuu Bandarini

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,593
29,711
Tuliangalie hili kwa makini sana. Jana wakati Waziri Mkuu akiwa anatembelea kukagua Kurasini Oil Jet (KOJ) aliambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala wa Vipimo (WMA) pamoja na wakubwa wengine. Swali alilomuuliza huku akitaka maelezo yake yatolewe ni ......KWA NINI ULIAMUA KUWASHA METER JANA BAADA YA KUTUMIWA UJUMBE WA SMS?......
.....“Nataka unieleze ni kwa nini ulitoa maelekezo ya kufunga mita hizo, na kwa nini jana uliamua kubadili uamuzi huo? Ni kwa nini umeamua kuchukua maamuzi haya baada ya kupokea ujumbe wa simu ya mkononi (sms) wakati mita zimekaa bila kufanya kazi kwa miaka mitano? Ni kwa nini umeamua kufanyia kazi ujumbe wa sms wakati unajua Serikali inafanya kazi kwa maandishi rasmi?” alisema Waziri Mkuu.....
Kwa jicho la weledi ni kwamba katika timu ya watakatifu waliowazunguka Majaliwa na JPM wapo wanaouza taarifa kwa watuhumiwa watarajiwa.

Kiintelejensia hili limekaaje?

Inanipa mashaka hata ulinzi wa viongozi hawa ambapo inawezekana Watanzania wasio wema wakaamua kuwauza ili waondoke mbele ya macho ya Watanzania wenye kuhitaji huduma zao.....
 
Serekali ya Ccm ipo uchi miaka yote,Ilivyaa nguo enzi ya mwalimu tu.Kwa sasa kwa Ccm hamna siri,tena kwa mwendo huu wa kukurupuka na kufukuza ovyo.Ndio kila kitu kitakuwa kinawekwa hadharani wao wakiamini kwao ni siri.
 
Hapo ni bandarini tu je maeneo mengine yalio kwenye fificho sikuna uozo mwingi sana! kuna Yule Waziri sijui wa nn alisema anawapa polisi sijui siku ngapi wampeleke majina yote ya wauza unga hadi Leo Sijawahi kumwona tena

Wanavyorukaruka unashindwa kujua nini kinaendelea.......kuna hao polisi......kuna wale waliopewa siku 7 kulipa kodi........
Mambo ni mengi sana......lakini hakuna kitu hata kimoja kinachofanyika....nilikuwa nasubiri siku 100 lakini zimeisha hakuna lolote........
 
Kuna kila dalili kwamba mambo hayaendi kama yanavyopaswa kwenda kwa sababu wana wa uovu wamejipanga vyema kweli kukwamisha...

Ikumbukwe Gap iliyopo baina ya walionacho na wasionacho imejengwa kwa umakini mkubwa na viongozi wetu ambao badala ya kutimiza wajibu wao walitumia ofisi za umma kujinufaisha kiasi kwamba leo tuna matajiri wa kutisha ambao kihistoria walitoka familia fukara wakaja wakawa viongozi na baada ya hapo historia ikabadilika.....

Intelejensia ijiangalie ktk hili
 
Kuna kila dalili kwamba mambo hayaendi kama yanavyopaswa kwenda kwa sababu wana wa uovu wamejipanga vyema kweli kukwamisha...

Ikumbukwe Gap iliyopo baina ya walionacho na wasionacho imejengwa kwa umakini mkubwa na viongozi wetu ambao badala ya kutimiza wajibu wao walitumia ofisi za umma kujinufaisha kiasi kwamba leo tuna matajiri wa kutisha ambao kihistoria walitoka familia fukara wakaja wakawa viongozi na baada ya hapo historia ikabadilika.....

Intelejensia ijiangalie ktk hili


nguruvi3 kila siku anahubiri mfumo humu

watu bado mnaamini kwenye 'individual brilliancy '

Kungekuwa na mfumo waziri mkuu wala asingekwenda bandarini
ingejulikana meter ni mbovu na mhusika mzembe
 
Kila sehemu ni jipu tena makubwa haswa mtumbuaji anatakiwa kujipanga la sivyo kabla hajaanza kutumbua linapotea baada ya muda linajitokeza sehemu nyingine ulishawahi fikwa na jipu la namna hiyo
 
Wanavyorukaruka unashindwa kujua nini kinaendelea.......kuna hao polisi......kuna wale waliopewa siku 7 kulipa kodi........
Mambo ni mengi sana......lakini hakuna kitu hata kimoja kinachofanyika....nilikuwa nasubiri siku 100 lakini zimeisha hakuna lolote........
Na walivokuwa wakisema CCM ni ile ile wewe ulielewa nini?

Wamejipangaaaa.....
 
nguruvi3 kila siku anahubiri mfumo humu

watu bado mnaamini kwenye 'individual brilliancy '

Kungekuwa na mfumo waziri mkuu wala asingekwenda bandarini
ingejulikana meter ni mbovu na mhusika mzembe
Ndio hapo sasa....
Waziri Mkuu anasafisha bandari na TRA
Rais anasafisha Muhimbili
Makamu wa Rais anamwakilisha Rais kwenye mialiko
Mawaziri na Wakuu wa Wilaya wanafanya ziara za kustukiza....
Manaibu mawaziri wanafungia wachelewaji mageti

Huko kwenye uozo uliotukuka ....TAMISEMI sijui nani ataenda huko......
 
Bado naitafakari ile single maarufu ''MTAISOMA NAMBA'', walimaanisha kweli, aseeee!
 
Kuna majizi huwa tunayataja humu kila siku JPM hasikii, sasa tumsaidiaje? Kuna majitu yamekubuhu kwa rushwa na figisu, lipo li Mwakyembe, kuna Li Muhongo, Kuna li Simbachawene, kuna li kipara februari marope. Ukiwa na haya majitu kwenye baraza la mawaziri tegemea hujuma kila dakika. Ni majitu ya figisu. Acha raisi wangu JPM avune alichopanda
 
Kuna majizi huwa tunayataja humu kila siku JPM hasikii, sasa tumsaidiaje? Kuna majitu yamekubuhu kwa rushwa na figisu, lipo li Mwakyembe, kuna Li Muhongo, Kuna li Simbachawene, kuna li kipara februari marope. Ukiwa na haya majitu kwenye baraza la mawaziri tegemea hujuma kila dakika. Ni majitu ya figisu. Acha raisi wangu JPM avune alichopanda

hahh hahha .
 
Mbona hata Kagame kasema bandari ya Dar pekee inatosha kwa Tanzania. Mkuu pengine hii nchi tumkodishe Kagame aje atufundishe maendeleo!
Mkuu ni kweli km ingekuwa inawezekana tungefanya hivyo hata kwa mwaka mmoja tu, aiseee Ng'ombe wa masikini hazai, kwa Mara ingine thabitisha huu msemo,
 
Back
Top Bottom